Natumai wengi wenu mmelala kwa kua ni ucku mkubwa,bat kwa upande wangu naic ni mchana kwani ndio natoka kufua now nguo zangu,sitoweza kukufuru na mshkuru MUNGU sana na nautumikia mtihani wake alonipa,siwezi jua kipi ameniandalia kizuri kwenye dunia au akhera yangu(maisha baada ya kifo)kwani nabii Ayubu aliumwa kwa miaka mingi mpaka mke na familia yake ikamtenga na wala hakukufuru na zawadi yake kupitia mtihani wa maradhi mungu alim2nukia pepo wakati kuna walopata uzima duniani wakamsahau mungu wakaonja moto,nachotaka kusema mtihani wowote unakufanya uwe karibu na mungu wako,uwe mtihani wa maradhi,riziki,ndoa n.k,naitaji dua zenu wana jf kwani nimemaliza waganga na wagaguzi,hospital bila mafanikio,hapa nilipo mikono inauma kwakufua kila siku,mda huu na kiu lakini nashindwa kunywa maji kwasasa np macho ila nikifumbatu jicho haja ndogo inanitoka bila hisia,ila nikilala mchana wala hii hali hijitokezi ni ucku tu,nashkuru mungu ni mzuri wa sura kiasi changu nilicho jaaliwa wengi wananitaka kwa ndoa ila na sita kwasababu ya tatizo langu huenda kilio kikazidi katika ndoa,nilijaribu kueka post yangu ya kutafuta mwenza mwenye sifa kama zangu bila mafanikio,hua naumia sana ndugu na majirani kujua matatizo yangu na kunibeza mda mwengine hua nahic nawatia aibu wazazi wangu,hua nasubiri watu wote walale ndionifue naona haya kuanika kwenye kamba kwa kuepusha maswali kwanini kilasiku nafua?nguo na anika ndani kwa hiyo hukauka bila kupigwa najua kwa hali hiyo kila cku na nusurika kunga'twa na tandu au nnge hufuata ubaridi katika nguo,ebu vuta picha kipindi hiki cha kipupwe âlafu unaamka ukiwa umeroa unaskia baridi kiasi gani?na nakoga sa 11 kabla watu hawajaamka hua baridi mda huo sana naomba mungu niepushe na nimonia.Wana jf mshukuruni mungu kwa maneno na vitendo kwa neema ya uhai,uzima,rizki,mali,watoto,ndoa,n.k kuna watu hawana.ucku mwema!