Sumba-Wanga
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 5,349
- 1,224
Jamaa ni mshamba sana, hana mpya kabisa...
Fuatilieni vizuri hii habari na wala Shigongo si wa kulaumiwa hiyo juu ni fabrication ya huyo Chamelion ni habari ya uzushi na anastahili kupigwa chini kwani ana dharau kwa watanzania.mi namsapoti sana Shigongo kwa kuliweka wazi suala hili alipoongea na waandishi wa habari.
Erick ni mnafiki mkubwa,
wamemalizana ameomba msamaha,
kwanini hakukomaa kuomba msamaha kama yeye ni kidume.
mkuu, sikitika kwanza kabla ya kumlaumu huyu bwana!
Mjasiliamali mzuri daima ni yule anayeweza kubaini gap kati ya kinachotakiwa na wanaokitaka na akitumia hiyo nafasi vizuri ananeemaka.
Shigongo alibaini ujinga wa ndugu zetu wengi kuwa wameathirika na mfumo mbovu wa elimu yetu na badala ya kutumia hiyo nafasi kuwasaidia akaamua kuitumia kwa kuwajaza ujinga zaidi. Na kinachotokea/kitakachotokea huko mbeleni ni ujinga kuongezeka kutokana na 'sumu' aliyotulisha.
Juzi Chameleon alipiga kambi ubalozi wa Tanzania nchini Uganda pale Kagera Road na hilo tukio lili-draw attention ya Waganda na uwezi jua ni wangapi wamejenga mtazamo hasi kuanzia hapo. Yote hayo sababu ya mtu mmoja kufanya mambo ya kipuuzi kwa makusudi mazima.
Ngoja tusubiri lakini historia inaweza kumkumbuka kwa kutumia 'ujinga' wa Watanzania kujitajirisha kama wanasiasa wengine badala ya kutoa mchango wa kuwaelimisha kwa kuwapa ufahamu
mimi binafsi nalisubiri gazeti ambalo siku moja litampiga picha za uchi Eric shigongo na mke wake wakiwa uchi halafu lizibandike picha zake ukurasa wa mbele. hakyanani hilo gazeti nitalinunua hata kwa elfu 30, kama nitakutwa nazo mfukoni. Huyu ni mpuuzi na mshenzi mno. halafu eti naye anaji-rank mjasiriamali. what a shame!!!!!! kupata riziki kwa biashara ya kishetani kama ya huyu bwana halafu unatembea na kujivuna hadharani, inatia huruma sana. ila kwa wanao mcha Mwenyezi Mungu, sio hawa watu wa shetani kama kina shigongo.
Wadau,
Mimi ni mmoja wa watu tunaopinga mienendo ya Shigongo na magazeti yake lakini kwenye hii issue ya Jose Chameleon lazima tuwe wakweli.
Huyu mganda ana matatizo sana tusifumbwe macho na chuki dhidi ya Shigongo bali pia upande wa pili wa Chameleon.Jamaa amelalamikiwa hadi Kenya na inasemekana hata A.Y alimtahadharisha Shigongo tabia ya udanganyifu ya Chameleon.
Inashangaza msanii wa level kama yake kuwa na tabia za namna hii! Sishangai matukio ya kutaka kujiua kule Impala Arusha,kubadili dini alafu baada ya kususwa na mkewe na watoto akarudia dini yake!
Kwa mafanikio ya kisanaa aliyonayo Chameleon anataka nini tena mbona mtata sana?