Finally, they are telling us.. !!

Mimi wote hawa nawaona kama vibudu tu. Hapa anataka kuwafanya Watanzania waone umasikini ni sehemu ya maisha yao yaani hakuta kuwa na mwanga mpaka miaka 40 ipite!!

Nakupa tano Mtanganyika nadhani umeeleza vizuri zaidi wapi CCM inakosea na ijirekebishe namna gani.
Kwa kauli ya Nduli ina maana JK ni tapeli.Alituahidi Watanzania kutuondolea umasikini katika kipindi cha miaka 5( ndo kipindi cha uongozi alichoomba).

Hii impact ya kukua kwa uchumi, kwanini inawanufaisha Wateule wa CCM,Viongozi wa serikali na wahindi wao??

Mwisho nasema CCM ni cha ambacho kinatuthibitia kwa mara ingine kuwa kimeshindwa kuwaondolea watanzania umasikini kwa kukosa Uongozi bora,Utawala bora,Usimamizi thabiti na mbinu bora za kupambana na umasikini.

80% ya watanzania wanaishi vijijini na wanategemea kilimo cha jembe la mkono. Hivi wanashindwa kuelewa kuwa ku-invest na kuweka effort kubwa kwenye sector ya kilimo pamoja na kutafuta masoko yake, kunaweza impact Watanzania wengi within 8years!! Sasa kama utawaacha hawa waendelee kulima kwa mkono unategemea lini watazalisha kwa wingi na kuboresha maisha yao.
Sasa hivi kuna njaa duniani,Tanzania tuna mabonde mazuri sana Mikoa ya Kagera,Kigoma,Rukwa,Tanga na Kigoma na baadhi ya mikoa ya kusini ambayo hayajaguswa, na tunavua za kutosha kabisa kustawisha mpunga na mahindi na ngano.Lakini tumeshindwa kutumia rasilimali hizi kutuletea neema.
CCM ni chama ambacho kimeshindwa ku-deliver kwa Watanzania, kinatafuta kila mbinu kuhalalisha kushindwa kwao.Waondoke
 
Hivi kuna matumaini gani ya kubadilisha maisha ya watu kama maafanikio ya kazi yao itakuwa ni miongo minne kuanzia sasa? Je wanaweza kufanya lolote ambalo linaweza kuwapa furaha ya matunda ya jasho lao sasa?

Hivi kujenga drainage system kwenye jiji la Dar (leo imenyesha tena mvua na mafuriko kama kawaida) hadi miaka 40 ijayo?

Hivi kuna tatizo gani la kuhakikisha kuwa kuna code za mining na mifumo ya uokoaji ya uhakika katika maeneo ya machimbo hadi miaka 40 ijayo?

Hivi aliyesema kuwa "linalowezekana leo, lisingoje kesho" alikuwa amechanganyikiwa?
 
Economic growth hard to feel - BoT

2008-04-03 08:50:28
By Lydia Shekighenda

The Bank of Tanzania (BoT) has projected that it will be between three and four decades before ordinary wananchi ``feel`` the country`s economic growth.


This is according to BoT Governor Benno Ndulu in a presentation at a forum for researchers and decision-makers in Dar es Salaam yesterday.

Prof Ndulu`s presentation centred on the challenges of growth Tanzania was contending with and was made at an annual research workshop organised by Research on Poverty Alleviation (Repoa).

The BoT chief argued that it was impossible for the results of economic growth to be felt within a short period, adding: ``Last year Tanzania`s economy was projected to have grown by 7.3 per cent.

If we had managed to grow consecutively for a period of 30 to 40 years, then the outcome would have been felt right down to the grassroots level.``

He recommended that greater attention be directed at areas with great potential of leading to positive results in the economy if given the right support.

``We should not focus only on how the economy is growing but also on areas able to provide greater opportunities to our people. This approach could be termed as pro-poor growth,`` he said.

The professor explained that Tanzania`s economy has improved much over the years in terms of structure, sources of growth and exports ``but one of the major challenges ahead is making sure that the country sustains these changes``.

``We should not focus only on how to improve agriculture by providing loans and subsidies on agricultural inputs but we should also come up with strategies with the capacity to bring about positive changes to our economy,`` he pointed out.

The central bank governor also underscored the need for local investors to contribute more substantially to the creation and strengthening of a vibrant private sector.

Opening the workshop, Industry, Trade and Marketing deputy minister Cyril Chami said it was possible to attain and sustain the country`s domestic and global development targets if they were based on a sound domestic economy.

Achievements based mainly on external resources were bound to face problems of sustainability, he asserted, noting that salvation lay in having the country focus on ``the refinement of its growth strategy - which must be brought into sharp focus within the development agenda``.

Repoa executive director Joseph Semboja said the forum has grown into the largest and longest running annual event hosted by his institution.

This year`s participants included researchers, central and local government officials, private sector players, and representatives of civil society organisations, and the donor community.

My Take:

I thought they could just push a button of development no waiting, no time lapsing, no hardship just kavoom!! We have to wait.. that means it'll be about 80 years after independence!! Is this reasonable.. why it couldn't have be done yesterday!!!? This one I blame Nyerere too, it is taking us too long!!!! Why Nyerere why? WE could have been like ze yunaitedi steti of america.

Why can't we just have rapid change? Why Ndulu why? Why do we have to wait? Why can't the government just make it possible? Nyerere is no longer there, in 40 years most of these people would not be here (probably me too).. so why even bother!!

grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr!

LIFE EXPECTANCY YA MTANZANIA NI TAKRIBANI MIAKA 40 NA USHEE..KWA HIYO PROF ANA MAANA MIAKA 40 IJAYO WENGI AU WOTE WALIO HAI LEO WANAWEZA KUWA WAMEKUFA IKIWEMO YEYE...KWA HIYO HAPATAKUWA NA ATAKAYESHUHUDIA AHADI YAKE YA KUFIKIRIKA..

PLEASE GAVANA ..TUNAOMBA MIPANGO YA UCHUMI YA KUBORESHA MAISHA YA MTANZANIA KUANZIA LEO NA MIAKA IJAYO.......
 
dahh

...........anyway kama kuna mtu ana paper yake kamili aliyoi-present please atuwekee hapa tuichambue.....tujue assumptions zipi ametumia........kabla ya hizo judgements zake
 
Dola ya marekani inaporomoka siku hata siku, jee shilingi yetu ambayo imeegemezwa kwenye dola hiyo imesalimika kwenye anguko hilo la Dola?
 
nimeambiwa na gavana kupituia gazeti la last week kuwa wana njia mpya ya kupima uchumi wetu...sikuelwa au labda mimi ni mzito kuelewa.........ila kuhusu shillingi yetu sijui itakuwaje kama ipo pale pale au la........
 
Kitu muhimu zaidi ya exchange rate ni Purchasing Power Parity.

Exchange rate inaweza isituambie chochote kuhusu maendeleo ya kiuchumi,kuporomoka kwa shilingi kinadharia kunaweza kuwa na matokeo mazuri kwa exporters wanaouza nje kwa shillingi (kama tunao) kwa sababu vitu vyetu vitakuwa rahisi zaidi kununua.Vilevile Shilingi kuongezeka thamani inaweza kusababisha export kupungua kwa sababu vitu vinakuwa ghali ku export.Ndiyo maana kuna baadhi ya manufacturers wa Marekani wanafurahia dollar kushuka thamani, na importers wa ulaya wanazidisha manunuzi yao marekani, ndiyo maana China hawataki hela yao ipande thamani na wanaifanya iwe chini artificially.

Kitu cha muhimu zaidi ya short term exchange rate ni effects za long term exchange rate zinazotokea katika PPP.

Ramani hii chini inaonyesha PPP za nchi mbali mbali duniani.

http://en.wikipedia.org/wiki/Image:PPP2003-World-Borders.png
 
Shilingi imepolomoka sana kutoka USD 1163 mwanzoni mwa march na sasa inakimbilia USD 1250 kwa leo asubuhi

Sikubali. Tuliaambiwa na waziri wetu hazina, Mheshimiwa Mkullo "shilingi inafukuzana na dola" na gavana mpya 'Ndulu anafanya maajabu!' Mbona mbishi jamco_za?
 
Sikubali. Tuliaambiwa na waziri wetu hazina, Mheshimiwa Mkullo "shilingi inafukuzana na dola" na gavana mpya 'Ndulu anafanya maajabu!' Mbona mbishi jamco_za?

Mheshimiwa ukiwasikia wanasiasa utapumbazika sana, ni porojo tu. Wanatuzuga tu au wanawazuga wajinga. Thamani ya sarafu haimaanishi hata kidogo level ya uchumi, ukiangalia thamani ya WON ya Korea kusini kimsingi inafanana sana na thamani ya shilingi yetu lakini ukilinganisha uchumi wa Tanzania na uchumi wa Korea Kusini, ni kama utakuwa unalinganisha noti ya shilingi elfu 10 na shilingi 100. Korea wako mbali zaidi.
Siri ya kuinua uchumi wa TAnzania ipo kwenye kuimarisha uzalishaji na exports(any legal exports), hili linawezekana kabisa na limo ndani ya uwezo wetu, lakini serikali yetu haijali hilo au haifanyi kazi za maana kushughulikia hilo. Na hili unaweza kuangalia kwenye B.O.T (balance of Trade), kama kuna uwiano wa tunachopeleka nje na tunachoingiza thamani ya shilingi yetu inaweza kuwa stable au kupanda, lakini ukweli wa mambo sio huo. Hali halisi ni kuwa tunanunua kuliko tunachouza na huenda tutaendelea hivyo kwa muda mrefu kama jamaa hawataacha uzembe, ukiangalia mapato ya TRA kutokana na imports utaona ni makubwa sana, lakini waulize kuhusu exports uone kama watakujibu, watapiga blaablaa tu.
Hapa ndipo siri moja ya mismanagement ya uchumi wetu ilipo, lakini hakuna mwanasiasa atakayekubali.
 
Angalieni takwimu hizo! I guess tupo nyikani miaka arubani ya kusubiri mana kutoka mbinguni huku tukitangatanga jangwani!

Tanzania, United Republic of

  • Total population (millions): 38.3
  • Population growth (annual %): 2.0
  • Surface area (sq. km): 945,087
  • GDP per capita (PPP US$): 730
  • GDP growth (annual %): 5.9
  • Inflation, GDP deflator (annual %): 6.3
  • Unemployment (% of total labor force): N/A
  • Life expectancy at birth (years): 49.7
  • Median age of total population (years): 17.5
  • Human Development Index (Rank 1 - 177): 162
  • Human Development Index Value: 0.4
  • Sex ratio at birth (males per 100 females): 103.0
    goal1_sm.gif

    Goal 1: Eradicate extreme poverty and hunger
  • Population below PPP $1 per day (%): 57.8
  • Children under 5 who are moderately or severely underweight (%): 21.8
  • Population living below the national poverty line (%): 35.7
    goal2_sm.gif

    Goal 2: Achieve universal primary education
  • Net enrolment ratio in primary education (% both sexes): 98.2
  • Percentage of pupils starting Grade 1 and reach Grade 5 (% both sexes): 79.2
    goal3_sm.gif

    Goal 3: Promote gender equality and empower women
  • Gender parity Index in primary level enrolment (ratio of girls to boys): 1.0
  • Literacy rates of 15-24 years old (% both sexes): 78.4
  • Seats held by women in national parliament (%): 30.4
    goal4_sm.gif

    Goal 4: Reduce child mortality
  • Mortality rate of children under 5 years old (per 1,000 live births): 122
  • 1-year-old children immunized against measles (%): 91
    goal5_sm.gif

    Goal 5: Improve maternal health
  • Maternal mortality ratio (per 100,000 births): 1,500
    goal6_sm.gif

    Goal 6: Combat HIV/AIDS, malaria and other diseases
  • People living with HIV,15-49 yrs old (%): 6.5
  • Prevalence of tuberculosis (per 100,000 people): 496
    goal7_sm.gif

    Goal 7: Ensure environmental sustainability
  • Land area covered by forest (%): 39.9
  • Carbon dioxide emissions per capita (metric tons): 0.1160
  • Access to improved drinking water sources (% of total population): 62
    goal8_sm.gif

    Goal 8: Develop a global partnership for development
  • Internet users (per 100 people): 1.0
  • Youth unemployment rate, ages 15-24, both sexes : N/A

NOTE: The MDG data presented here is the latest available from the United Nations Statistics Division.
 
Mheshimiwa ukiwasikia wanasiasa utapumbazika sana, ni porojo tu. Wanatuzuga tu au wanawazuga wajinga. Thamani ya sarafu haimaanishi hata kidogo level ya uchumi, ukiangalia thamani ya WON ya Korea kusini kimsingi inafanana sana na thamani ya shilingi yetu lakini ukilinganisha uchumi wa Tanzania na uchumi wa Korea Kusini, ni kama utakuwa unalinganisha noti ya shilingi elfu 10 na shilingi 100. Korea wako mbali zaidi.
Siri ya kuinua uchumi wa TAnzania ipo kwenye kuimarisha uzalishaji na exports(any legal exports), hili linawezekana kabisa na limo ndani ya uwezo wetu, lakini serikali yetu haijali hilo au haifanyi kazi za maana kushughulikia hilo. Na hili unaweza kuangalia kwenye B.O.T (balance of Trade), kama kuna uwiano wa tunachopeleka nje na tunachoingiza thamani ya shilingi yetu inaweza kuwa stable au kupanda, lakini ukweli wa mambo sio huo. Hali halisi ni kuwa tunanunua kuliko tunachouza na huenda tutaendelea hivyo kwa muda mrefu kama jamaa hawataacha uzembe, ukiangalia mapato ya TRA kutokana na imports utaona ni makubwa sana, lakini waulize kuhusu exports uone kama watakujibu, watapiga blaablaa tu.
Hapa ndipo siri moja ya mismanagement ya uchumi wetu ilipo, lakini hakuna mwanasiasa atakayekubali.


Bongolander, niliposema Shilingi inafukuzana na dola na Ndulu kafanya maajabu nilikuwa natumia tasnifa. Yani hukuona kwamba ni kichekesho kusema Ndulu kafanya maajabu? Nilikuwa nawadhihaki wakina Mkullo!
 
Ndullu huyu huyu aliyebebwa na mafisadi wa CCM mpaka Butiama, leo anapata ubavu wa kusema "ukweli"?

Au labda tumempata Profesa wa mazingaombwe huko benki kuu? Yote yawezekana Tanzania yetu hii.
 
Back
Top Bottom