Mungi
JF Gold Member
- Sep 23, 2010
- 16,975
- 9,566
Na Dustan Shekidele, Morogoro
GUMZO wikiendi iliyopita ya shamrashamra za Sikukuu ya Pasaka mjini hapa, ni lile la bosi wa kiwanda cha maturubai aliyetajwa kwa jina la Daudi, kufumwa gesti akiwa na mfanyakazi wake ambaye ni mke wa mtu aliyetajwa kwa jina la Aisha.
Tukio hilo la aibu kwa bosi huyo lililoshuhudiwa na paparazi wetu, lilitokea muda mfupi kabla ya Pasaka majira ya saa 1:00 usiku ndani ya gesti maarufu iliyopo maeneo ya Sabasaba mjini hapa.
Habari zilizopatika eneo la tukio zilidai kuwa mzee huyo ana mazoea ya kufika mahali hapo na mwanamke huyo anayefanya kazi chini ya usimamizi wake ambapo huwa wanajiachia sehemu ya baa kabla ya kuingia ndani.
Siku ya tukio, 40 yao ilitimia baada ya wawili hao kutinga kwenye gesti hiyo na kujianika wakiponda raha.
Ilidaiwa kuwa wakiwa mahali hapo, kuna mtu alimuona Aisha ‘akidendeka' na mzee huyo hivyo akamjulisha mumewe aliyetajwa kwa jina la Mwinshehe.
Ilisemekana kuwa, baada ya kupokea taarifa hizo, Mwinshehe alipanga mikakati ya fumanizi ambapo alitinga kwenye gesti hiyo na kuhakikishiwa kuwa mkewe yupo ndani katika chumba chenye jina la Uganda ndipo alipoingia vitani.
Akiwa kwenye mvutano na wenye gesti waliomkataza kuingia, ghafla alimuona mkewe akitokea msalani akiingia ndani na ndipo alipovamia kwenye chumba na kumkuta mgoni wake ameshamaliza mchezo.
Baada ya kumuona mumewe, mwanamke huyo alianza kuangua kilio huku akisikika akisema, ‘Baba Nassoro nisamehe, makosa wamewekewa binadamu, sitarudia tena'.
Hata hivyo, Mwinshehe ambaye alikuwa na hasira hakumsikiliza zaidi ya kuwashushia kipigo ambapo yule mzee alishindwa kumudu mashambulizi baada ya kuzidiwa na kujikuta akichanika paji la uso, wenye gesti waliingilia kati na kuwatoa nje kisha wakafunga geti.
Baada ya hapo, timbwili zito lilihamia kwenye kituo kidogo cha polisi cha Kiwanja Cha Ndege ambapo baada ya kufika, Mwinshehe aliangua kilio alipowaona wakwe zake (baba na mama wa mkewe Aisha).
Aidha, wawili hao walitoa maelezo yao kituoni lakini hawakuelewana hivyo polisi waliingilia kati, wakaita gari la kuwapeleka kituo kikuu.
Tukio hilo la aibu kwa bosi huyo lililoshuhudiwa na paparazi wetu, lilitokea muda mfupi kabla ya Pasaka majira ya saa 1:00 usiku ndani ya gesti maarufu iliyopo maeneo ya Sabasaba mjini hapa.
Habari zilizopatika eneo la tukio zilidai kuwa mzee huyo ana mazoea ya kufika mahali hapo na mwanamke huyo anayefanya kazi chini ya usimamizi wake ambapo huwa wanajiachia sehemu ya baa kabla ya kuingia ndani.
Siku ya tukio, 40 yao ilitimia baada ya wawili hao kutinga kwenye gesti hiyo na kujianika wakiponda raha.
Ilidaiwa kuwa wakiwa mahali hapo, kuna mtu alimuona Aisha ‘akidendeka' na mzee huyo hivyo akamjulisha mumewe aliyetajwa kwa jina la Mwinshehe.
Ilisemekana kuwa, baada ya kupokea taarifa hizo, Mwinshehe alipanga mikakati ya fumanizi ambapo alitinga kwenye gesti hiyo na kuhakikishiwa kuwa mkewe yupo ndani katika chumba chenye jina la Uganda ndipo alipoingia vitani.
Akiwa kwenye mvutano na wenye gesti waliomkataza kuingia, ghafla alimuona mkewe akitokea msalani akiingia ndani na ndipo alipovamia kwenye chumba na kumkuta mgoni wake ameshamaliza mchezo.
Baada ya kumuona mumewe, mwanamke huyo alianza kuangua kilio huku akisikika akisema, ‘Baba Nassoro nisamehe, makosa wamewekewa binadamu, sitarudia tena'.
Hata hivyo, Mwinshehe ambaye alikuwa na hasira hakumsikiliza zaidi ya kuwashushia kipigo ambapo yule mzee alishindwa kumudu mashambulizi baada ya kuzidiwa na kujikuta akichanika paji la uso, wenye gesti waliingilia kati na kuwatoa nje kisha wakafunga geti.
Baada ya hapo, timbwili zito lilihamia kwenye kituo kidogo cha polisi cha Kiwanja Cha Ndege ambapo baada ya kufika, Mwinshehe aliangua kilio alipowaona wakwe zake (baba na mama wa mkewe Aisha).
Aidha, wawili hao walitoa maelezo yao kituoni lakini hawakuelewana hivyo polisi waliingilia kati, wakaita gari la kuwapeleka kituo kikuu.
Katika hali ya kushangaza, wakiwa njiani, wahusika hao walielewana na kurudi tena kituoni hapo ambapo Mwinshehe aliwaeleza polisi hao kuwa ameamua kumsamehe mkewe hivyo ametaka mgoni wake, Daudi alipe faini ya shilingi elfu 70.
Mzee Daudi aligoma kulipa kiasi hicho akidai kuwa ni kikubwa na alipoulizwa ana uwezo wa kulipa fidia ya kiasi gani alidai
atalipa elefu 50
. Mwishehe alichukua kiasi hicho cha fedha na kuondoka na mkewe nyumbani.