Gari la Ole Sendeka lavunjwa vioo Kiteto, Polisi wafyatua risasi na mabomu

JAMHURI

JF-Expert Member
Dec 15, 2010
449
60
Wanachama wa CCM Wilayani Kiteto mkoani Manyara wamejikuta katika malumbano na mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka baada ya Mbunge huyo machachari kuwaambia "Kiteto hakuna mwanaume"

Kauli hiyo alitokana na kile kilichodaiwa kuhofiwa kubadilishwa matokeo ya Ubunge na kufanya wanachama hao kufika kwa wingi katika ofisi hizo kushinikiza matokeo yasibadilishwe.

Kauli hiyo iliwaudhi wanaCCM hao na kujikuta wakirusha mawe na kuvunja gari lake kioo cha nyuma kisha kusababisha kuchafuka kwa hali ya amani ofisini jambo lililolazimu polisi kutumia mabomu ya machozi na risasi za moto kuwatawanya wafuasi hao.

Pia wanachama hao walienda kufanya fujo nyumbani kwa mbunge huyo na kuvunja taa za nje pamoja na kumpiga mlinzi jambo ambali lilidaiwa ni kosa.

Wajumbe hao wa CCM mkoa walifika kwa ajili ya kuhakiki matokeo ya Ubunge ambapo Benedict Ole Nangoro alilalamika kuhusu kuhujumiwa katika uchaguzi huo uliompa nafasi Emmanuel Papian.

• Gari la Ole Sendeka lavunjwa vioo,Ole Nangoro anusurika kichapo
• Nyumba yake yavamiwa na wanachama, wavunja taa na kumpiga mlinzi

JESHI la Polisi wilayani Kiteto mkoani Manyara limetumia mabomu ya machozi na silaha za moto kuokoa aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Kiteto Benedict Ole Nangoro na Christopher Ole Sendeka pamoja na kamati ya siasa ya Mkoa wa Manyara waliofika kuhakiki matokeo ya Ubunge.

Awali wajumbe hao walizuiwa kwa mawe na magogo barabarani kata ya Engusero wasifike makao makuu ya wilaya ya Kiteto wakitokea Dodoma, hali iliyolazimu Jeshi la Polisi kuwaokoa kwa kuwapa ulinzi kwa kuwafikisha Kibaya kwaajili ya kuhakiki matokeo hayo

Baada ya kamati ya siasa ya mkoa kufika katika ofisi za CCM Wilaya ya Kiteto majira ya mchana walianza kuhakiki matokeo ya Ubunge ambayo yalidaiwa kulalamikiwa na aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Kiteto Benedict Ole Nangoro aliyeambatana na wajumbe hao kutaka yahakikiwe.


attachment.php


Hali ilivyokuwa muda mchache uliopita.

“Baada ya kusikia kuna kamati ya siasa mkoa wa Manyara imefika wanachama tulilazimika kufika ofisi za CCM kutaka kujua hatma ya ujio wao, kwani tumeshuhudia maeneo mengi matokeo ya uchaguzi yanabadilishwa baada ya kutangazwa washindi”alisema mwananchi Rajabu Jagon
 
Yaani kutoka Simanjiro kwenda kuvunjiwa vioo, Kiteto. Kweli nimeamini kifo cha nyani miti yote huteleza. Hii ndo niagieni CCM.
 
tuliyaona haya kwa ndugai, sasa kwa ole sendeka. huko ccm bila shaka kutachimbia. njaa hizi mbaya sana.
 
Kwa muungwana lugha ya matusi si nzuri, tena wamemuhurumia alitakiwa apewe kipigo cha mbwa mwizi. Hii ndo jeuri ya makada wanajiona wao ni bora zaidi na kwamba serikali ni yao. Kwani mbunge ni kitu gani hadi atukane watu? Hawa dawa yao ni kuwabwaga kuanzia diwani, mbunge hadi rais. Wakae pembeni wajifunze na watuonyeshe walikoweka pesa zetu
 
Muda wa tindikaki wenyewe bado naona police kimya hawasemi wamekamata tindikali kwamba mwakahuu kimya! nashauri waanze kuwabana watu mapema
 
Back
Top Bottom