Gwajima na Manji wananikumbusha yaliyotokea nchini Jamaica

Ujinga ni kitu kimoja kibaya sana....Nakumbuka jinsi Dudus alivyokuwwa anatumia watu wake kuua watu ili amiliki biashara ya unga peke huku akisaidia hao mambumbumbu/misukule mahitaji yao. Ikumbukwe, Dudus alikuwa anasomesha watoto wa hawa misukule yake, alilipa kodi za nyumba kwa baadhi ya misukule yake ambao walikuwa hawana uwezo wowote (unemployed na illiterate), kuwapa food rations, na vinginevyo kama alivyosem mleta mada. Ile misukule ya Dudus haikujali kuwa Lord wao anaua watu kujinufaisha yeye lakini walikuwa radhi kumtetea, kisa wanasaidiwa na jangili. Tuje sasa kwa hawa Gwajima na Manji....hawa jamaa ni watuhumiwa tu japo kuna taarifa chini ya zuria kuwa Gwajima kwa muda mrefu anashughulisha na hii biashara ya uuzaji unga, I can confirm kuwa ni habari ya ukweli kwa sababu aliyesema alikuwa kwenye ule mtandao na alikuwa na wadhifa fulani. Waumi wake wengi walimtoroka baada ya kupata taarifa zake including my own brother. Kama nilivyosema kwenye ufunguzi kuwa ni ujinga, haiwezekani mtu mwenye akili timamu kumsindikiza Gwajima au Manji mahakamani ikiwa anaangamiza jamii. Hata kama anakulipia pango la nyumba au kukuchapia mkeo (kama Flora Mbasha) kusingizia anampa fadhila za kiroho, huu ni ujinga na misukule wa namna hii pia ni janga la taifa kwani wanafuga maradhi ndani ya jamii.
 
Kwa hiyo wewe ushauri wako ni nini.?
Ushauri gani utolewe, wakati vita iliyoanzishwa na RC Makonda ina mbinu na mikakati madhubuti ambayo ni mipya kabisa, kiserikali, duniani kote.

Gwajima au Manji kama wanahusika, kwa njia moja au nyingine, ni bora watoe ushirikiano usio na masharti kwa Serikali.

Waheshimiwa Wabunge, na wao kama wanahusika, kwa njia moja au nyingine, wajisalimishe, badala ya kujificha mjengoni kwa kinga yake.

Watanzania, wenye taarifa dhabiti, tutoe ushirikiano kwenye vita hii. Kwani fedha za hayo madawa ndizo zinazochangia, kwa hali ya juu, maelewano mabaya kisiasa, nchini.

.
 
MsemajiUkweli

There was an arrest warrant for Dudus.

There is no arrest warrant for Manji nor Gwajima. There is no evidence produced by Makonda/Sirro to indict the two in drug related charges.

On the other hand Makonda has publicly named to two (and many others) to have been said to be dealing and/or abusing drugs without a shred of evidence.

In this sense, your thread is the case of oranges and mangoes. Lakini kuna wenye uelewa mfinyu watakusifu na ujinga huu.

Makonda kama kweli anapambana na madawa ya kulevya asisumbue watu kwa kuwachafua bila ushahidi. Akusanye ushahidi, awashike na mawakili wa serikali wafungue kesi mahakamani ili watu hawa waadhibiwe immediately.

Haya maigizo ya kutoka na majina huku huna ushahidi wowote mwisho wake vita nzima itaonekana haina seriousness na waliotajwa wanaweza kuishtaki ofisi ya mkuu wa mkoa kwa kuchafuliwa majina yao. Kodi zetu zitatumika kuwalipa.

Tusifanye mambo kishabiki na kipuuzi. The Government has intelligent resources to deal with the matter but not in this way.
Huo ndio ukweli. Eti unaita waandishi wa habari na kutangaza list ya wafanyabiashara wa mihadarati, kweli?? Kitendo hicho peke yake kinaonesha kesi hamna. Mr. X anauza mihadarati arrest warrant hapohapo, kusanya vielelezo (ushahidi), peleka mahakamani. Hivi mkuu hata ingekuwa wahusika ni kweli wanauza mihadarati ukiwatangaza kwenye vyombo vya habari tena ukawapa na muda wa kwenda polisi, unategemea kuna kitu utakamata kweli? Labda kama na wao wanajidunga ndio utakuta wamezubaa kiasi hicho. Waulizeni Wamarekani vita yao waliyoanzisha mwaka 1971 chini Richard Nixon, hivi leo wamepiga hatua gani kama sio "mark time" Binafsi nakubali vita tupige lakini kwa staili hii tunataniana tu.
 
Hawa jamaa Mchungaji na Mfanyabiashara wanashindwa kusoma nyakati walizoea awamu iliyopita mtu anatukuzwa kwa Pesa na kufadhili watu, Wakati huu watu wote sawa hakuna mwenye thamani zaidi au heshima zaidi. Kama utajiri wao unategemea unga mambo yanajulikana, Makonda kuwaweka wazi itawafanya vijana wajitafakari upya kuhusu kujenga maisha, hawa role models kama wanauza madawa ni vyema jamii tufahamu,


Tunataka Tanzania yenye heshima na adabu....mimi bado nashangaa tu kwa nini Ridhiwani, Kinjeketile, Jo Kusaga, Ruge Mutahaba, kukamatwa. Marehemu Mangwea aliwalalamikia sana hawa kina Kusaga na mchezo wao mchafu kabla ya kifo chake. Sote twaelewa, panapofuka moshi lazima....!
 
Ushauri gani utolewe, wakati vita iliyoanzishwa na RC Makonda ina mbinu na mikakati madhubuti ambayo ni mipya kabisa, kiserikali, duniani kote.

Gwajima au Manji kama wanahusika, kwa njia moja au nyingine, ni bora watoe ushirikiano usio na masharti kwa Serikali.

Waheshimiwa Wabunge, na wao kama wanahusika, kwa njia moja au nyingine, wajisalimishe, badala ya kujificha mjengoni kwa kinga yake.

Watanzania, wenye taarifa dhabiti, tutoe ushirikiano kwenye vita hii. Kwani fedha za hayo madawa ndizo zinazochangia, kwa hali ya juu, maelewano mabaya kisiasa, nchini.

.


Una akili sana wewe pia unaonyesha jinsi ulivyo na uchungu na nchi yako. Big up.
 
kw kweli mi nashindwa kuelewa kwa nini mambo yao binafisi wayanasibiashe na watu wengine?mi ni shabiki mstaafu lkn siungi mkono kbs hayo mambo yao km wana msala ni bora wawashirikishe gamilia zao lkn sio sisi bana
Wanafahamu hiyo ni silaha mathubuti katika kuficha maovu au kupambana na dola katika mahakama ya public opinion.
 
Siungi mkono uuzwaji wa madawa,ila makondakta ajue kwamba kuna nguvu ya pesa,amezidi kukurupuka na kutaka sifa za kijinga
 
Yaani unashindwa kuelewa kuwa unapomtuhumu Gwajima mojakwamoja umewagusa waumini wake.
Unaweza kumtofautishaje kati ya Gwajima na kanisa lake LA Ufufuo?
Kanuni moja wapo ya kanisa ni kusaidiana kwa shida na raha
HivyoGwajima kwa sasa yuko ktk shida hivyo wamsapoti kwa nguvu zote
Mfano ukimtaja Pengo huwezi kumtofautisha na kanisa la RC lazima wajitolee kumsaidia.
Anashindwa kufahamu kwamba kanisa nalo ni taasisi
 
A so called "IMANI" ni heroine tosha, huyo "askofu wako" kawafanya misukule...... bila shaka ulikuwepo pale na suti yako.
Wewe uelewa wako ni mdogo sana. Hivi kwa kuwa makonda katamka, tayari askofu ni mhalifu? Hivi nyie uvccm huwa mnafundishwa nini? Halafu utakuta na wewe eti umepitia shule with such a poor reasoning capacity, hopeless.
 
Huo ndio ukweli. Eti unaita waandishi wa habari na kutangaza list ya wafanyabiashara wa mihadarati, kweli?? Kitendo hicho peke yake kinaonesha kesi hamna. Mr. X anauza mihadarati arrest warrant hapohapo, kusanya vielelezo (ushahidi), peleka mahakamani. Hivi mkuu hata ingekuwa wahusika ni kweli wanauza mihadarati ukiwatangaza kwenye vyombo vya habari tena ukawapa na muda wa kwenda polisi, unategemea kuna kitu utakamata kweli? Labda kama na wao wanajidunga ndio utakuta wamezubaa kiasi hicho. Waulizeni Wamarekani vita yao waliyoanzisha mwaka 1971 chini Richard Nixon, hivi leo wamepiga hatua gani kama sio "mark time" Binafsi nakubali vita tupige lakini kwa staili hii tunataniana tu.
Wewe, na wenye mawazo kama yako unataka zitumike mbinu gani katika vita hii!

Hivi unadhani na kuamini RC Makonda anakurupuka, na atashikishwa adabu. Kwa nini tusiamini pia kuwa ana ushahidi dhidi ya wahusika wa madawa ya kulevya, kiasi cha kuwa jasiri kuwataja hadharani!

Hao waliotajwa wameombwa kwenda kutoa ushirikiano, na wala hawajahusishwa na kuhusika kwao moja moja. Watamchukulia hatua gani ya kisheria? Kama hawahusiki, kiherehere cha nini!!!
 
Kujenga mtandao wa watetezi ni sifa kuu ya watu wanaofanya biashara zilizo kinyume ya sheria, maadili ya kibinadamu au udanganyifu katika nchi masikini.

Ikumbukwe kuwa kuna umasikini wa aina mbili ambao ni elimu na fedha. Ndani ya umasikini wa elimu kuna umasikini wa mawazo.

Hakuna umasikini mbaya kama umasikini wa mawazo kwa maana kwamba, hakuna kitu kibaya kama kuikabidhi akili yako kwa mtu mwingine huku pia ukisumbuliwa na njaa na maradhi.

Mjamaica aitwaye Christopher "Dudus" Coke aliweza kutumia umasikini wa wananchi wa Jamaica kujijenga na kupendwa kutokana na kutoa huduma mbali mbali za kijamii kama kutoa chakula, elimu na afya kwa wananchi kutokana na serikali kushindwa kutoa huduma hizo. Pesa za kugharamia huduma hizo alizipata kutokana na biashara ya kuuza madawa ya kulevya.

Wananchi walimpenda sana kiasi kwamba hata serikali ilishindwa kupambana naye kwa sababu hata Waziri Mkuu wa nchi hiyo alitokea jimbo la huyo mfanya biashara wa madawa ya kulevya.

Wananchi hawakuliona tatizo la Christopher "Dudus" Coke kuuza madawa kwa sababu aliwasaidia kuwapa huduma muhimu za kijamii.

Mfanyabiashara huyo alihakikisha anajenga mtandao ndani ya serikali na chama tawala na pia aliweza kuvizibiti vyombo vya habari.

Serikali ya Marekani ilifikia hatua ya kutoa vitisho kwa viongozi wa Jamaica wamkamate kwa sababu anahitajiwa kwenda kujibu mashitaka nchini Marekani.

Jeshi la Jamaica lilipojaribu kwenda kumkamata lilikuta wananchi kwa maelfu wameizunguka nyumba yake usiku na mchana wakiwa tayari kufa kwa ajili yake. Mapambano yalisababisha zaidi ya wananchi 30 kupoteza maisha.

Ukisikiliza Press Conference za Gwajima na Manji utagundua kuwa wanatumia njia hiyo hiyo kama aliyotumia Christopher "Dudus" Coke.

Manji anataka suala lake binafsi liwe ni suala la mashabiki na wapenzi wa Yanga kwa sababu anaisaidia Yanga kifedha. Manji anajaribu kuhakikisha vyombo vya habari vinaandika kile anachokitaka.

Gwajima anataka suala lake binafsi liwe ni suala la waumini wa kanisa la Ufufuo na Uzima kwa sababu anatoa huduma za kiroho na kifedha kwa waumini wake.

Tumeona Manji akiongozana polisi na kundi la mashabiki na wapenzi wa klabu ya Yanga.

Tumemuona Gwajima akiongozana polisi na kundi la waumini wa Kanisa la Ufufuo na Uzima.

Kwa mpango huu, Manji na Gwajima wanaweza kufanikiwa kwa sababu ya umasikini wa elimu na fedha uliotamalaki nchini.

Je, serikali imejiandaa kwa kiwango kipi katika mapambano yaliyo mbele yake?

A Chinese military general, strategist and philosopher, Sun Tzu once said, If you know the enemy and know yourself, you need not fear the result of a hundred battles. If you know yourself but not the enemy, for every victory gained you will also suffer a defeat. If you know neither the enemy nor yourself, you will succumb in every battle.
Hamna enemy mbaya Kama Yule aliyeenda underground.
 
Kujenga mtandao wa watetezi ni sifa kuu ya watu wanaofanya biashara zilizo kinyume ya sheria, maadili ya kibinadamu au udanganyifu katika nchi masikini.

Ikumbukwe kuwa kuna umasikini wa aina mbili ambao ni elimu na fedha. Ndani ya umasikini wa elimu kuna umasikini wa mawazo.

Hakuna umasikini mbaya kama umasikini wa mawazo kwa maana kwamba, hakuna kitu kibaya kama kuikabidhi akili yako kwa mtu mwingine huku pia ukisumbuliwa na njaa na maradhi.

Mjamaica aitwaye Christopher "Dudus" Coke aliweza kutumia umasikini wa wananchi wa Jamaica kujijenga na kupendwa kutokana na kutoa huduma mbali mbali za kijamii kama kutoa chakula, elimu na afya kwa wananchi kutokana na serikali kushindwa kutoa huduma hizo. Pesa za kugharamia huduma hizo alizipata kutokana na biashara ya kuuza madawa ya kulevya.

Wananchi walimpenda sana kiasi kwamba hata serikali ilishindwa kupambana naye kwa sababu hata Waziri Mkuu wa nchi hiyo alitokea jimbo la huyo mfanya biashara wa madawa ya kulevya.

Wananchi hawakuliona tatizo la Christopher "Dudus" Coke kuuza madawa kwa sababu aliwasaidia kuwapa huduma muhimu za kijamii.

Mfanyabiashara huyo alihakikisha anajenga mtandao ndani ya serikali na chama tawala na pia aliweza kuvizibiti vyombo vya habari.

Serikali ya Marekani ilifikia hatua ya kutoa vitisho kwa viongozi wa Jamaica wamkamate kwa sababu anahitajiwa kwenda kujibu mashitaka nchini Marekani.

Jeshi la Jamaica lilipojaribu kwenda kumkamata lilikuta wananchi kwa maelfu wameizunguka nyumba yake usiku na mchana wakiwa tayari kufa kwa ajili yake. Mapambano yalisababisha zaidi ya wananchi 30 kupoteza maisha.

Ukisikiliza Press Conference za Gwajima na Manji utagundua kuwa wanatumia njia hiyo hiyo kama aliyotumia Christopher "Dudus" Coke.

Manji anataka suala lake binafsi liwe ni suala la mashabiki na wapenzi wa Yanga kwa sababu anaisaidia Yanga kifedha. Manji anajaribu kuhakikisha vyombo vya habari vinaandika kile anachokitaka.

Gwajima anataka suala lake binafsi liwe ni suala la waumini wa kanisa la Ufufuo na Uzima kwa sababu anatoa huduma za kiroho na kifedha kwa waumini wake.

Tumeona Manji akiongozana polisi na kundi la mashabiki na wapenzi wa klabu ya Yanga.

Tumemuona Gwajima akiongozana polisi na kundi la waumini wa Kanisa la Ufufuo na Uzima.

Kwa mpango huu, Manji na Gwajima wanaweza kufanikiwa kwa sababu ya umasikini wa elimu na fedha uliotamalaki nchini.

Je, serikali imejiandaa kwa kiwango kipi katika mapambano yaliyo mbele yake?

A Chinese military general, strategist and philosopher, Sun Tzu once said, If you know the enemy and know yourself, you need not fear the result of a hundred battles. If you know yourself but not the enemy, for every victory gained you will also suffer a defeat. If you know neither the enemy nor yourself, you will succumb in every battle.
Usijali sana kwa sababu makundi ya watu hawa, hata kabla ya serikali, tayari ndani ya jamii yenyewe wana maadui. Tunao wapinzani wa Yanga na wapinzani wa dini za uamusho.

Kidogo inanishangaza kwamba kumbe kuna watu wengi ambao wana pesa, lakini uwezo wa kutengeneza hoja kwao ni mdogo sana! Yaani unaitwa na polisi halafu unaanza kuhoji muda utakaotumia hapo polisi! Eti watu zaidi ya sitini watamalizika saa ngapi? Hawa ndo wale wanaoishi TZ wakiwa wamejisahaulisha maisha ya wengine yakoje.
 
Back
Top Bottom