bushman
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,411
- 743
Kwa kweli hawa mawaziri wa tanzania sijui wanaishi miongoni mwa jamii za kitanzania au wamekuja kwa mkataba kuafanya kazi na kuondoka huyu waziri yuko mikoa ya kusini kwenye ziara zake huko,kuna kauli alinukuliwa na vyombo vya habari (tbc 8:00pm) juzi akisema;
nina maswali yafutayo
- walimu wote wakuu waliofaulisha wanafunzi ambao hawajui kusoma wala kuandika katika mtihani wa darasa la saba watawajibishwa.
nina maswali yafutayo
- anayetakiwa kuwajibishwa ni mwalimu mkuu au viongozi waandamizi wa wizara ya elimu na idara zake.??
- mkuchika anajua kuwa kuna shule zina walimu watatu tu??na wote wanafundisha masomo yanayofanana??
- anajua kuwa huko mashuleni siku hizi hakuna hata "chaki' za kuandikia ubaoni??je unategemea nini katika mazingira kama haya??hili nimeliona kwa macho yangu kwa sababu wazee wangu wote walimu wa shule ya msingi.
- anajua kwamba mitaala inabadilishwa na wizara bila kutoa mafunzo kwa walimu ambao ndio wadau wakubwa katika kufundisha???
- anaelewa kuwa walimu ndio tabaka ambalo limesahaulika sana katika utumishi wa umma?tofauti na kipindi cha enzi za mwalimu ambapo mwalimu,bwana shamba na bwana waganga walikuwa wanathaminiwa sana katika jamii??amefanya utafiti kujua nini chanzo cha matatizo hayo???
- serikali yenu imewalaghai walimu mara ngapi kuhusu madai yao??unajua kuwa walimu wamekata tamaa sana???je unategemea kupata matokeo mazuri kutoka kwa walimu waliokata tamaa??