anunuliwe mara ngp, bado za lowasa haijaisha...Vip huyo dau limekataa maana kumsajili huyo Sio kazi ndogo
anunuliwe mara ngp, bado za lowasa haijaisha...Vip huyo dau limekataa maana kumsajili huyo Sio kazi ndogo
Igwe wanaJF
Zama za mfalme Suleiman paliwahi kutokea wanawake wawili wakigombea mtoto, mmoja akiwa ni kahaba. Ili kuamua ile kesi Mfalme Suleiman aliwapa uchaguzi ya kuwa mtoto yule agawanywe kisha kila mwanamke apate kipande kuepusha zogo. Yule kahaba huku akifurahia alikubali mtoto agawanywe lakini yule mwanamke mwenye huruma alimwambia Mfalme Suleiman asimkate yule mtoto amwache abaki hai.Mfalme kwa hekima na busara kubwa aliamua mtoto yule apewe huyu mama mwenye huruma na sio kahaba hii ni kwa mujibu wa biblia takatifu.
Pamoja na kupewa ushauri wenye manufaa Mbowe ameweka pamba sikioni huku asionyeshe kujali mustakaabli wa Chadema na wafuasi wake. Kwa mkono wake ameamua kuwasujudia aliowahi kuwakejeli na kueneza siasa chafu dhidi yao huku akiwadhibiti na kuwafurumusha wote wenye kumpa changamoto chanya.
Ni ngumu kuamini japo ndio hali halisi leo vijanaa asili ndani ya Chadema wakipuuzwa ili kuwafurahisha vijana wa 4U movement huku kibehi dhidi yao ikipata baraka zote bila kukemewa.
Ni ngumu leo kuelewa falsafa ya Chadema, pesa nyingi zinatuka katika kampeni za chaguzi ndogo/marudio badala ya kukijenga
Wee jamaa una akili sana!Habari zenu, binafsi nitangaze interest kuwa ni muumini wa democrasia (multipartism) licha ya kuwa ni mwanachama wa chama kimoja cha siasa.
Niseme kwa dhati kabisa nakutoa angalizo kuwa USIONE UKADHANI maana kuona tu hakutoshi kuthibitisha ukweli ( observation isn't enough to reveal the truth). Nasema hivi maana hapa wenda kuna watu siyo muda watanishambulia sababu tu wao wanalinda chama chao na kudhani wengine hatuna vyama ila kuna wakati tunasimama katikati..!
Baada ya maelezo mafupi twende SAKO KWA BAKO kwenye mjadala.
Binafsi namuona mh. Freeman Mbowe kama mzimu au jinamizi lingine linaloikabili Demokrasia ya Tanzania. Wengi hamtanielewa maana hapa ni watu wenye ubongo mkubwa (bigbrain people) ndiyo wataelewa ninachotaka kusema. Sababu ni kama zifuatavyo:-
Kwanza mh. Mbowe hajawahi kuwa mwanasiasa na hawezi kuwa mwanasiasa licha kuwa amebahatika (kiujanjaujanja) kushika madaraka ya kisiasa kwenye chama na bungeni. Nasema hivi maana ukweli ni kuwa mh. Mbowe nje ya maslahi yake ya kibiashara siasa kwake si kitu ni upuuzi mtupu, sasa mtu wa namna hii utasema ni mwanasiasa sababu hana political vision ya kusomea au kuzaliwa huyu jamaa naweza kumtuita MJASIRIA MALI WA SIASA (political entrepreneur man).
Pili kuthibitisha haya kama kuna mtu makini atanielewa, binafsi sijawahi kushiriki siasa za nchi hii kwa maana ya kugombea/kuwanis cheo ndani ya chama cha siasa kiwacho nchini humu au nafasi ya uongo wa umma/serikali ingawa nimufuatiliaji murua/mzuri wa siasa za nchi hii kwa zaidi ya miaka 20 sasa. Mh. Mbowe anaonekana katika wajihi/wasifu wake wa kisiasa akipanda tu vyeo bila yeye kuonesha ubora wake katika siasa za nchi hii, ni mtu anayefurahia kuvuna asipopanda Mbowe nimjuaye ni mtu ambaye hajawahi kupata political grievances(misukosuko ya kisiasa) hapo kabla ila kwa wakati huu wa mh. Magufuri. na pia hii misukosuko ni yake binafsi zaidi na siyo ya kichama.
Tatu, huu ni ushuhuda kwa wenye macho ya ubongo, Mh. Mbowe tangu utawala wa awamu ya tano(mh. Magu) aingie madarakani amemudu kumnyamazisha sababu alimjua vyema na mbinu rahisi imekuwa ni kucheza maslahi ys huyu jamaa (Mbowe), SIASABIASHARA (politic-business) ndiyo mchezo wa mh. Mbowe ndiyo nikamwita (political entrepreneur man), wafanyacho CCM ni kumshika kwenye maslahi yake naye ameufyata.
Nne, bila shaka mtamkumbuka katibu mkuu wa CHADEMA wa zamani dr. Wilbroad Slaa(maarufu kama DR.MIHOGO-waneno ya wafia chama) alikuwa ni moyo/mtima wa chama cha CHADEMA alifanya mengi yaliyompa sifa yeye na chama chenyewe (CHADEMA), huku mh. Mbowe akibaki kuvuta utamu kwa mrija mrefu aliouchomeka ndani ya mtungi (chadema) mwisho Mh. Mbowe na mchezomchezo wake wa ajabu akamleta LOWASSA alininangwa na ambaye aliaminika kwa maelfu ya wafuasi wa chadema kuwa fisadi mkuu akatumbukia ndani ya mtungi dr. Slaa huyo akasepa alitukanwa sana. Ila madhara sasa hivi mnayaona kumbuka dr. Slaa alionya sana juu ya VIJANA WAPENDA MAGEUZI alisema ni jambo jema ila kutaka mageuzi bila kujua nini unachotaka kugeuza ni kupotea kwa mara ya pili.
Tano, nisiwachoshe, Mh. Mbowe na Mh. Lowassa niwe tu muwazi hawa watu ni sawa karibia kwa kila kitu, sifa nilizompa Mh. Mbowe na Lowassa anazo sasa kazi ya CCM ni nyepesi mno, nijuavyo mh. Lowassa anajus fika hawezi kuchukua nchi hii, ila anachofanya ni kutafuta hifadhi ya kiasiasa kwa ajili ya biashara zake, ni wazi kwa trend ya siasa za hii nchi Lowassa na chadema wanapoteza umaarufu na sababu ccm wanejua namna ya kuwathibiti na palipo na Mbowe na Lowassa yupo pembeni (birds with same color flock together) huu mchezo hauhitaji hasira.
Mwisho nitoe tu angalizo upinzani kuwa na watu wenye kashifa, maslahi binafsi ya kisiasa na ambao system (ccm) inawajua vyema hakika kifo chao hakitaepukika maana ccm knows well the point/angle of their weaknesses.
Jifunzeni kwa wabunge kama Mnyika ni kati ya wabunge wanaopata shida kufanya kazi na viongozi km Mbowe, Lowassa, Sumayi na wengine wenye mizizi isiyo safi. Twende turudi upinzani(chadema/cuf) mjitafakari upya hasa vyama vikuu ya upinzani kuweni makini. Mafanikio ya ghafla yataangamiza upinzani nchini jengeni, wafundeni, na kuwalea viongozi vijana kwa ajili ya viongozi wa kesho. Chadema na Cuf zina zaidi ya miaka 20 iweje hazijengi vijana wake kwa kuwapa uwezo kiuongozi, kuwafunda wanaishia kutoa vyeo kwa ndugu, jamaa, marafiki, maslahi, ukanda, na nepotism za ajabu huku wakituacha wenye haki tukilia (usije dhani nina maslahi) mbinu za kisanii, mapigo wanayopata ni mazao ya usaliti wa vijana wanaojituma kupigania na kujenga chama ila hawalipwi na kupewa stahiki za uanachama wao.
Mtanitukana najua, ila ukweli siku zote lazima utamalaki tuu.
Anzisha chama chako ama ujiunge na huyu unayemshabikia pambafffff!Kwa mwendo wa Magufuli ,Mbowe ameshindwa kuja na fikira mpya za kuendesha chama ,Tafadhali tuachie chama.
Ndugu zang na wanachama wenzang hili nimeliona na bado najiuliza ni kutokana na elim yake (from 6 zero) imeshindwa kuendana na Docta Magufuli au nini,Tafadhali Mbowe tuachie chama.
Yangu ni hayo tu.
Ebu onesha kadi yako ya uanachama you Expansion jointsKwa mwendo wa Magufuli ,Mbowe ameshindwa kuja na fikira mpya za kuendesha chama ,Tafadhali tuachie chama.
Ndugu zang na wanachama wenzang hili nimeliona na bado najiuliza ni kutokana na elim yake (from 6 zero) imeshindwa kuendana na Docta Magufuli au nini,Tafadhali Mbowe tuachie chama.
Yangu ni hayo tu.
akionesha utajisikiaje?Ebu onesha kadi yako ya uanachama you Expansion joints
umelazimishwa kuwa cdm?unaweza kushuka na kudandia gari lingine kama kafulila na wengineo wanavyofanya usilete unafiki hapaKwa mwendo wa Magufuli ,Mbowe ameshindwa kuja na fikira mpya za kuendesha chama ,Tafadhali tuachie chama.
Ndugu zang na wanachama wenzang hili nimeliona na bado najiuliza ni kutokana na elim yake (from 6 zero) imeshindwa kuendana na Docta Magufuli au nini,Tafadhali Mbowe tuachie chama.
Yangu ni hayo tu.
we unasema chama sio mali yake unaijua vizuri historia ya chadema wewe??Kwa mwendo wa Magufuli ,Mbowe ameshindwa kuja na fikira mpya za kuendesha chama ,Tafadhali tuachie chama.
Ndugu zang na wanachama wenzang hili nimeliona na bado najiuliza ni kutokana na elim yake (from 6 zero) imeshindwa kuendana na Docta Magufuli au nini,Tafadhali Mbowe tuachie chama.
Yangu ni hayo tu.
atajitetea kwamba kwa kuwa ana makalio makubwa basi yeye ni genius kwa kuwa akiba ya akili kaihifadhi sehemu hiyo pendwa!Hamna mwanachama wa chadema kibaka namna hii,Navyojua CDM wote wana akili kubwa.Wewe una makalio makubwa