Kamuibia nani hapo?Enyi mliokua mnabishia UFISADI wa Ndugu Lowassa bila huruma kwa taifa lake, na wallahoi tulio wengi kila kona ya nchi hii na ugumu wa maisha, hebu sasa semeni tena!!!
Hakuna ubishi kwamba Mgombea mtarajiwa wa magamba ni fisadi. Huu ni uthibitisho mwingine wa ufisadi wake. Sijui fisadi Lowassa alilipa kodi kiasi gani kutokana na bulungutu lake hilo.
Hii habari ni ya siku nyingi sana. Nyie ndio mnaishushia hadhi JF. Hebu mod ondoeni huu uzi!!!
kwa hakika inashangaza kwa kumuona Lowassa kuwa ni fisadi kwa dili hili. Kinachoonekana hapa ni kuwa alifanya biashara halali na hao wasomali na ndio maana walikubali kumlipa. Labda kama alivyosema BAK, kama hakulipa kodi ya mapato kutokana na kipato hicho, hapo ndipo penye tatizoHivi hapo kuna ufisadi gani
jamani, au kuuza kitu chako kwa shea ni ufisadi. Sibishi kuwa mamvi ni
fisadi ila hivi kwani nani sio fisadi? Bora fisadi mfanyakazi na
mtafutaji au fisadi pumbafu anaetuibia na hatuoni anachofanya wala
hatusaidii?
Kamuibia nani hapo?
Haujui alilipa kodi kiasi gani af unadai kafanya ufisadi, labda utuambie kamuibia nani kwenye hiyo biashara?
Hii habari ni ya siku nyingi sana. Nyie ndio mnaishushia hadhi JF. Hebu mod ondoeni huu uzi!!!
Hii kampuni ya kisomali ilipata mtaji wapi wa kuweza kuwekeza nchini? Isije kuwa ni wasomali ambao walikuwa wanateka meli za makampuni mbali mbali duniani na kisha kuomba mapesa chungu nzima ili kuziachia meli hizo. Na mapesa yao hayo yaliyopatikana kwa njia za haramu ndio sasa wanakuja kuzitakaza Tanzania.
Kuna tatizo lipi Lowassa akifanya biashara na Wasomali, mlitaka afanye nao Mbowe pekee?
Umeshaenda Bilicanas? mpaka machangu wa kisomali wanafanyia biashara zao hapo, pitia ukaone.
Mkuu Zomba hebu funguka kidogo, wenzako tunachokihoji tena kwa nguvu zote hapa ni kwamba wewe na wenzako wote humu MKATUTAJIE AMA AINA YA BIDHAA AU HUDUMA ambayo Mzee Lowasa alipata kuwauzia WaSomali kwa hiyo thamani kubwa ya Milioni 450 ili ubishi na mshaka uishe.
1. Mzee Lowassa, kwa kuwa ni mwenyekiti wa kamati ya Usalama nchini, je aliwauzia Wasomali HAKI YA KUPITA nchini hadi Dodoma bila kustukiwa na vyombo vyetu vya usalama?
2. Je, aliwauzia WaSomali au watu walioko nyuma ya WaSomali ardhi ya ndugu zetu WaMasai na kufanywa kuwa Taifa la Uarabuni ndani ya mipaka yetu ya Tanzania?
Toa jibu la moja kwa moja bila kuzunguka buyu hapa.
But the guy is a businesman na wote tunajua hivyo so nashindwa kuthibitisha ufisadi hapa maana barua hiyo imesema tu anazotudai labda tungejua zilikuwa ni zanini otherwise inaweza ikawa ni clean money!