Habari mpya na njema katikati ya janga la Covid-19

Togolani, upo sahihi kwa kiwango kikubwa, ila napingana na wewe kwakutokuwa muwazi sana kwa kuinyooshea serikali moja kwa moja na badala yake umegusa na mtu mmoja mmoja.

Sheria zinazowekwa na serikali na bunge letu ni kandamizi sana.
Na hii inatokana na tuliowaamini kuwa wameelimika na kuishi dunia ya kwanza kielimu au ya pili, tukawapa madaraka kutuongoza(kumbe hawajaelimika)
ndiyo waliotufikisha hapa.
Wamezoea kutambika tu na siyo kuiishi elimu waliyosoma.
Tafiti zako fanyia pia wakati ujao wa uchaguzi kama utakuwepo, utaona wanavyopishana kwa waganga wa kienyeji.
Watu kama hao utegemee wataleta sheria wenzeshi kwenye tafiti za kulisaidia taaifa?

Serikali ya uingereza imetoa billions kufadhiri tafiti siyo mtu Brother.

Sent using Jamii Forums mobile app

Ndugu nguruka wa kig0ma, sijailamu serikali moja kwa moja kwa kuwa hiyo haikua msingi wa hoja yangu. Hoja yangu ni kuonesha msingi wa tatizo. Siku zote naamini serikali na vyombo vingine tulivyo navyo ni reflection yetu sisi. Wanaoongoza wanatoka kwenye jamii hivyo wanayofanya, kusema, kusimamia, na kuweka kama vipaumbele kwa sehemu kubwa ni yale yaliyoko kwenye jamii. Hivyo kama tunataka kujadili tatizo kisayansi, lazima tupanue macho kutazama angles zote za tatizo badala ya kuirushia mawe serikali pekee.

Ukitaka kuelewa msingi wa hoja yangu jiulize kama shida ni serikali pekee, kwa nini wabunge nao walikubaliana na hoja za serikali? Wangetakiwa kuikataa sheria kama sio nzuri. Pili, jiulize kwa nini wabunge hawahawa wanaopitisha sheria hizihizi unazoona zina shida, wanaendelea kuchaghuliwa na wananchi kila mara?

JIBU: tatizo sio wabunge wala serikali. Wao ni matokeo tu. Tatizo ni mfumo mzima unaozalisha walio kwenye hizo nafasi tukianza na mimi na wewe. Hivyo kama tunataka mabadiliko ya kweli na endelevu, tuanzie chini na sio juu.

MM
 
Chuo chetu kikuu cha Dar kilifunguliwa rasmi 1961 kikiwa chini ya University of London
Sasa kama ni hivyo huku kwa miaka zaidi ya 50 tumeshindwa hata kutengeneza dawa ya kumaliza kunguni au mbu
Kweli inatakiwa hela ndefu kwa utafiti lakini hiyo ni sababu ndogo sana kama tunataka tuwe wabora kama mfunguzi wetu wa London
Tulikwama wapi?
Rais ajae nasema awekeze kwenye utafiti kama huyu alivyowekeza kwenye ndege


Sent from my iPhone using Tapatalk

Kwa kauli yako nina hakika huna ufahamu wa tafiti na gunduzi za zinazofanywa na UDSM. Ukifanya homework, utarudi hapa kuomba radhi. Ila ninasita kukulaumu maana tayari nilishasema mwanzoni tuna tatizo kubwa na mfumo wetu wa utoaji na upashanaji habari za mambo muhim.

MM
 
Nakubaliana na wewe Pascal!
Madawa ya nchi za Waafrika tuna dawa nyingi za Asili ambazo zinatibu magonjwa mbalimbali.
Tatizo lililopo ni Taasisi zinazosimamia Waganga wa tiba za Asili.
Nazungumzia National Institute for Medical Research (NIMR).
Hivi NIMR toka imeanzishwa kuna dawa gani ambayo wameithibitisha na Ku ibrand kutoka kwa Waganga wa tiba za Asili
 
Fo
Ndugu wana JF,

Kumekua na tafiti kadhaa za kisayansi sehemu mbalimbali duniani (hasa katika vyuo vikuu na taasisi nyingine za tafiti za tiba) zilizoanza ndani ya miezi michache iliyopita, zikitafuta chanjo na/au tiba ya Covid-19. Wako binadamu wenzentu wamekua wakikesha maabara na kwenye vitabu kwa miezi kadhaa sasa wakitafuta namna dunia itasaidika na janga hili. Kwa wale ambao wamejikita katika kusikiliza na kuamini masimulizi, uongo na porojo za nadharia njama juu ya chanzo cha Covid-19 na kinachoitwa mbinu ya kutengeneza chanjo/kinga itakayowaweka watu alama, wanaweza wasiwe na uelewa wa kinachoendelea.

Mbili kati ya tafiti zinazofanyika ni za nchini Uingereza. Moja inafanywa na Chuo Kikuu cha Imperial College London na nyingine inafanywa na watafiti walioko Chuo Kikuu cha Oxford. Ingawa ni ndani ya miezi michache, lakini tafiti hizi mbili zimeshaonesha mafanikio makubwa na sasa ziko kiwango cha majaribio ya kitafiti yajulikanayo kama Clinical Trials.

Nini maana ya clinical trials?
Clinical trials ni aina za tafiti za tiba (biomedical research) zinazolenga kugundua tiba au kinga mpya ya magonjwa au hali nyingine za kiafya ikiwa ni pamoja za matatizo ya kisaikolojia. Wanasayansi wanapotafuta kutenegeza dawa au tiba (kama ilivyo sasa kwa ajili ya Covid-19), wanaanza na tafiti za kimaabara ambazo zinaweza kuwa za kikemikali au kibayolojia. Wakifikia hatua ambayo walichokitengeneza kinaonesha dalili ya kuwa dawa au kinga, ni lazima wakifanyie majaribio kwenye viumbe hai. Majaribio hayo yanalenga mambo mawili makuu: moja kupima uwezo wa tiba au chanjo kufanya kilichokusudiwa, na mbili kupima madhara ya dawa au chanjo husika na kutafuta njia za kuyaondoa kwa kuboresha dawa au chanjo husika.

Kutegemeana na dawa wanayoitengeneza, clinical tirials huanza na wanyama wadogo kama panya au chura. Zinaponesha mafanikio, majaribio yanakwenda ngazi nyingine ambayo huusisha wanyama wakubwa na ambao biolojia ya miili yao inakaribiana na ya binadamu. Wakivuka hatua hiyo, majaribio mengine yanafanyika kwa watu wachache kwa kuzingatia umri, jinsia, mazingira, majukumu, magonjwa, na mambo mengine yatakayoonekana ni muhim kuchunguzwa kwa dawa na ugonjwa husika. Hatua hii ikionesha mafanikio, majaribio yanakwenda hatua nyingine kubwa zaidi ambayo ni kujaribisha dawa au kinga husika kwa watu wengi au kwenye eneo kubwa na kufutilia kwa karibu matokeo yake. Matokeo yakiwa mazuri, basi dawa au chanjo husika huanza kutengenezwa kwa wingi kwa ajili ya kutumiwa na wanadamu. Mchakao wote huu ndio huiwa CLINICAL TRIAL.

View attachment 1426071
Clinical trials huchukua muda gani?
Kwa kawaida Clinical Trials huchukua muda mrefu na kuna taasisi nyingi zinazoratibu na kusimamia michakato yake ili kuhakikisha kinachotengenezwa hakiendi kuwa na madhara kitakapoanza kutumika na kama ni lazima kiwe na madhara basi yasiwe na athari kubwa au za kudumu. Ndio mana kila dawa ina maelezo yanayoshauri ni watu gani wanaweza kuitumia au hawatakiwi kuitumia. Pia inaoanisha aina ya madhara (side effect) unayoweza kupata unapoitumia. Kwenye mchakato wa clinical trials, iwapo katika hatua yoyote ile matokeo yataonekana sio mazuri, watafiti watarudi maabara na kufanya marekebisho. Wakimaliza, wanaanza tena pale walipokwamia. Hii ndio mana mchakato wa kutengeneza dawa au kinga (na hasa kama ni ya tatizo jipya kama la Covid-19), huweza kuchukua miaka miwili na zaidi. Watafiti wa madawa walisema iwapo kinga ya Covid-19 itapatikana mapema basi itakua ni angalau baada ya miezi 18 (mwishoni mwa 2021).

Habari njema za kinga ya Covid-19
Utafiti unaofanywa na chuo kikuu cha Oxford, umekua na mafanikio makubwa na ya haraka. Wameweza kupitia hatua za awali za mchakato wa clinical trials (fast tracking) na matokeo yamekua mazuri. Hivyo basi, kesho Alhamis ya terehe 23/04/2020 wanaanza rasmi hatua ya kwanza ya kujaribisha uwezo na usalama wa chanjo ya Covid-19 kwa kutumia binadamu. Haya ni mafaniko makubwa na ya kufurahisha sana. Kwa wale waliokua wanaombea wanasayansi duniani kama mimi ili wafanikiwe kuja na majawabu ya Covid-19, habari hizi zinadhihirisha Mungu anasikia maombi yetu. Hivyo tuendelee kuombea hatua za majaribio zitakazoanza ili nazo zifanikiwe bila changamoto nyingi.

Siku ya jana serikali ya Uingereza imetoa kiwango cha takribani shilingi Bilioni 130 kufadhili tafiti hizi mbili katika hatua zilizobaki. Pia imeanza kufanya maandalizi ya kutengeneza chanjo hii kwa wingi ili majaribio yatakapomalizika tu, ianze kuzalishwa na kusambazwa duniani kadiri ya mahitaji.

Kwa nini Oxford na Imperial College London wameweza kufanya majaribio haya kwa haraka?
Watu wengi wanaweza kuwa na maswali au hofu juu ya usalama wa chanjo zinazofanyiwa majaribio sasa kwa kuwa umetumika muda mfupi. Hofu hizi ni halali kabisa kwa mtu yoyote yule. Ila yako mazingira yanayowezesha tafiti ngumu na za muda mrefu kufanyika ndani ya muda mfupi. Nitaje mambo mawili:

  • Historia ya dunia inatuonesha kwamba gunduzi nyingi kumbwa na ngumu zilifanyika nyakati za majanga au hali ngumu kama vile vita ya kwanza na ya pili ya dunia; vita baridi kati ya Ubepari na Usoshalilisti; na wakati ambapo maendeleo ya mwanadamu yalifanyika haraka na kusababisha mahitaji mengi na makubwa kama wakati vile mapinduzi ya viwanda kule Ulaya.
Katika muktadha wa kitafiti hasa kwa vyuo vikuu, gunduzi zinaweza kufanyika kwa haraka kutokana na mambo kadhaa.
  • Vyuo vikuu kuwa na msingi mzuri wa tafiti za kisayansi kwa maana ya kusomesha watafiti wengi na bora; kuwa ma maabara za kisasa zenye vifaa na madawa ya kutosha; na kuwa na raslimali fedha.
  • Vyuo, taasisi na vitengo vyake kuongozwa kisayansi na viongozi kupatikana kwa mchujo wa wazi na wenye kuzingatia tija, uwezo, uzoefu, ubunifu, na mafanikio ya wanaopewa nafasi.
  • Kuwa na miradi mukubwa na endelevu ya kitafiti kwa kushirikiana na serikali na sekta binafsi.
  • Serikali kuheshimu nafasi ya tafiti za kisayansi na teknolojia kama msingi wa kutatua changamoto za kila siku na za muda mrefu za kijamii, uchumi na maendeleo.
  • Serikali kuthamini na kuheshimu watafiti, ikiwa ni pamoja na kuvipa uhuru vyuo vikuu kufanya kazi zake bila kuingiliwa na siasa hata wanapofanya makosa. Pia, kuwapa watafiti uhuru wa kutoa mawazo yao bila kujali wanafanya hivyo kwa lengo la kushauri, kuchambua, kuleta fikra chokonozi, kuboresha jambo, au kukosoa na kuonesha madhaifu.
  • Kuwa na msingi wa jamii inayoheshimu elimu, taaluma, utaalamu, na sayansi.
  • Kuwa na miundombinu wezeshi, imara na ya kuaminika. Watafiti wa wa vyuo vya UK, hawana hofu ya kukatika wala kutingishika kwa umeme au internet kwa mwaka mzima; hivyo wanaweza kufanya kazi siku na muda wowote.
Mambo niliyotaja hapa juu (huenda na mengine) huwezesha watafiti walio vyuo vikuu kuwa na msingi na mbinu za kuvamia tafiri au tatizo au changamoto mpya za kisayansi bila kupoteza muda mwingi wa kufanya maandalizi na kutafuta rasilimali. Kunakua ta msingi imara unaowawezesha kupandisha tofali kwa haraka na kumaliza ujenzi. Pia, mambo haya huwapa ujasiri kwamba iwapo watahitaji rasilimali serikali ya mashirika binafsi itasikiliza na kuingilia kati.

Mwisho
Moja (this is serious), wale wanaofanya maombi kuombea wanasayansi/watafiti kote duniani, tafadhali tuongeze bidii maana kuna mwangau unaonekana kwamba tunaweza (wanadamu) kupambana na Covid-19 tukaishinda kama tulivyoshinda magonjwa mengine mengi.

Pili (Sarcasm), tafadhali usiache kuwashikirisha habari hizi njema wale ambao wameaminishwa nadharia njama na porojo kwamba kuna chanjo za kidigitali zinatengenezwa na kina Bill Gates ili wazitumie pamoja na 5G kutawala dunia. Wahakikishie kwamba, kwa neema ya Mungu, siku sio nyingi tutakua na chanjo ya kudhibiti Covid-19 na maisha yataendelea kwa wale watakaokua wamesalimika na kirusi Korona. Nina imani nao pia watapanga foleni bila kulazimishwa kupata chanjo pale itakapobidi kujikinga.


Imeandikwa na: Mathew Mndeme (mmtogolani@gmail.com)
Mwanasayansi/Mtafiti wa Mifumo ya Digitali katika Ufuatiliaji na Udhibiti wa Magonjwa

Rejea:

For the first time in so many days I feel a little bit safe. Thank you for this good information on the trials being done by our colleagues in other parts of the World. We also have Research Institutes in our country. One of them is Ifakara Health Institute based in Ifakara and Bagamoyo. Not many of us know what is going on there, but our fellow researchers outside the country appreciate and funds most of these researches. They know how important these are in terms of human health but unfortunately we, as a country, do not appreciate what is being done there.
 
Nakubaliana na wewe Pascal!
nchi zetu za Afrika tuna dawa nyingi za Asili ambazo zinatibu magonjwa mbalimbali.
Tatizo lililopo ni Taasisi zinazosimamia tafiti zitokanazo na tiba za Asili.
Nazungumzia NIMR.
Hivi NIMR toka imeanzishwa kuna dawa gani ambayo wameithibitisha na Ku ibrand kutoka kwa Waganga wa tiba za Asili
 
Kumjua mungu ni kuzuri sana,
Unamtaja Mungu kwa kinywa chako lakini moyo wako uko mbali naye.

Hii unataka kutuaminisha kuwa kauli ya Mtukufu wako kuwa siku3 tumwombe mungu imefanikiwa!!!

1. Mlimwomba mungu atuondolee corona na siyo atupe chanjo au dawa.
2. Ningeamini kama ugunduzi wa chanjo au kinga mungu angeufunua hapahapa tanzani.
MAWALI.

Kwanini maombi yakajibiwe ulaya na si kuliko fanyikia maombi?

Kwani mungu anashindwa kuikomesha corona kwa uweza na nguvu zake bila dawa kama alivyoikomesha tauni wakati wa mfalme Daudi,alipofanya maombi kwenye kiwanja cha Arauna tauni ilikoma mara mojai? ( maombi yenu hayajafika,tusubiri yafike)

Watu tulipiga kelele humu kuwa Mungu ametupa akili nguvu na maarifa, alitaka tuvitumie ivyo kwa ajili ya maisha haya.
Mbona hamjaomba kwa ajili ya malaria, ukimwi, polio, nk
Mbona hamkuomba magovi yaondoke kwa wasio tahiriwa ili kupunguza maambukizi ya ukimwi badala yake mnazunguka nchi nzima kuwakata watu bure?

WATU WANGU WANAPOTE KWA KUKOSA MAARIFA, ASEMA BWANA WA MAJESHI.
Badala ya kufunga mipaka mapema ili adui asiingie,mkaacha mipaka wazi kwa uroho wa vipande therathini vya fedha kama yuda aliyemsalitu Yesu.

Mmetusaliti watanzania kwa vipande vya fedha,dhambi hii itawatafuna mpk kizazi chenu cha kumi,labda muitubie.

Mbona mlishindwa kumwomba mungu Corona isiingie nchini?
Mnaomba wakati ugonjwa umeingia unatafuna watu!!!
Au mungu mliyemwomba anaweza kuondoa wakati umeingia na hawezi kuuzuwia usiingie?
Viongozi wa dini wanalakujibu mbele ya kiti cha huku cha mwenyezi mungu, kwakutowaambia ukweli watawala.

HAKUNA ALIYE MKUU MBIGUNI NA DUNIANI ILA MWENYEZI MUNGU ALIYE HAI, MUUMBA MBINGU NA NCHI.
Iliwapasa kuwakea watawala wanaopopotoka ktk ukweli.
Kama mpo humu, piteni hapa labla roho mtakatifu anawaonyesha kosa letu mkatubia na kuanza kusimama kwenye zamu yenu kama viongozi wa kiroho mungu amewaamini kuisimamia kweli bila woga.

Sent using Jamii Forums mobile app

Ndugu nguruka wa kig0ma , umeongelea mambo mengi ambayo nahofia ni nje ya mada hii. Ila nitaje moja kuhusu hoja ya sala. Hakuna popote nilipoongelea maombi ya siku 3 wala kuiombea Tanzania. Nimesema kwa wale waliokua wanaombea upatikanaji wa solution na kuombea wanasayansi duniani (bila kujali wako kona gani ya dunia na ni kina nani).
 
Bill gates kugundua Microsoft products alisaidiwa na serikali? Hana digrii lakini had I maprofesa wanatumia products zake

Toyota na ubunifu wake Wa magari ya Toyota alisaidiwa na serikali?

Mzee mwasapile na kikombe cha babu alisaidiwa na maabara ya serikali?

Wamasai na dawa zao za kimasai ambazo ni maarufu waisaidiwa na serikali?

Mgunduzi Wa mobile money alisaidiwa na serikali?

Ndugu YEHODAYA naomba nikujibu kwa maswali.

Moja, unaweza kwanza kuweka historia ya kila ugunduzi ulioutaja na ulivyofikia ulipofikia kisha ndio uulize hayo maswali?

Pili, dawa za kimasai ni maarufu kwa nani? Zinaitwaje?

Tatu, ungejua serikali inafanyaje kazi ku-support gunduzi zipate majina, ungeelewa kwamba hata babu wa Loliondo asingepata support ya serikali, angenyamazishwa baada ya wiki moja na mimi na wewe tusingemjua. Tuachie hapo.

Nne, kwa bahati nzuri sana nina uelewa wa kutosha kwenye historia ya mobile money kisayansi). Unaweza kunipa historia ya mobile money ilivyoanza? Unajua waliofanya huyo utafiti ni kina nani na walifadhiliwa na nani na kwa kiasi gani?

MM
 
Ndugu YEHODAYA naomba nikujibu kwa maswali.

Moja, unaweza kwanza kuweka historia ya kila ugunduzi ulioutaja na ulivyofikia ulipofikia kisha ndio uulize hayo maswali?

Pili, dawa za kimasai ni maarufu kwa nani? Zinaitwaje?

Tatu, ungejua serikali inafanyaje kazi ku-support gunduzi zipate majina, ungeelewa kwamba hata babu wa Loliondo asingepata support ya serikali, angenyamazishwa baada ya wiki moja na mimi na wewe tusingemjua. Tuachie hapo.

Nne, kwa bahati nzuri sana nina uelewa wa kutosha kwenye historia ya mobile money kisayansi). Unaweza kunipa historia ya mobile money ilivyoanza? Unajua waliofanya huyo utafiti ni kina nani na walifadhiliwa na nani na kwa kiasi gani?

MM
Kifupi nchi zetu wasomi huiangalia tu serikali ili watoke wenzetu huiona sekta binafsi ya muhimu na ndio yenye pesa na ndio hufadhili tafiti nyingi wakijua zina faida za kifedha mbeleni

Bill gates foundation kaanchia mabilioni ya dola kutafiti chanjo ya corona.Huku msomi haoni umuhimu Wa kushirikiana na private sekta kwene tafiti utasikia aah bakhresa hakusoma yule darasa la pili!!!!

Ndio maana unaona hata watu matajiri kama mengi waliona bora pesa zake awape albino na walemavu kuliko kuwapa watafiti ambao hata hicho wanachotafiti hakijulikani wala kueleweka .

Bakhresa anaona heri tu awape maskini na kujenga misikiti tu

Wasomi watafiti Wa Africa hawana uhusiano na sekta binafsi tofauti na ulaya ,marekani na Asia.
 
Fo

For the first time in so many days I feel a little bit safe. Thank you for this good information on the trials being done by our colleagues in other parts of the World. We also have Research Institutes in our country. One of them is Ifakara Health Institute based in Ifakara and Bagamoyo. Not many of us know what is going on there, but our fellow researchers outside the country appreciate and funds most of these researches. They know how important these are in terms of human health but unfortunately we, as a country, do not appreciate what is being done there.

Thank you very much ndugu KUTATABHETAKULE for helping me respond to some of the issues I've been trying to respond to. The comments in this thread (any few others I posted in the past) show that many Tanzanians don't know what our scientists are doing. They think our scientists are helpless toothless dogs.

However, the sentiments presented here can be a wake-up call to our scientific community, precisely, to rethink on how better we can engage the society in our research projects and establish effective channels for information dissemination.

MM
 
Haha Mkuu Pascal Yote tisa Kumi Kuna mtu kawaangusha ye kakimbia zakeee alijua ni yale mafua ambayo hayawapati mwishowe katutia hasara na kakimbia
No, ka kolona ni kaugonjwa kadogo tuu hakawezi kukimbiza watu wetu!. Kule watu tuko zetu vacation, hatuwezi kukatisha vacation zetu kwasababu ya kaugonjwa kadogo tu ka kolona!.
P
 
Kifupi nchi zetu wasomi huiangalia tu serikali ili watoke wenzetu huiona sekta binafsi ya muhimu na ndio yenye pesa na ndio hufadhili tafiti nyingi wakijua zina faida za kifedha mbeleni

Bill gates foundation kaanchia mabilioni ya dola kutafiti chanjo ya corona.Huku msomi haoni umuhimu Wa kushirikiana na private sekta kwene tafiti utasikia aah bakhresa hakusoma yule darasa la pili!!!!

Ndio maana unaona hata watu matajiri kama mengi waliona bora pesa zake awape albino na walemavu kuliko kuwapa watafiti ambao hata hicho wanachotafiti hakijulikani wala kueleweka .

Bakhresa anaona heri tu awape maskini na kujenga misikiti tu

Wasomi watafiti Wa Africa hawana uhusiano na sekta binafsi tofauti na ulaya ,marekani na Asia.
Ndugu YEHODAYA kwenye hili uko sahihi kwa sehemu kubwa. Ila nikuhakikishie wasomi wetu (hawa wa chuo che UDSM ninapofanya kazi) wengi wanafanya tafiti nyingi zinazofadhliwa na sekta binafsi. Hawategemei sana serikali.

Ulichoshauri kuhusu ushirika na sekta binafsi nalo ni la msingi sana. Ila kwa uzoefu tu nikujulishe kwamba shida sio wasomi tu bali sekta binafsi pia. Ukipeleka proposal ya research kweney kampuni (say ya telecom) na msanii fulani akapeleka ya kufanya tamasha ambalo gharama yake ni mara 10 ya uliyoomba wewe kwa utafiti, wanaweza kumsikiliza yeye wewe wasikujibu. Mifumo yao ya research and development bado ni hafifu sana na hawatazami vyuo vyuo vikuu kama ni washika muhim wa kuendeleza kazi zao.

Ndio mana nimesema, bado tuna safari ndefu ya kubadili mifumo maana haya tunayoona ni matokeo ya mifumo ya elimu na kijamii tuliyonayo.

MM
 
Ndugu YEHODAYA kwenye hili uko sahihi kwa sehemu kubwa. Ila nikuhakikishie wasomi wetu (hawa wa chuo che UDSM ninapofanya kazi) wengi wanafanya tafiti nyingi zinazofadhliwa na sekta binafsi. Hawategemei sana serikali.

Ulichoshauri kuhusu ushirika na sekta binafsi nalo ni la msingi sana. Ila kwa uzoefu tu nikujulishe kwamba shida sio wasomi tu bali sekta binafsi pia. Ukipeleka proposal ya research kweney kampuni (say ya telecom) na msanii fulani akapeleka ya kufanya tamasha ambalo gharama yake ni mara 10 ya uliyoomba wewe kwa utafiti, wanaweza kumsikiliza yeye wewe wasikujibu. Mifumo yao ya research and development bado ni hafifu sana na hawatazami vyuo vyuo vikuu kama ni washika muhim wa kuendeleza kazi zao.

Ndio mana nimesema, bado tuna safari ndefu ya kubadili mifumo maana haya tunayoona ni matokeo ya mifumo ya elimu na kijamii tuliyonayo.

MM
Nafikiri ujengaji hoja kwenye proposal muhimu msanii aweza waambia Mimi Nina wapenzi wengi iwe Facebook I,Instagram, blog nk nitumie nikuongezee makert share na wateja sasa mtafiti utafiti wako unaisaidiaje kampuni kupata pesa nyingi now or in future kwenye proposal yako? Usilaumu tu private sekta

Na ukiona wanaona msanii ni more important kuliko mtafiti msomi do your research why proposal yako ikataliwe ashinde msanii usije na jibu rahisi kwenye swali gumu

Vyuo ndio vibadlili mitizamo iendane na sekta binafsi

Tafiti zinatakiwa zijibu matarajio ya sekta binafsi sio ya vyuo !!!!!
 
Kwa kauli yako nina hakika huna ufahamu wa tafiti na gunduzi za zinazofanywa na UDSM. Ukifanya homework, utarudi hapa kuomba radhi. Ila ninasita kukulaumu maana tayari nilishasema mwanzoni tuna tatizo kubwa na mfumo wetu wa utoaji na upashanaji habari za mambo muhim.

MM

Wala usinilaumu maana mnajua mnakwama wapi
Ni hapo kwenye mambo muhimu na upatikanaji wa habari
Kama tafiti na gunduzi zingekuwa zinaandikwa kwenye magazeti au mitandaoni tusingebeza na kuongea lolote
Nisamehe bure


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Back
Top Bottom