Genius: Ushauri wa simoni Patrick Ili kukuza soka la Tanzania

Labani og

JF-Expert Member
Sep 15, 2020
15,774
24,209
Simon Patrick (Mwanasheria wa klabu ya Yanga SC)

Hongereni sana @taifastars_ , binafsi siwadai, matokeo haya ndio kipimo chetu cha uwekezaji wetu kwenye soka.

Kwa maslahi mapana ya Taifa, nipende kushauri yafuatayo;

1. Tuziunganishe TFF & ZFF na tuwe na ligi moja bora yenye timu kutoka bara na Zanzibar.

2. Serikali itoe ruzuku kwa timu za vijana kama inavyofanya kwa vyama vya siasa.

3. Serikali ifute kodi na michango isiyo na tija kwa timu za mpira mfano NSSF, WCF, SDL, etc haina tija kwa wachezaji bali huongeza mzigo kwa vilabu, ianzishe kodi maalam ya zuio (WHT) kwa ajili ya wachezaji.

4. Hela zetu za FIFA za maendeleo ya mpira wa miguu zielekezwe kwenye kurekebisha miundombinu ya viwanja hasahasa sehemu ya kuchezea (pitch) ili ligi iwe na ubora zaidi.

5. TFF ianzishe mashindano ya vijana ya kitaifa nje na vilabu na yafanyike kila mwaka sambamba na kurudisha mashindano ya mashuleni.

6. Serikali ianzishe scholarship maalum kwa wanafunzi wote wenye vipaji na kuwataftia akademi nje.

7. Kwakuwa AFCON ya 2027 tunaandaa wenyewe hivo hatutakua na presha ya kufudhu, tuandae timu ya taifa kuanzia leo.

Je ni ushauri Gani unaona ni konk??

#daimambelenyumamwiko
1706251182528.jpg


Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
8. Serikali irasmishe hadhi maalum za wachezaji wote wanaocheza nje ya mipaka ya Tanzania na wenye asili ya kitanzania watakaotaka kuja kulitumikia taifa.

9. Tulete wakufunzi na wataalamu wa soka la vijana, wapewe jukumu la kukuza talent kila mwaka, na vijana hawa wakulie sehemu moja.

10. Wadhamini wote wa michezo wapewe msamaha maalum wa kodi kwenye biashara zao, hii itavutia uwekezaji zaidi kwenye mpira wetu.


Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Simon Patrick (Mwanasheria wa klabu ya Yanga SC)

Hongereni sana @taifastars_ , binafsi siwadai, matokeo haya ndio kipimo chetu cha uwekezaji wetu kwenye soka.

Kwa maslahi mapana ya Taifa, nipende kushauri yafuatayo;

1. Tuziunganishe TFF & ZFF na tuwe na ligi moja bora yenye timu kutoka bara na Zanzibar.

2. Serikali itoe ruzuku kwa timu za vijana kama inavyofanya kwa vyama vya siasa.

3. Serikali ifute kodi na michango isiyo na tija kwa timu za mpira mfano NSSF, WCF, SDL, etc haina tija kwa wachezaji bali huongeza mzigo kwa vilabu, ianzishe kodi maalam ya zuio (WHT) kwa ajili ya wachezaji.

4. Hela zetu za FIFA za maendeleo ya mpira wa miguu zielekezwe kwenye kurekebisha miundombinu ya viwanja hasahasa sehemu ya kuchezea (pitch) ili ligi iwe na ubora zaidi.

5. TFF ianzishe mashindano ya vijana ya kitaifa nje na vilabu na yafanyike kila mwaka sambamba na kurudisha mashindano ya mashuleni.

6. Serikali ianzishe scholarship maalum kwa wanafunzi wote wenye vipaji na kuwataftia akademi nje.

7. Kwakuwa AFCON ya 2027 tunaandaa wenyewe hivo hatutakua na presha ya kufudhu, tuandae timu ya taifa kuanzia leo.

Je ni ushauri Gani unaona ni konk??

#daimambelenyumamwikoView attachment 2883098

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
Viwanja vya chama virudishwe serikalini.
 
Hapo point ya maana ni hiyo #2 tu ya ruzuku kwa timu za vijana, mengine yote ni kama porojo tu ya mtu anayetafuta sifa za haraka haraka bila kujua anachokisema. Halafu kwa taaluma yake ningedhani angejikita kutoa ushauri wa masuala ya kisheria zaidi.

Baadhi ya ushauri aliotoa ukiweka katika mizania ya kisheria, hata yeye akiuangalia upya katika jicho la kisheria hawezi kuukubali.
 
Hapo point ya maana ni hiyo #2 tu ya ruzuku kwa timu za vijana, mengine yote ni kama porojo tu ya mtu anayetafuta sifa za haraka haraka bila kujua anachokisema. Halafu kwa taaluma yake ningedhani angejikita kutoa ushauri wa masuala ya kisheria zaidi.

Baadhi ya ushauri aliotoa ukiweka katika mizania ya kisheria, hata yeye akiuangalia upya katika jicho la kisheria hawezi kuukubali.
Vipi hili la kuweka ligi Moja kati ya zenji na TZ

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Je ni ushauri Gani unaona ni konk??
Ni ushauri ambao hata asingeutoa, bado TFF ingefanya hayo maana ndio iliyofanikisha mambo mengi kuliko utawala wowote tangu nchi ipate uhuru. By the way, ni ushauri ambao umebagua soka la wanawake na la ufukweni, mambo ambayo pia ni majukumu ya TFF
 
Ni ushauri ambao hata asingeutoa, bado TFF ingefanya hayo maana ndio iliyofanikisha mambo mengi kuliko utawala wowote tangu nchi ipate uhuru. By the way, ni ushauri ambao umebagua soka la wanawake na la ufukweni, mambo ambayo pia ni majukumu ya TFF
Lakini pia tunaangalia influence ya hicho kitu

Mfano soka la wanawake Je Lina uzika kiasi Gani ....

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Lakini pia tunaangalia influence ya hicho kitu

Mfano soka la wanawake Je Lina uzika kiasi Gani ....

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
Soka la wanawake ndiyo lina fursa ya kututoa nashangaa kwa nini hatuongezi nguvu huko. Angalia mafanikio ambayo wameweza kupata katika kipindi kifupi. Usiangalie leo tu, future ya dunia huko tunakokwenda mwanamke ana nguvu sana. Na tumechelewa sana maana hili nililiiona kitambo sana.
 
Soka la wanawake ndiyo lina fursa ya kututoa nashangaa kwa nini hatuongezi nguvu huko. Angalia mafanikio ambayo wameweza kupata katika kipindi kifupi. Usiangalie leo tu, future ya dunia huko tunakokwenda mwanamke ana nguvu sana. Na tumechelewa sana maana hili nililiiona kitambo sana.
Daaah ni kama Kuna kaukweli

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Lakini pia tunaangalia influence ya hicho kitu. Mfano soka la wanawake Je Lina uzika kiasi Gani ....
FIFA inapotoa ruzuku huwa inazingatia kuwapo kwa mchezo wa soka wa makundi yote, kama vile wanaume, wanawake, walemavu, vijana na ufukweni. Ndio maana nikasema utawala wa Karia umefanikiwa kuliko tawala zote maana kila kundi hapo limefika hatua nzuri. Hao walemavu ndio wamefuzu hadi fainali za kombe la dunia, jambo ambalo halikuwahi kutokea
 
FIFA inapotoa ruzuku huwa inazingatia kuwapo kwa mchezo wa soka wa makundi yote, kama vile wanaume, wanawake, walemavu, vijana na ufukweni. Ndio maana nikasema utawala wa Karia umefanikiwa kuliko tawala zote maana kila kundi hapo limefika hatua nzuri. Hao walemavu ndio wamefuzu hadi fainali za kombe la dunia, jambo ambalo halikuwahi kutokea
Yaah nikweli ... kipindi hiki Cha karia kajutahidi sana

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom