babu onyango
JF-Expert Member
- Jan 12, 2023
- 334
- 813
Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Nbc na mabingwa wa muda wote nchini Tanzania Young Africans S.C almaarufu Yanga leo tena wanashuka dimbani kukabiliana na maafande wa Ruvu shooting katika mwendelezo wa ligi kuu ya Nbc...
Mchezo huo utakuwa mgumu Kwa timu zote kwani Yanga wanataka kushinda ili kuzidi kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi ya Nbc huku Ruvu shooting nao wakiitaji alama zote tatu ili kujinasua kutoka mkiani mwa ligi.
Mchezo huu utapigwa kunako dimba la Benjamini Mkapa mnamo saa1.00 usiku
Je ni Wananchi au Mafande ndio watakao ondoka na kicheko baada ya dakika 90?? Kuwa nami mwanzo paka mwisho wa kipute
"" Wachezaji wa timu zote mbili wapo uwanjani wakipasha misuliili kujiweka sawa
'''""""""""'''''"""""''""”"”""""""'"""""""""
00" Kipenga Cha mwamuzi kimepulizwa kuashiria Mpira umeanza hapa kadika Dimba la Benjamini Mkapa katika
02" Hatari langoni mwa Yanga ila mpira unaenda nje inakuwa ni goal kick
05" Ruvu shooting wameanza vizuri mchezo wa leo huku utulivu ukiwa mkubwa
10" Kennedy Musonda yupo chini akipatiwa matibabu baada ya kugongana na goalkeeper wa Ruvu shooting
15" Mayele anaachia shuti kali lakini linapanguliwa na Mlinda mlango wa Ruvu shooting inakuwa Kona ambayo haikuzaa matunda
25" Bado milango ni migumu kwa timu zote
32" Gooooal Yanga wanatangulia Kwa bao Moja baada ya beki Mpoki Mwakinyuke kujifunga
40" Mayeleeeee....... Golikipa wa Ruvu anaokoa inakuwa ni kona. Hii ni Kona ya 5 Kwa Yanga wakati Ruvu hawajapa kona paka sasa
42" Moloko anapaisha akiwa kwenye nafasi nzuri ya kufunga. What a miss!
45" Shambulizi lingine langoni mwa Ruvu shooting lakini mpira unakwenda nje.
HT" Naaam ni mapumziko katika uwanja wa Benjamin Mkapa Wananchi wakiongoza kwa bao 1-0 dhidi ya Ruvu shooting.
Tukutane kipindi cha pili
"Kipindi cha pili kimeanza
49" Mayele anapoteza nafasi ya wazi kufunga goli la pili Kwa Yanga akiwa yeye na goli
62" Mayele anapiga kichwa kikali langoni mwa Ruvu shooting lakini golikipa anatoa mpira nje inakuwa kona ambayo haikuzaa goli
65" Yanga wamefanya mabadiliko ya wachezaji watatu kwa mpigo, wametoka Musonda, Farid,Moloko na Nafasi zao zimechukuliwa ni Mzize, Ambundo pamoja na Aziz K
Mechi imechangamka sana
80" Bado Yanga anaongoza kwa goli 1-0
87" Yanga wanapata faulo eneo zuri, Aziz K anapiga gooal lah lah golikipa wa Ruvu shooting anadaka vizuri kabisa
90+3" Naam mpira umekwisha hapa Uwanja wa Benjamin Mkapa timi ya Yanga inaondoka na alama zote 3 na kuzidi kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya Nbc kwa kufikisha jumla ya point 56 huku Ruvu shooting wakisalia mkiani mwa msimamo wa ligi.
Mlikuwa nami Babu Onyango kwa Dak zote 90 za mtanange huu
hadi wakati mwingine
Mchezo huo utakuwa mgumu Kwa timu zote kwani Yanga wanataka kushinda ili kuzidi kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi ya Nbc huku Ruvu shooting nao wakiitaji alama zote tatu ili kujinasua kutoka mkiani mwa ligi.
Mchezo huu utapigwa kunako dimba la Benjamini Mkapa mnamo saa1.00 usiku
Je ni Wananchi au Mafande ndio watakao ondoka na kicheko baada ya dakika 90?? Kuwa nami mwanzo paka mwisho wa kipute
"" Wachezaji wa timu zote mbili wapo uwanjani wakipasha misuliili kujiweka sawa
'''""""""""'''''"""""''""”"”""""""'"""""""""
00" Kipenga Cha mwamuzi kimepulizwa kuashiria Mpira umeanza hapa kadika Dimba la Benjamini Mkapa katika
02" Hatari langoni mwa Yanga ila mpira unaenda nje inakuwa ni goal kick
05" Ruvu shooting wameanza vizuri mchezo wa leo huku utulivu ukiwa mkubwa
10" Kennedy Musonda yupo chini akipatiwa matibabu baada ya kugongana na goalkeeper wa Ruvu shooting
15" Mayele anaachia shuti kali lakini linapanguliwa na Mlinda mlango wa Ruvu shooting inakuwa Kona ambayo haikuzaa matunda
25" Bado milango ni migumu kwa timu zote
32" Gooooal Yanga wanatangulia Kwa bao Moja baada ya beki Mpoki Mwakinyuke kujifunga
40" Mayeleeeee....... Golikipa wa Ruvu anaokoa inakuwa ni kona. Hii ni Kona ya 5 Kwa Yanga wakati Ruvu hawajapa kona paka sasa
42" Moloko anapaisha akiwa kwenye nafasi nzuri ya kufunga. What a miss!
45" Shambulizi lingine langoni mwa Ruvu shooting lakini mpira unakwenda nje.
HT" Naaam ni mapumziko katika uwanja wa Benjamin Mkapa Wananchi wakiongoza kwa bao 1-0 dhidi ya Ruvu shooting.
Tukutane kipindi cha pili
"Kipindi cha pili kimeanza
49" Mayele anapoteza nafasi ya wazi kufunga goli la pili Kwa Yanga akiwa yeye na goli
62" Mayele anapiga kichwa kikali langoni mwa Ruvu shooting lakini golikipa anatoa mpira nje inakuwa kona ambayo haikuzaa goli
65" Yanga wamefanya mabadiliko ya wachezaji watatu kwa mpigo, wametoka Musonda, Farid,Moloko na Nafasi zao zimechukuliwa ni Mzize, Ambundo pamoja na Aziz K
Mechi imechangamka sana
80" Bado Yanga anaongoza kwa goli 1-0
87" Yanga wanapata faulo eneo zuri, Aziz K anapiga gooal lah lah golikipa wa Ruvu shooting anadaka vizuri kabisa
90+3" Naam mpira umekwisha hapa Uwanja wa Benjamin Mkapa timi ya Yanga inaondoka na alama zote 3 na kuzidi kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya Nbc kwa kufikisha jumla ya point 56 huku Ruvu shooting wakisalia mkiani mwa msimamo wa ligi.
Mlikuwa nami Babu Onyango kwa Dak zote 90 za mtanange huu
hadi wakati mwingine