Stabilaiza
JF-Expert Member
- Jul 11, 2012
- 1,843
- 1,143
Ukifuatilia habari na vichwa vya habari mbalimbali za Mtanzania kuhusu Zitto, utagundua zinaandikwa kishabiki na kuelekea kuwa za Ukajanja. Kwa mfano katika toleo la leo wametoka na kichwa cha habari kinaonyesha kuwa Chadema waanzisha vita mpya na Zitto huku wakijua kuwa si hotuba ya Chadema bali kambi rasmi ya upinzani bungeni. Kama hiyo haitoshi, wakaonyesha ukajanja pale waliposema mwenyewe akubali ‘kuajibika' badala ya kuwajibika. Hii inaonesha Mtanzania wanaandika habari za Zitto kiushabiki na kwa kuhemkwa hadi kuanika ukajanja wao. Mtanzania nalo limeingia kwenye orodha ya magazeti ya ukajanja kama yalivyo Habari Leo, Uhuru, Mzalendo na Jambo