Furaha ya maisha ipo nje au ndani ya ndoa?

Bra-joe

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
1,562
986
Hi wana Jf, naomba tujadili kuhusu maisha ya ndani au nje ya ndoa ni yapi yanafuraha zaidi? Sasa hivi ukikaa na wana ndoa hawaishi kulalamika juu ya ndoa zao, vile vile wasio na ndoa wanatamani sana kuingia ktk ndoa, hapo ndipo ninapoachwa njia panda. Furaha ya maisha ipo wapi? Ndani au nje ya ndoa?
 
kwaani malengo ya watu wote yanafanana?

Nipe jibu la hili, life in town is better than life in village.
 
Ni wewe mwenyewe na ujipime kwenye kila kitu
Maana kila kitu kina kiasi na ukizidisha ni kero
Unataka kupata nini katika ndoa
Na anayelalamika kuhusu ndo aana yake aliyoyatamani ambayo kwake anaona hajatimiza na ambaye anafurahia ujana nae ana yake ambayo bado anaendelea nayo nayo yanampa furaha
Jipime kwa kila kitu kama uko tayari kuingia kwenye ndoa ingia kama hauko tayari na unaona maisha ya kuwa single ni mazuri endelea nayo mpaka muda wako
Usilazimishe chochote au usifuate mkumbo
 
Hi wana Jf, naomba tujadili kuhusu maisha ya ndani au nje ya ndoa ni yapi yanafuraha zaidi? Sasa hivi ukikaa na wana ndoa hawaishi kulalamika juu ya ndoa zao, vile vile wasio na ndoa wanatamani sana kuingia ktk ndoa, hapo ndipo ninapoachwa njia panda. Furaha ya maisha ipo wapi? Ndani au nje ya ndoa?
kote kuna raha yake ili mradi umpate yule munaendana kwa kila kitu na kuelewana kwa kila sehemu hapo mtaenjoy sana na hutaona tofauti ya aliye ktk ndoa au nje ya ndoa
 
Ukijua hitaji lako duniani utapata furaha!Pia furaha haiwezi kupatikana nje yako kijana!
 
Kila mtu anataste yake..hatuwezi kufanana wote!
Kwa upande wangu maisha nje ya ndoa nayaona matamu compare na walio ndoani..
 
Kila mtu anataste yake..hatuwezi kufanana wote!
Kwa upande wangu maisha nje ya ndoa nayaona matamu compare na walio ndoani..
we umo nje au ndani ya ndoa???
mana huwezi kuzungumzia ndani kama hujaingia bado na kama uko nje hapo sawa ni haki yako kuona nje kutamu kuliko ndani
 
Ni wewe mwenyewe na ujipime kwenye kila kitu
Maana kila kitu kina kiasi na ukizidisha ni kero
Unataka kupata nini katika ndoa
Na anayelalamika kuhusu ndo aana yake aliyoyatamani ambayo kwake anaona hajatimiza na ambaye anafurahia ujana nae ana yake ambayo bado anaendelea nayo nayo yanampa furaha
Jipime kwa kila kitu kama uko tayari kuingia kwenye ndoa ingia kama hauko tayari na unaona maisha ya kuwa single ni mazuri endelea nayo mpaka muda wako
Usilazimishe chochote au usifuate mkumbo
umeongea vizur sana hasa ktk black
 
Back
Top Bottom