Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa wana tuhuma nzito za ufisadi wa Website ya CHADEMA

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wana body, amani iwe kwenu.

Taarifa za kuaminika ambazo intelijensia ya Lizaboni imepata ndani ya CHADEMA ni kwambaFreeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA na Katibu Mkuu Dr Slaa wanahujumu pesa ambazo zilitengwa kwa ajili ya kuendeshea Website ya chama ambayo ni Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo – Chadema. Kwamba, kiasi cha shilingi milioni 25 kilitengwa kila mwezi na mfadhili mkuu wa chama, taasisi ya Ujerumani ya CAS kwa ajili ya kuboresha mfumo wa kusambaza taarifa za chama kupitia website hiyo. Kwamba fedha hizo zimeingizwa kwenye akaunti ya chama na zinatolewa kila mwezi kwa maelezo eti zinatumika kulipa mishahara waandishi wa mtandao huo, kugharamia gharaza za simu, tozo mbalimbali na matumizi mengine.

Cha kushangaza ni kwamba, hakuna hata mwandishi mmoja ambaye anapokea mshahara kutokana na kazi ya kuandika kwenye mtandao huo. Inaelezwa pia kuwa kwa sasa mtandao huo hauna msimamizi maalum na inaelezwa kuwa Dr Slaa alisitisha ajira za vijana waliokuwa wanaandika taarifa kwenye mtandao huo mwishoni mwa Oktoba 2014 kwa maelezo kuwa mtandao unafanyiwa ukarabati. Miongoni mwa vijana ambao ajira zao zilisitishwa ni pamoja na Ben Saanane, Yeriko Nyerere, Michael Aweda na wengineo.

Intelijensia ya Lizaboni baada ya kupata taarifa hiyo ilijiridhisha kwa kutembelea mtandao huo. Ilichokikuta ni aibu tupu. Pamoja na mtandao kupambwa kwa rangi mbalimbali za CHADEMA, hauna taarifa mpya hata moja licha ya matukio mengi kutokea ndani ya nchi yetu. Tukio la karibuni ni sakata la AKAUNTI ya ESCROW ambalo lilipamba vyombo vyote vya habari hapa nchini. Cha kushangaza ni kwamba, kwenye mtandao huo wa Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo – Chadema hakuna mada yoyote inayohusu sakata la ESCOW. Uchunguzi wa Intelijensia ya Lizaboni umegundua kuwa taarifa tatu za mwisho ambazo zimewekwa kwenye mtandao huo ni hizi zifuatazo;

  1. SIRI ZA CCM KUHUJUMU KATIBA YA WANANCHI ZAFICHUKA ( Iliyowekwa tarehe 5/11/2014)
  2. TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA( Imewekwa tarehe 9/10/2014) na
  3. MKUTANO MKUU WA CHAMA KUMCHAGUA MWENYEKITI TAIFA LEO (imewekwa tarehe 14/9/2014)

Kutokana na hali hiyo, fedha hizo wanagawana Mwenyekiti, FREEMAN MBOWE ambaye anapata mgawo wa shilingi milioni 8, Katibu Mkuu, Dr Slaa anapata shilingi milioni 7, Mkurugenzi wa Fedha wa chama, Anthony Komu anachukua shilingi milioni 5 na kiasi kinachobaki kinatumika kuendeshea blog ya chama ambayo ni chademablog.blogspot.com ambayo pia gharama za uendeshaji ni ndogo.

Hakika hii inatisha. Ni ajabu kubwa kwa watu wanaojifanya kuwa wanapinga ufisadi kumbe wao ni mafisadi wakubwa.

Bado tuna safari ndefu katika kupambana na ufisadi.

Nawasilisha
 
Mtu wa IT wa chadema ni JOSEPHINE MUSHUMBUSI, (mke?) wa SLAA. Hiyo ndio chadema bwana. Sasa ajitokeze panya yoyote aandike waraka kuhusu hili jambo, viongozi wala hawatajibu waraka bali wataitisha mkutano watasema "huyu ni msaliti, pipoooo?" mazombi yataitikia "pawaaaaa", "afukuzwe, pipooooo?" mazombi "pawaaaaa". kwishnei!


"Mr Wasira who is also Minister of State in the President's Office, Civil Society Relations and Coordination, has called for Dr Slaa to come clean on reports that his spouse, Ms Josephine Mushumbusi has forced CHADEMA officials to pay her 10m/-.

Mr Wasira alleged that the money was meant to pay one Ms Mushumbusi to install computer software to be used to manage CHADEMA's accounts, even though the party already had a computer expert to do the job. Addressing a series of campaign rallies in Ngarenanyuki Ward of Meru District, Mr Wasira said that CHADEMA was wrong to pay such large sums of money to Dr Slaa's spouse on unofficial arrangements."

source: http://archive.dailynews.co.tz/index.php/local-news/3165-wasira-accuses-slaa-of-self-interest
cc: FaizaFoxy.
 
Last edited by a moderator:
Milioni 25 za kwenye tovuti na bilion 300 plus za kashfa moja tu ya TEGETA ESCROW. Sijui nani fisadi hapa lakini kwa akili yangu ya kuzaliwa billions ni greater amount than millions. Let say ni kweli 25 million zimeliwa je ni wangapi labda kwa population ya TANZANIA wamekuwa affected compared to those TEGETA ESCROW billions? Nawaza kwa sauti tu.
 
Naona Ben Saanane na wenzakeyalishawashinda, Yeriko Nyerere ndo bado anapumulia mashine huku mitandaoni akitafuta fadhila.
 
Milioni 25 za kwenye tovuti na bilion 300 plus za kashfa moja tu ya TEGETA ESCROW. Sijui nani fisadi hapa lakini kwa akili yangu ya kuzaliwa billions ni greater amount than millions. Let say ni kweli 25 million zimeliwa je ni wangapi labda kwa population ya TANZANIA wamekuwa affected compared to those TEGETA ESCROW billions? Nawaza kwa sauti tu.
.....toa kwanza fedha halali za kulipia umeme toka kwenye hiyo 300bilioni.
......Rais kashasema fedha hazikuwa za umma. Ndio maana mpaka sasa hakuna kesi ya kurudisha fedha.
......kwenye hizi za chama ni rahisi kuchukua maamuzi. kwa nini maamuzi hayajachukuliwa?
 
Dada Eliza Boni mbona unahangaika sana na CHADEMA! Kuna mchumba alikutosa kukuoa? Tatizo siwezi kuoa wake wawili dini yangu hairuhusu ningejitolea tu ili usije kuwa chizi bure!
ndiyo maana cybercrime anasema mmefanywa mazuzu, badala mchukue hatua kunusuru fedha za chama kutoka kwenye SACCOS mnatukana watu?
 
Milioni 25 za kwenye tovuti na bilion 300 plus za kashfa moja tu ya TEGETA ESCROW. Sijui nani fisadi hapa lakini kwa akili yangu ya kuzaliwa billions ni greater amount than millions. Let say ni kweli 25 million zimeliwa je ni wangapi labda kwa population ya TANZANIA wamekuwa affected compared to those TEGETA ESCROW billions? Nawaza kwa sauti tu.
Mkuu, kwa hiyo unahalalisha matumizi ya kifisadi ndani ya chadema hata kama ni kwa kiasi kidogo? Kwako milioni 25 kwa mwezi ni fedha ndogo? Hakika kuna watu wana laana kweli
 
Lizaboni

wazee wa ufipani na vijana wake, mjibu kwa hoja wacheni mahaba kwa slaa na mbowe
 
Last edited by a moderator:
Hii project ya kusha na uwachafuahawa viogozi haijawahi kuwasaidia CCM, pamojana feda zote zilzomwawa na CM wapambe waaane kuwachfa miandaoni ndio kanz Dr Slaa na Mbowe wanaendelea kuwatwanga CCM kiasi cha kukosa usingizi wakisikia majina yao
 
Ifike wakati tuweni wakweli kama tunakemea wizi au ufisadi tusitake side. Hivi tuseme haya mauzauza yanayoendelea ya mali na fedha za umma kuibiwa tunaona ni sawa? Hivi tuko radhi kuutetea uovu kwa ajili tu ya mapenzi na chama flani? Sidhani kama iko sawa. Hebu tuwekeni uzi ambao tunaweza kujadili namna ya kujikwamua kiuchumi vijana wenzangu. Mwaka wa uchaguzi huu kila neno litasemwa tu. Hebu tujadilini namna ya kumpata kiongozi mwenye uzalendo,utashi na ambaye atakuwa dira ya kuleta taifa lenye uchumi imara na thabiti.
 
Back
Top Bottom