Ndugu wanaJF, kwenye kipindi cha Usiku wa Habari kinachorushwa na TBC1 kuanzia saa 5 usiku, kuna mfanyabishara mmoja Kariakoo (leo Julai 4) alikuwa akidai amenunua maji feki (yanayo fanana na yale ya kiwandani na yanatumia nembo ya Maji ya Uhai) na wateja waliyoyatumia walilalamika kuwa siyo salama (walianza kuumwa matumbo baada ya kuyatumia) na walipofuatilia waligundua kuwa ni maji yaliyochakachuliwa na matapeli ya mjini.Jamani haya matapeli yatatumaliza kwa sababu ya kuabudu mali na kutaka utajiri wa harakaharaka! Kuna matapeli nayouza dawa feki na vyakula feki (ikiwa ni pamoja na mayai feki, maziwa feki, mafuta ya kupikia feki). Kuna tuhuma pia kuwa matapeli mengine yanawawapa kuku wa kienyeji na wa kigeni madawa wanayotumia watu wanaoishi na virusi vya ukimwi ili wanenepe au madawa mengine ambayo hayastahili kuwapa kuku au mifugo tunayotumia kama kitoweo.Huku kupenda hela kupita kiasi kumetoka wapi?