Filikunjombe: Serikali ya CCM imevaa miwani ya mbao

Hivi huyu Filikunjombe angekuwa CDM kama akina ZZK,Mdee na kuwachana akina Mbowe,Slaa kama anavyofanya kwa CCM, nini kingetokea? Viongozi wa CDM wanauvumilivu wa kukosolewa?Vijana radicals kama hawa ni muhimu katika jamii.
 
Huu ni mfano wa kuigwa!

Sasa huwa naona WanaJF wakiguswa na hoja za mtu either positively au negatively huhoji maana ya majina ya wahusika.... Filikunjombe nafikiri inaweza kumaanisha pilipili kali.... inayodumu kuwa pilipili bila kujali imewekwa 'mdomo' wa nani!...
 
Anasema wanafanya mambo kwa - funika kombe mwanaharamu apite. Anasema Waziri Mkuu aliapa kuilinda katiba lakini sasa wanachokifanya ni kulindana tu.

Anasema bungeni kuna mawaziri 30 lakini wanaowajibika ni kama 10 na anaweza kuwataja.

Anasema tusifanye kazi za Nape Nnauye bungeni. Anasema tusiwabeze wapinzani kwa kila kitu.

Huyu jamaa anaonekana moyo wake hauko tena CCM.

Source: Bungeni leo asubuhi


Hawa ndiyo wazalendo wanaotakiwa ................... tatizo kubwa la nchi yetu wasafi na wazuri CCM wameamua kukaa kimya kitu ambacho hakitusaidii wote!!
 
Ukiona mwana ccm si mzalendo basi huyo yupo kwa maslahi na tumbo lake. Fili huyu wa kule madunda namfahamu si sana nilipata kuonana nae once maelezo yake tu yalinionyesha ni mtu wa staili gani. huchukia uonevu na hupenda haki ni mtu wa watu wa chini ingawa kwa wakati ule alikua tayari anajiweza mwenyewe. Tatizo hawa ambao maisha mazuri wameyapata kupitia hila za ccm hicyo wanaiabudu ccm kuliko kitu chochote kwani hawawezi simama kwa miguu yao. Hao wamevaa miwavi ya mbao iliyotengenezwa na mti uitwao CCM hawaoni chochote isipokua ccm hata wananchi wao hawawaoni. GOD BLESS FILI
 
Ni mbunge pekee mwenye akili kati ya wabunge wote wa CCM. Wengine ni bendera fuata upepo!
 
aa hapana kaka punguza mkari basi ss kama wapenda maendeleo ungepaswa umpongeze kisha umwombe aongeze kazi, nguvu na ari mpya ktk kuikosea serikali pale inapokosea si lazima aje ila afanye wajibu wake kama mbunge hicho ndo tunataka si lazima uwe mbunge wa cdm hata hao waccm kama alivyoonyesha njia MHESHIMIWA DEO
ndani ya ccm hakuna uhuru wa kutoa maoni hata hayo aliyosema tayari yameshamuweka matatani,. wewe hukumbuki alivosaini kumuondoa waziri mkuu aliitwa na kuhojiwa??akiwa nje ya ccm atatoa mchango mpana zaidi kwa maendeleo ya taifa letu!
 
Awataka wabunge CCM waache kufanya kazi za NAPE na wawajibike badala ya kufanya SIASA BUNGENI. WASIPOPATA meli katika jimbo lake wataandamana muda wowote na mahala popote, amekataa kuunga mkono hoja ya waziri mkuu hadi mambo ayatakayo yatimizwe.

Njano5.
Rangi, Umeeleweka.
 
Hawa ndiyo wazalendo wanaotakiwa ................... tatizo kubwa la nchi yetu wasafi na wazuri CCM wameamua kukaa kimya kitu ambacho hakitusaidii wote!!

Bora waongee sasa kwani wakijakungea baadae baada ya ukombozi tutawaaminije?
 
UKO SAWA DEO -IMEVAA MIWANI KWANI UONGO,HAYA YANATHIHIRISHA.

1.HALI NGUMU YA MAISHA nauli/kodi juu wakati kipato ni kile kile
2.HUDUMA ZA AFYA MBAYA.DAWA hakuna zikiwepo zaenda kwa hospital binafsi.
3.UBINAFSI WA VIONGOZI WETU -Kujilimbikizia mali kila mahali.Kufa kufaana
4.UFISADI -Dowans na Richmond
5.MIKATABA MIBOVU.Idara za madini na mali asili
6.KULINDANA KUNAKOLETA VIONGOZI WABOVU.Watoto wa vigogo kila penye idara nyeti nenda TRA,BOTn.k
7.UTAPANYAJI WA MALI NA RASILIMALI ZA UMMA.Magari ya umma kwa issue binafsi
8.KUONGEZEKA KWA TABAKA LA WALIONACHO NA WASIONACHO.Tajiri na masikini
9.KUTUMIA RASILIMALI ZA NCHI KUENEZA PROPAGANDA NA CHUKI.
10.UKOSEFU WA AJIRA.64% ya wahitimu ni jobless
11.VIWANDA VINGI KUFA NA KUFANYWA MAGOFU.
12.UKOSEFU WA HAKI KWENYE VYOMBO VYA MAAMUZI MFANO MAHAKAMA.
13.MIGOGORO KILA KONA HASA YA ARDHI ,WAWEKEZAJI KWANZA MZAWA BAADAYE..loliondo,kiteto n.k
14.MIFUMO MIBOVU YA UONGOZI HIVYO KUSABABISHA MZIGO MKUBWA KWA SERIKALI mfano vyeo vya ajabu tu kila
kona.
15.SIASA CHAFU HASA KWENYE MASUALA YA MSINGI MFANO MAJI AMBAYO NI ISSUE MUHIMU TEMBELEA SHY
TOWN,NZEGA,TABORA YOTE,SIMIYU,MPANDA KWA PINDA,DODOMA,DSM,MANYARA,GEITA ,BUNDA,N.K HAKUNA MAJI.
16.UJAMBAZI ULIKITHIRI WA RASILIMALI ZA TAIFA MFANO WANYAMA KUTOROSHWA.
17...........
 
Bila shaka Filikunjombe ni mbunge makini na wa kuigwa na magamba maana itakuwaje mtu utoe mapungufu na mwisho wa siku upitishe kwa kukubali kwa 100% ? huu ni unafiki kama c ujuha au aina yoyote ya umbumbumbu wa fikra. tunategemea mb AMBAYE atakosoa bajeti bac asiunge mkono hoja na kama ataikubali asitoe kasoro. yaan kuna wabunge hawajui wajibu wa mawaziri wanafikia hatua ya kufanya kazi mawaziri, halafu kuna swali huwa najiuliza iv ukiwa ccm ni lazima uwe na fikra na mawazo mgando maana naona kama maprofesa wamegeuka na wanaonekana kama si watu wa kuwaza mambo ya maana ma Dr ndo kabisa mfno wa Dr wa Nzega. tubadilike tuende na wakati hongera Mp Filikunjombe hakika umeonesha njia na utakuwa ni mfano wa kuigwa kwa wengine wapendao uzalendo.
 
Yaani kweli Bungeni ukuwasema wapinzani kwa lugha mbaya unasifiwa, kama jana Mkamia alivyoendelea baada ya kumtukana Sugu, leo Filikunjombe kalazimishwa kutoa neno miwani ya Mbao, ila ndo hivyo Waziri Mkuu hapo anapata machungu na kukumbuka yale majina ya wabunge waliosaini kutokuwa na imani naye, Filikunjombe alikuwa muwazi na si mnafiki kama wengine:rockon:
Nampomgeza na kumkubali sana Filikunjombe. Huyu ni mbunge aliye makini na mwenye mawazo huru yenye taswira ya maslahi ya taifa: si mnafiki. Wenzake wa chama chake wanamuona kwa jicho baya: Nadhani hakufaa kuwa CCM maana mawazo yake hayafanani na ya wao.
 
Back
Top Bottom