TAJIRI MKUU WA MATAJIRI
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 5,720
- 10,216
Kamati ya mashindano ya Kombe la Mapinduzi ilikuwa na nafasi kubwa ya kufanya haya mashindano yawe na heshima na hadhi ya juu kimataifa, lakini figisu na kukesa weledi kunafanya mashindano yaonekane kituko hasa kwa timu wageni tunaowaalika.
Ushauri wangu kwa kamati ya mashindano haya, isiundwe na Watanzania peke yake (Tanganyika na Zanzibar) bali kamati iundwe na wataalamu wa soka kutoka kwenye nchi zote zitakazoshiriki mashindano.
Pia waamuzi watoke kwenye mataifa shiriki ili mashindano yawe na ladha zaidi na kubeba sura ya kimataifa zaidi.
Hii ni fursa, mashindano yakiboreshwa, timu zitaleta mashabiki wao. Mashabiki watakula, watalala na kutalii kwa gharama zao na kutunisha sehemu ya pato la taifa hususan upande wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Wito wangu:-
Fanyeni muwezavyo muwaombe radhi APR na muwaeleze ni kwa jinsi gani mtaboresha mashindano yajayo.
Ondoeni siasa kwenye mpira, eti lazima timu ya Zanzibar icheze fainali hata kwa kubebwa, hii ni aibu kubwa sana kwa soka la Zanzibar.
Ushauri wangu kwa kamati ya mashindano haya, isiundwe na Watanzania peke yake (Tanganyika na Zanzibar) bali kamati iundwe na wataalamu wa soka kutoka kwenye nchi zote zitakazoshiriki mashindano.
Pia waamuzi watoke kwenye mataifa shiriki ili mashindano yawe na ladha zaidi na kubeba sura ya kimataifa zaidi.
Hii ni fursa, mashindano yakiboreshwa, timu zitaleta mashabiki wao. Mashabiki watakula, watalala na kutalii kwa gharama zao na kutunisha sehemu ya pato la taifa hususan upande wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Wito wangu:-
Fanyeni muwezavyo muwaombe radhi APR na muwaeleze ni kwa jinsi gani mtaboresha mashindano yajayo.
Ondoeni siasa kwenye mpira, eti lazima timu ya Zanzibar icheze fainali hata kwa kubebwa, hii ni aibu kubwa sana kwa soka la Zanzibar.