Mkuu, pia ujue matumizi yake ktk kujilinda, vinginevyo ndiyo itatumika na hiyo mijitu kukumaliza.jifunze kulala na silaha chini ya godoro lako
Cc KakaJambazina majambazi nao wanasoma hapa
Kwa kuongezea tu ukilala na kahaba inabidi ukeshe kama bundi!maana utajikuta unapata tabu saaana!Tafadhali chukua dakika chache kupitia maoni haya
1. Majambazi kwa kawaida huanzisha mashambulizi yao kupitia mlango wa nyuma (kawaida milango ya jikoni) kwa sababu kwa kawaida hawaonekani. Weka milango mizuri jikoni kwako. Tumia "chuma cha kukatisha" ama "Kizuiawezi" nyuma ya milango ndani ya nyumba. Kama una funguo "Kizuiawezi," kamwe usiache ndani ya kufuli. Kama inawezekana, tumia kufuli kwa kuongeza. lengo ni kuleta ugumu kadiri inavyowezekana kwa wezi kuingia ndani ya nyumba na kukuongezea wewe muda wa kuwaita watu kwa msaada.
2. Unaposikia mtu anavunja mlango wako, kama huna unahakika kabisa vitendo vyako vitazuia kuingia ndani ya nyumba, usijaribu kuwa shujaa kwa kusukuma nyuma ya mlango (Wanaweza kukupiga risasi kupitia mlangoni), au kuweka vitu vizito kama jokofu au makochi (Wanapatwa na hasira zaidi na kama watafanikiwa kuingia ndani wanaweza kufanya ukatili vibaya mno).
3. Kama unalala bila nguo au na nguo kidogo, Vaa haraka mara tu uwasikiapo. Kwa wanawake hasa, usijaribu kubaki na nguo za kulalia. Vaa suruali na blauzi isiyovutia.
4. Iwapo umepiga simu kwa mtu kwa msaada, weka simu mbali nawe kama vile huitaki ili usijulikane kuwa umepiga simu.
5. Angalia sehemu ya kukatia umeme kwenye nyumba yako kisha zima umeme iwe giza nyumba yote (hii itawachanganya na kusababisha wakimbie.
6. Kama una bunduki, imesajiliwa au la, itumie lakini tu kama una unauhakika kuwa unaweza kuwasababishia madhara. Huu siyo muda wa kupiga risasi juu kuwatisha! Mauaji ya mvamizi katika eneo la nyumba yako wakati wa kujilinda mwenyewe na mali zako ni halali kisheria upande wa utetezi. Pia hata ukitumia silaha nyingine yoyoyte kama vile kisu.
7. Wakati Majambazi wamefanikiwa kuingia wape chochote wakitakacho. Usifiche chochote. Usijaribu kuwa Jasiri wala kujadiliana nao.
8. Usiwatazame moja kwa moja (au usiwafanye wajue kuwa unafanya hivyo). Kama unamfahamu yeyote kati yao usioneshe dalili zozote za kumtambua na wala usitaje jina lake. Hata hivyo kariri maumbile yoyote unaweza kusaidia na kutambulisha katika uchunguzi.
9.Wakati hatimaye wanaondoka katika nyumba yako usiwafukuzie ..
10. Kuwa mlinzi wa jirani yako kama utasikia uvunjaji katika nyumba zao, piga simu polisi kwa msaada.
11. Wakati Majambazi yanaingia kwenye eneo la nyumba yako, usiwashe taa yoyote katika chumba chako. Washa taa za nje lakini zima taa za ndani zote ili majambzi/wezi wasiweze kukuona.
Mbwa Walinzi wanakubalika sana majumbani kwa ajili ya kutoa taarifa mara kitu kigeni cha hatari kinapokuwa kwenye eneo.
Mwenye mawazo ya ziada anaweza kuongezea
Mzee wamkute binti na kichupi unadhani watamuacha hivi hivi?lazima wambakeHapo kwenye kuvaa suruali ngumu na blauzi isiyovutia, naomba ufafanuzi
Hahaha..tunalala kwenye mkeka nini mkuu??Mpaka nikishakua nacho cha kuwafanya majambazi wanitamani nitarudi tena
Huyo atakua sio jambazi ni kibaka tuMbinu nyingine wakiwa wanahangaika kuvunja mlango au dirisha lako jitahidi kuwasoma wako eneo gani,kisha fungua mlango uwe wazi,wasipo kuona wakati ukifungua mlango na wakakuta uko wazi lazima wasepe
Haya jambazi ana roho piaHuyo atakua sio jambazi ni kibaka tu