Ni muda mrefu sana Gazeti la Mwanahalisi halionekani, wanaJF naomba mnijulishe sakata la Gazeti hili limeishia wapi na tutarajie nini kuhusu hatima yake. Tumeona kuibuka magazeti ya wiki kama hilo yanayoshambulia kinyume na Mwanahalisi kwa maana ya kushambulia uanaharakati badala ya kuiunga mkono. Je inawezekana wenye Magazeti hayo ndio wameshinikiza Mwanahalisi lifungiwe ili magazeti yao yakue? Naombeni ufafanuzi kuhusu hili.