paartey
Member
- Jun 26, 2023
- 39
- 53
FEMI (play boy)
MTUNZI: PATRICIA ANTONY
SEHEMU YA: 01
MAWASILIANO: 0783642467
Anza nayo.....
Femi kijana fulani hivi machachali ambaye shida anaisikia tu kwa wengine wanavyosema maisha ya shida maisha sijui hivi, Femi amezaliwa kwenye familia yenye pesa sana ambapo baba yake na mama yake mzazi wamekuwa wakiishi Marekani miaka na miaka, ila femi alibaki Tanzania akiwa na bibi yake yaani bibi alimtaka mjukuu wake bibi pia yuko vizuri sana kwenye mambo ya pesa lakini hakuwa bibi yule mzee watu wangu wa nguvu wanasemaga wabibi wa mjini bibi amekuwa akimuacha mjukuu wake afanye kile anachokisikia bibi anahakikisha account ya mjukuu wake iko full mda wote anafanyiwa anachokitaka picha linaanza nyumbani kuna wadada wa kazi wawili na mkaka wa garden mmoja
Femi amekuwa mtu wa kulala na kuamka tu agusi kitu chochote zaidi ya simu yake na kula tu sio mtu wa kufanya kazi ata kufua anafuliwa na wadada wake na kama wewe ni mfanyakazi wa ndani halafu ukamfanya femi kuchukia basi vita itaama kutoka kwa femi mpaka kwa bibi yake.
SONGA NAYO....
Ilikuwa siku ya jumanne kama kawaida shughuli za hapa na pale ziliendelea kijana femi majila ya saa nne (4) asubuhi ndio alikuwa anatoka usingizini yaani ndio anaamka
"Brandina nani anatakiwa kufanya usafi ndani kwangu ?"
Aliuliza femi baada tu ya kutoka chumbani kwake na kwenda sebuleni, brandina ni mmoja kati ya wafanyakazi wao
"Ni mimi nilikuwa nikisubili uamke...."
"Kafanye chap nina mgeni wangu anakuja muda sio mrefu nisingependa apakute vile....."
"Sawa kaka...."
"Wewe hivi hayo mambo ya kuniita kaka nimekuambiaje ?? Eeeh mimi sio kaka ako halafu unataka nikose nini kutoka kwako ?? Usije ukaru......."
Kabla hajamaliza kuzungumza simu yake ya mkononi iliita
"Hallow..."
Alizungumza femi baada tu ya kupokea simu akakaa kimya kwa muda akisikiliza sauti ya upande wa pili kisha akaendelea
"Aaah ndo hivyo fanya kweli kwenye presentation me siji leo subira anakuja nyumbani nitakuwa nae....."
Waliongea sana baada ya muda akarudi chumbani kwake
"Mbona mashuka ubadilishi sasa ??"
"Eeeh....."
Alimuuliza brandina ambaye kwa kumtazama tu unajua kuwa alikuwa akimuogopa sana femi
"Nikuulize kitu brandina wewe uwa ausikii vizuri au mtu akizungumza unakuwa na mawazo yako mengine ??"
"Nakuelewa kaka "
"Sasa unaniuliza mara mbili mbili ili iweje ??
"Samahani, naomba nibadilishe na nimalize kufanya usafi nitakuita "
"Unataka nikakae nje ?? Una akili wewe ? Halafu embu njo....."
Femi alimuita brandina kwa dharau sana brandina alizidisha uoga na kubaki akiwa ameganda tu na kumtazama femi kwa wasiwasi
"Njoo basi..
."
Alizungumza femi na alipoona kuwa brandina amfati akainuka alipokuwa amekaa na kumsogelea zaidi
"Hivi ujawai kufikilia kuwa na mimi ?? Yaani na uzuri wangu huu unakubalije kutandika kitanda kwaajili ya wenzio.??"
Alizungumza femi uku akijaribu kumshika shika brandika
"Kaka femi niachie nimalize kazi natakiwa kwenda sokoni pia "
Alilalamika brandina lakini malalamiko yake hayakufua dafu femi alionesha kudhamilia kufanya jambo baya kwa brandina wa watu ambaye alionekana kuwa msichana mpole na mtulivu sana
"Kaka femi......"
Ilisikika sauti ya juu sana ikiita kutokea sebuleni hapo femi alistuka na kutoka ili kujua nani alikuwa akiita hakuwa mwingine Bali ni mdada wa kazi mwingine aliyejulikana kama zuhura
"Kuna mgeni wako huyu sijui unamafahamu"
Alizungumza zuhura uku akioneshea mkono mlangoni
"Oooh subira wangu jamani karibi kipenzi "
Alizungumza femi na kumfata subira na kumkumbatia
"Karibu sana nimefurahi kukuona "
Alizungumza femi kwa furaha sana muda wote huo zuhura alikuwa ameganda akimshangaa femi
"Kaendelee na kazi zako "
Alizungumza femi na zuhura hakuwa na namna zaidi aligeuka na kutoka kuelekea jikoni
"Oooh utamletea juice chumbani na sambusa "
Alitoa oda femi na msichana yule alifanya kama ambavyo aliagizwa....
"Ujamaliza tu kufanya usafi ??"
Alifoka femi akimfokea brandina kuwa amechelewa kufanya usafi
"Baby ongea nae taratibu ata hivyo mimi nipo leo nafikili kilichobaki ni mimi kushika majukumu yangu "
Alizungumza subira akiamini kuwa kuletwa kwenye nyumba hiyo ni kweli anapendwa eeeh hayo mawazo kwa mwanaume huyu yaani huyu femi ondoa kabisa anachojua yeye ni shwaaaaah..... kupita na wadada yaani hakuna mdada mzuri anayepita kwenye macho yake bila yeye kummezea mate lakini pia michezo yake amekuwa akiicheza kwa akili sana anaweza akatembea na wasichana kama watatu tena marafiki na wasijuane yuko vizuri sana femi ni kijana wa ovyo hakuna mjadala.
Basi mwaya subira wa watu pasi na kujua kuwa chumba iko ni kama dangulo alifanya usafi ulioenda shule alifanya kila kitu kama mwanamke aliyeolewa na kujali familia yake, hakuishia hapo tu alitoka nje na kwenda kuungana na wafanya kazi kwajili ya kuandaa chakula
"Leo nipo kwaajili yenu jamani msinionee huruma ni wajibu wangu "
Hayo maongezi kwa muda huo yalikuwa yakifanyika jikoni ambapo subira alikuwa bize na mapishi na kila kitu alifanya mwenyewe hakuitaji ata kusaidiwa
"Lakini madamu akikukuta unafanya kazi kama hivi tutagombezwa sana "
"Wasiwasi wenu nini ?? Wifi yenu na nusu nishafika kila kitu kitakuwa sawa...."
Ila subira mbwa huyu atakuja kulia vibaya akija kujua kuwa anapitiwa tu maana daaah ameamua kujiveka majukumu makubwa mno.....
"Demu mazinguo huyu tangu amefika anaangaika na kufanya kazi za ndani ananikera hatari can you imagine tangu amefika yuko bize na kazi za ndani kama roboti wala hayuko romantic "
Alilalamika femi akiwa kitandani kwake na alikuwa akiongea na rafiki yake ambaye walionekana kuwa na karibu sana....
Baada ya muda subira alipakua chakula na bila kupoteza muda alichukua chakula na kumpelekea femi na sio tu kumpelekea alimlisha kabisa ila mbwa huyu namuonea huruma femi sio wa hivyo kabisa..I.......
Majila ya saa 2 usiku bi femi alikuwa amesharudi nyumbani alimkuta subira na walika kwa muda wakazungumza mawili matatu, sasa baada ya yote muda subila kuondoka uliwadia femi hakuwa na budi kumuaga ile wanatoka tu nje ya geti waka.....Waka......
ITAENDELEA
MTUNZI: PATRICIA ANTONY
SEHEMU YA: 01
MAWASILIANO: 0783642467
Anza nayo.....
Femi kijana fulani hivi machachali ambaye shida anaisikia tu kwa wengine wanavyosema maisha ya shida maisha sijui hivi, Femi amezaliwa kwenye familia yenye pesa sana ambapo baba yake na mama yake mzazi wamekuwa wakiishi Marekani miaka na miaka, ila femi alibaki Tanzania akiwa na bibi yake yaani bibi alimtaka mjukuu wake bibi pia yuko vizuri sana kwenye mambo ya pesa lakini hakuwa bibi yule mzee watu wangu wa nguvu wanasemaga wabibi wa mjini bibi amekuwa akimuacha mjukuu wake afanye kile anachokisikia bibi anahakikisha account ya mjukuu wake iko full mda wote anafanyiwa anachokitaka picha linaanza nyumbani kuna wadada wa kazi wawili na mkaka wa garden mmoja
Femi amekuwa mtu wa kulala na kuamka tu agusi kitu chochote zaidi ya simu yake na kula tu sio mtu wa kufanya kazi ata kufua anafuliwa na wadada wake na kama wewe ni mfanyakazi wa ndani halafu ukamfanya femi kuchukia basi vita itaama kutoka kwa femi mpaka kwa bibi yake.
SONGA NAYO....
Ilikuwa siku ya jumanne kama kawaida shughuli za hapa na pale ziliendelea kijana femi majila ya saa nne (4) asubuhi ndio alikuwa anatoka usingizini yaani ndio anaamka
"Brandina nani anatakiwa kufanya usafi ndani kwangu ?"
Aliuliza femi baada tu ya kutoka chumbani kwake na kwenda sebuleni, brandina ni mmoja kati ya wafanyakazi wao
"Ni mimi nilikuwa nikisubili uamke...."
"Kafanye chap nina mgeni wangu anakuja muda sio mrefu nisingependa apakute vile....."
"Sawa kaka...."
"Wewe hivi hayo mambo ya kuniita kaka nimekuambiaje ?? Eeeh mimi sio kaka ako halafu unataka nikose nini kutoka kwako ?? Usije ukaru......."
Kabla hajamaliza kuzungumza simu yake ya mkononi iliita
"Hallow..."
Alizungumza femi baada tu ya kupokea simu akakaa kimya kwa muda akisikiliza sauti ya upande wa pili kisha akaendelea
"Aaah ndo hivyo fanya kweli kwenye presentation me siji leo subira anakuja nyumbani nitakuwa nae....."
Waliongea sana baada ya muda akarudi chumbani kwake
"Mbona mashuka ubadilishi sasa ??"
"Eeeh....."
Alimuuliza brandina ambaye kwa kumtazama tu unajua kuwa alikuwa akimuogopa sana femi
"Nikuulize kitu brandina wewe uwa ausikii vizuri au mtu akizungumza unakuwa na mawazo yako mengine ??"
"Nakuelewa kaka "
"Sasa unaniuliza mara mbili mbili ili iweje ??
"Samahani, naomba nibadilishe na nimalize kufanya usafi nitakuita "
"Unataka nikakae nje ?? Una akili wewe ? Halafu embu njo....."
Femi alimuita brandina kwa dharau sana brandina alizidisha uoga na kubaki akiwa ameganda tu na kumtazama femi kwa wasiwasi
"Njoo basi..
."
Alizungumza femi na alipoona kuwa brandina amfati akainuka alipokuwa amekaa na kumsogelea zaidi
"Hivi ujawai kufikilia kuwa na mimi ?? Yaani na uzuri wangu huu unakubalije kutandika kitanda kwaajili ya wenzio.??"
Alizungumza femi uku akijaribu kumshika shika brandika
"Kaka femi niachie nimalize kazi natakiwa kwenda sokoni pia "
Alilalamika brandina lakini malalamiko yake hayakufua dafu femi alionesha kudhamilia kufanya jambo baya kwa brandina wa watu ambaye alionekana kuwa msichana mpole na mtulivu sana
"Kaka femi......"
Ilisikika sauti ya juu sana ikiita kutokea sebuleni hapo femi alistuka na kutoka ili kujua nani alikuwa akiita hakuwa mwingine Bali ni mdada wa kazi mwingine aliyejulikana kama zuhura
"Kuna mgeni wako huyu sijui unamafahamu"
Alizungumza zuhura uku akioneshea mkono mlangoni
"Oooh subira wangu jamani karibi kipenzi "
Alizungumza femi na kumfata subira na kumkumbatia
"Karibu sana nimefurahi kukuona "
Alizungumza femi kwa furaha sana muda wote huo zuhura alikuwa ameganda akimshangaa femi
"Kaendelee na kazi zako "
Alizungumza femi na zuhura hakuwa na namna zaidi aligeuka na kutoka kuelekea jikoni
"Oooh utamletea juice chumbani na sambusa "
Alitoa oda femi na msichana yule alifanya kama ambavyo aliagizwa....
"Ujamaliza tu kufanya usafi ??"
Alifoka femi akimfokea brandina kuwa amechelewa kufanya usafi
"Baby ongea nae taratibu ata hivyo mimi nipo leo nafikili kilichobaki ni mimi kushika majukumu yangu "
Alizungumza subira akiamini kuwa kuletwa kwenye nyumba hiyo ni kweli anapendwa eeeh hayo mawazo kwa mwanaume huyu yaani huyu femi ondoa kabisa anachojua yeye ni shwaaaaah..... kupita na wadada yaani hakuna mdada mzuri anayepita kwenye macho yake bila yeye kummezea mate lakini pia michezo yake amekuwa akiicheza kwa akili sana anaweza akatembea na wasichana kama watatu tena marafiki na wasijuane yuko vizuri sana femi ni kijana wa ovyo hakuna mjadala.
Basi mwaya subira wa watu pasi na kujua kuwa chumba iko ni kama dangulo alifanya usafi ulioenda shule alifanya kila kitu kama mwanamke aliyeolewa na kujali familia yake, hakuishia hapo tu alitoka nje na kwenda kuungana na wafanya kazi kwajili ya kuandaa chakula
"Leo nipo kwaajili yenu jamani msinionee huruma ni wajibu wangu "
Hayo maongezi kwa muda huo yalikuwa yakifanyika jikoni ambapo subira alikuwa bize na mapishi na kila kitu alifanya mwenyewe hakuitaji ata kusaidiwa
"Lakini madamu akikukuta unafanya kazi kama hivi tutagombezwa sana "
"Wasiwasi wenu nini ?? Wifi yenu na nusu nishafika kila kitu kitakuwa sawa...."
Ila subira mbwa huyu atakuja kulia vibaya akija kujua kuwa anapitiwa tu maana daaah ameamua kujiveka majukumu makubwa mno.....
"Demu mazinguo huyu tangu amefika anaangaika na kufanya kazi za ndani ananikera hatari can you imagine tangu amefika yuko bize na kazi za ndani kama roboti wala hayuko romantic "
Alilalamika femi akiwa kitandani kwake na alikuwa akiongea na rafiki yake ambaye walionekana kuwa na karibu sana....
Baada ya muda subira alipakua chakula na bila kupoteza muda alichukua chakula na kumpelekea femi na sio tu kumpelekea alimlisha kabisa ila mbwa huyu namuonea huruma femi sio wa hivyo kabisa..I.......
Majila ya saa 2 usiku bi femi alikuwa amesharudi nyumbani alimkuta subira na walika kwa muda wakazungumza mawili matatu, sasa baada ya yote muda subila kuondoka uliwadia femi hakuwa na budi kumuaga ile wanatoka tu nje ya geti waka.....Waka......
ITAENDELEA