Girlfriend wangu ametekwa,alazimishwa kufanya mapenzi at a gun point naombeni ushauri

Bushloiaz

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
721
806
Great thinker ni mara yangu ya kwanza kuweka bandiko humu jf,nimekuwa nikitembelea kwa muda hadi nilipoamua kujiunga na nimeona baadhi yenu mkitoa ushauri mzuri tu kwa watu wanaopatwa na masahibu mbalimbali. Nina msichana ambaye nilikuwa nafahamiana nae tangu 2009,kwa sasa anasoma taasisi ya uhasibu tanzania mwaka wa kwanza kuna jamaa alikuwa dr wa kituo kimpja cha afya tabata ambacho kimefungwa na serikali ambaye aliwahi kumtibu huyu girlfriend wangu akiwa form two amemteka pale chuoni kwao kwa kumshikia bastola na kumlazimisha kufanya nae mapenzi,kampora simu niliyokuwa nimempa huyo msichana,am confused gt,huyu msichana nilikuwa nimepanga awe mke wangu mwaka ujao tukio hili limeniacha njia panda,nimuache kutokana na hili tukio au niendelee nae?Hili tukio limetokea usiku wa kuamkia jana. Note:huyu msichana is one of those good girls nimemtoa bikra mwenyewe feb this year,hanywi pombe naomba asichukuliwe kama labda malaya.
 
Pole, mi sioni kama kuna haja ya kumwacha mchumba wako kwani hata kwa maelezo yako alifanya kwa kulazimishwa(sawa kabakwa), angekuwa kafanya hivyo kwa kukuibia ningekushauri umkimbie kama ukoma.
Pili kwa sababu tukio lenyewe mi maweza kuliita la ubakaji, huyo dada alichukua uamuzi gani? Au alilihuzunika tu kitendo?
 
uchunguz ufanyike kuhusiana na tukio .sheria ichukue mkondo wake.pia nadhani yuo just need to calm down ,mwonen mtaalam wa saikoloji ili aweze kumshauri accordingly, usimwache b'se sio intention yake.pole sana may god comfort u
 
mmmhhhh sasa we unfanya nini JF jamani si unatakiwe uwe polisi sasa mfuatane mpaka sehemu ya tukio.. hiyo ni kama hii story ni ya kWeli.. au amesha achiliwa
Asante Afrodenzi kwa ushauri,mimi nafanya kazi mkoani siko dar,ishu ya police walifanya jana yeye na dada yake,unfortunately ishu ya kubakwa haina nguvu kwa sasa baada ya huyo msichana kuoga baada ya huyo jamaa kumrudisha chuoni na kumtisha kwamba asijaribu kufanya lolote kwa sababu yeye ana mtandao mrefu,na aliogopa kuniambia mimi coz if ningejua ishu hiyo ilitokea ninajua alikuwa anatakiwa aende polisi bila kuoga
 
Hapo wala haukutakiwa kujadiliana humu Jf. Ripoti tukio polisi. Huyo mtekaji achukuliwe hatua za kisheria. Kisha endelea kumpenda huyo mchumba wako na ufanye haraka umuoe. Kuhusu kutoana bikra wala haukua na haja ya kutueleza kwani hatutoweza kuthibitisha kama ni kweli au si kweli!.
 
Pole kwa tatizo kaka yangu. Ni wazi hajafanya kwa utashi na bahati nzuri nawe walijua hilo so haina sababu ya kumwacha. Kama kweli unaamini anakupenda na wewe unampenda kwa dhati lichukulie kama ajali tu ambayo haikuwa na kinga! Cha muhimu chekini afya kisha maisha yaendelee. Watu wanafumania wachumba zao wakifanya mapenzi kwa utashi wao, sembuse huyu aliyetishiwa maisha?
 
Pole, mi sioni kama kuna haja ya kumwacha mchumba wako kwani hata kwa maelezo yako alifanya kwa kulazimishwa(sawa kabakwa), angekuwa kafanya hivyo kwa kukuibia ningekushauri umkimbie kama ukoma.
Pili kwa sababu tukio lenyewe mi maweza kuliita la ubakaji, huyo dada alichukua uamuzi gani? Au alilihuzunika tu kitendo?
Kaka huyo msichana yuko katika hali mbaya,ninaongea nae mara kwa mara,leo for instance tumewasiliana usiku kucha we couldn't sleep bro,imagine kwenye dunia ya mapenzi kaingia feb this year and hili limemtoke juzi you can imagine yuko kwenye hali gani kaka
 
Kama kabakwa, katika mazingira yoyote yale, si kosa lake. Ni kosa mbakaji. Huo ndiyo msimamo wangu kwenye haya mambo ya ubakaji na unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake. Haijalishi kama alijilengesha mwenyewe, alivaa nguo ya uchokozi, au walikubaliana halafu baadaye akabadili mawazo. Kwangu hapana inamaanisha hapana, nukta, mwisho wa majadiliano.

Ila kama unafikiria kumuacha kwa sababu hiyo ya kubakwa utakuwa humtendei haki. Labda uniambie kuwa una wasiwasi kuwa hakubakwa na anasema hivyo ili usimshutumu kwa kuchiti. Lakini kama kabakwa kweli kumtupa wakati kama huu si vizuri. Huu ndiyo wakati ambao wewe mwandani wake unatakiwa kuwa naye karibu kumfariji, kumpa moyo, na kumwambia kuwa kilichotokea ni kibaya lakini siyo mwisho wa dunia.

Pia angalieni nini katika upande wa sheria ambacho mnaweza kufanya. Manake kesi kama hizi zinatakiwa ziripotiwe polisi mapema iwezekanavyo ingawa sina imani kabisa na hivi vyombo vyetu vya kisheria hususan ikija kwenye haya mambo ya ubakaji na unyanyasaji wa wanawake na watoto. Lakini ni bora kufanya kitu kuliko kutofanya kabisa.

Sasa sijui hata kama tuna wapelelezi na maofisa wa polisi wanaohusika na kushughulika moja kwa moja na kesi za ubakaji au hata kama wanavyo vitendea kazi kama vile Sexual assault forensic evidence (SAFE) kit.

Na kama amepatwa na kiwewe (traumatized) jaribuni kutafuta ushauri nasaha. Huwa unasaidia sana. Ila cha muhimu zaidi ni wewe kuwa karibu naye katika kipindi hiki kigumu. Ukimuacha mtoto wa watu unaweza ukamsababishia mabaya zaidi kuliko hata hilo balaa alilokumbana nalo.
 
Kaka huyo msichana yuko katika hali mbaya,ninaongea nae mara kwa mara,leo for instance tumewasiliana usiku kucha we couldn't sleep bro,imagine kwenye dunia ya mapenzi kaingia feb this year and hili limemtoke juzi you can imagine yuko kwenye hali gani kaka

Nakushauri umpeleke kwenye ushauri nasaha kwa sababu hali aliyoipata inaweza ikaathiri mwenendo mzima wa maisha yake ya mapenzi huko mbeleni. Usijeshangaa akakosa kabisa hamu ya kufanya mapenzi au akawa kila mkikutana faragha anashrink au kulalamika maumivu makali (kama alipata maumivu wakati anabakwa).

Huyo Dr. aliyembaka, hata kama hakuna ushahidi tafuta namna ya kumnyoosha................ah!
 
Take ur time. okey alikuwa bikra kwanza? kama hakuwa then kapime afu nende kanisa mkafunge.
 
Eric Shigongo stories, Hakuna ukweli wowote, Demu yupi wa kumshikia bastora, sema kapigwa sound na Dr na kakubali yeye mwenyewe.
 
She is a victim! Si mkosaji, mkosaji ndiye anayehukumiwa; victim husaidiwa. Good thing kuwa at least ameanza na experience ya kuwa na wewe; mwanaume mwenye mapenzi, maana angekutwa na hiyo dhahma kabla yako labda asingekupenda!
Anahitaji mapenzi zaidi; ili asigeneralize kuwa wanaume wote wabaya! Ukimuacha atawachukia wote! Good thing imeingia humu JF naamini utaweza fanya informed decisions!
 
Asante Afrodenzi kwa ushauri,mimi nafanya kazi mkoani siko dar,ishu ya police walifanya jana yeye na dada yake,unfortunately ishu ya kubakwa haina nguvu kwa sasa baada ya huyo msichana kuoga baada ya huyo jamaa kumrudisha chuoni na kumtisha kwamba asijaribu kufanya lolote kwa sababu yeye ana mtandao mrefu,na aliogopa kuniambia mimi coz if ningejua ishu hiyo ilitokea ninajua alikuwa anatakiwa aende polisi bila kuoga

Dahhhhh
poleni sana
binafsi naona bibie umtafutie msaada kwanza. maana tendo la kubakwa huwa linabaki na mtu kwa muda mrefu saana na linaweza kumuathiri kiakili pia.. na hata kusababisha matatizo mengine baadaye kwenye uhusiano wenu.. kwa sasa ningumu lakini hatua za kisheria zikifuatwa ili huyu jamaa atiwe mbaroni kwani atawaumiza wengi kwa kuwatishia kama alivyofanya hapo awali..
 
Eric Shigongo stories, Hakuna ukweli wowote, Demu yupi wa kumshikia bastora, sema kapigwa sound na Dr na kakubali yeye mwenyewe.
Kaka nashukuru kwa hayo mawazo yako,but try to think if you were in our shoes?sio kila kitu ni story za shingongo ndugu yangu
 
Great thinker ni mara yangu ya kwanza kuweka bandiko humu jf,nimekuwa nikitembelea kwa muda hadi nilipoamua kujiunga na nimeona baadhi yenu mkitoa ushauri mzuri tu kwa watu wanaopatwa na masahibu mbalimbali.
Nina msichana ambaye nilikuwa nafahamiana nae tangu 2009,kwa sasa anasoma taasisi ya uhasibu tanzania mwaka wa kwanza kuna jamaa alikuwa dr wa kituo kimpja cha afya tabata ambacho kimefungwa na serikali ambaye aliwahi kumtibu huyu girlfriend wangu akiwa form two amemteka pale chuoni kwao kwa kumshikia bastola na kumlazimisha kufanya nae mapenzi,kampora simu niliyokuwa nimempa huyo msichana,am confused gt,huyu msichana nilikuwa nimepanga awe mke wangu mwaka ujao tukio hili limeniacha njia panda,nimuache kutokana na hili tukio au niendelee nae?Hili tukio limetokea usiku wa kuamkia jana.
Note:huyu msichana is one of those good girls nimemtoa bikra mwenyewe feb this year,hanywi pombe naomba asichukuliwe kama labda malaya.

Angekuwa si malaya ungewezaje kumtoa bikra nje ya ndoa?

Jee, ulikuwepo wakati anatekwa na bastola? Au ndio story aliokupa yeye?

Usiwe ****, kama hiyo story kakupa yeye basi kakudanganya kijinga nawe umeingia mkenge kwa kuwa unamuamini sana.
 
mkuu hizo story zipo sana kwa mademu wa kibongo,haswa pale wanapopata jamaa mpya mwenye nazo,na wanataka kukupiga chini,mm nilishaletewa hzo story,baadae atakuambia sipo tayari tena kuwa na wewe kwa vile nshabakwa,bora tuachane tuu!chukua hatua kaka.ni usanii tuu huo
 
Angekuwa si malaya ungewezaje kumtoa bikra nje ya ndoa?

Jee, ulikuwepo wakati anatekwa na bastola? Au ndio story aliokupa yeye?

Usiwe ****, kama hiyo story kakupa yeye basi kakudanganya kijinga nawe umeingia mkenge kwa kuwa unamuamini sana.
Asante lwa mawazo yako Faiza
 
mkuu hizo story zipo sana kwa mademu wa kibongo,haswa pale wanapopata jamaa mpya mwenye nazo,na wanataka kukupiga chini,mm nilishaletewa hzo story,baadae atakuambia sipo tayari tena kuwa na wewe kwa vile nshabakwa,bora tuachane tuu!chukua hatua kaka.ni usanii tuu huo
Asante kaka,hebu fikiria kama sio hizo story,halafu mimi nikamwambia basi je,unadhani litakuwa jambo sawa kufanya?
 
Nashukuru Faiza na Parachichi,binafsi cjaweza kuamimi hii stori naona huyu dada amemchezea tu huyu kaka akili na inawezekana kafanya kwa kupenda kabisa ila anasingizia na unajua inawezekana haku2mia kinga kwa hyo anategemea katoto hapo na aliyempa hana time wewe unafikiri angekuambiaje?wewe subri 2 utasikia la mtoto,halafu unajua nn inawezekana tayari anajua ana mimba,pole lakini tatizo u a so in love that coments like this one unaona tunakuponda,tulia hoji vizuri,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom