Forex: Milionea Sandile Shezi kutua Dar es Salaam Jumamosi

Hahaha Asije akazingirwa na JWTZ, Maana Gavana wetu hataki usanii kwenye pesa yetu. Ila hawa matajiri wasiku hizi wana niacha hoi kitu kimoja. Eti wamekuwa naroho nzuri sana, wanataka nasisi masikini tuwe matajiri, Mashaka yangu yako hapo, MATAJIRI HUWA NI CLASS NYINGINE, Natena huwa hawapendi kuishi uswahilini nasisi MASIKINI. Na hujinadhifu ili kuonyesha tofauti yao na sisi wazi wazi, ukimuona TAJIRI hata huulizi, anaonekana tu. Na huwa hawanaga haya mambo YAKUTUFUNDISHA Masikini tuwe matajiri. Yaani jiulize lini umewahi kumsikia Mzee Mengi, Rostam Aziz, MO, Mfuruki, Bkhresa na wengine unaowafahamu, eti wanatoa SEMINAR kwetu masikini ili nasisi tuwe matajiri?! Lakini hii sampuli ya akina Ontario imekazana kwelikweli, mimi sitaki niwe fursa.
 
Back
Top Bottom