Bumpkin Billionare
JF-Expert Member
- Jan 5, 2012
- 1,332
- 621
Huu mchezo wa kupenda kupiga domo kwenye vyombo vya habari unaofanywa na mabondia wa hapa nyumbani pindi wanapoomba pambano na dume la milima ya Uluguru utaisha lini?
Jana, Karama Nyilawila amepata zawadi ya kuropoka baada ya kukong'otwa TKO ya round ya 6 katkia pambano la masumbwi lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA kurasini DSM dhidi ya Francis Cheka.
Awali Karama Nyilawila alijigamba (kama ilivyo ada ya mabondia wote wenye njaa) kuwa Cheka hana ubavu wa kumshinda na hata pambano alilopigwa Moro Cheka alipendelewa tu na majaji.
Sasa jana ndio alijua kwa nini mfuko wa Rambo haubebewi kaa la moto. Round ya 6 kalamba sakafu, refa kahesabu mpk mia, hajaamka.
Chezea CHEKA wee, waulize ukoo wa Matumla, mpk wakastaafu ngumi.
Promota Bumpkin Billionare nataka orodha ya mabondia uchwara wote wanaotaka kupigwa (na sio kupigana, Cheka hapigani) na Cheka wajiandikishe ili niweze kuandaa ratiba ya wao kupigwa.
Cheka hoyeeeeeee!
Madam Maugo asijiandikishe, ameshapigwa vya kutosha awaachie na wenzake nao wapigwe
Jana, Karama Nyilawila amepata zawadi ya kuropoka baada ya kukong'otwa TKO ya round ya 6 katkia pambano la masumbwi lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA kurasini DSM dhidi ya Francis Cheka.
Awali Karama Nyilawila alijigamba (kama ilivyo ada ya mabondia wote wenye njaa) kuwa Cheka hana ubavu wa kumshinda na hata pambano alilopigwa Moro Cheka alipendelewa tu na majaji.
Sasa jana ndio alijua kwa nini mfuko wa Rambo haubebewi kaa la moto. Round ya 6 kalamba sakafu, refa kahesabu mpk mia, hajaamka.
Chezea CHEKA wee, waulize ukoo wa Matumla, mpk wakastaafu ngumi.
Promota Bumpkin Billionare nataka orodha ya mabondia uchwara wote wanaotaka kupigwa (na sio kupigana, Cheka hapigani) na Cheka wajiandikishe ili niweze kuandaa ratiba ya wao kupigwa.
Cheka hoyeeeeeee!
Madam Maugo asijiandikishe, ameshapigwa vya kutosha awaachie na wenzake nao wapigwe
Last edited by a moderator: