Idimi
JF-Expert Member
- Mar 18, 2007
- 14,970
- 10,462
Yaah Thomas Edson alikuwa mkali sana, ni mfano mzuri sana wa kutokata tamaa, kuna kitu alikuwa anakiona, PICHA AKILINI, ambayo hakuna mtu mwingine alikuwa anaiona ni sawa na Steve Jobs wa Aple Computer na falsa yake ya "Computer as simple to use as toaster".
Watu woote waliofanikiwa hakukubali kukatishwa tamaa na mtu awaye yote au mazingira au kushindwa mara kadhaa, waling'ang'ania kile walichokuwa wanakiona akilini mwao VISION au MAONO, Hii ndio msukumo mkubwa wa mafanikio yao.
Unapokuwa na MAONO au VISION ya jambo fulani unakuwa na picha halisi kichwani mwako, hivyo kushindwa kunageuka kuwa njia ya kujifunza. Maono yoyote lazima yakumbane na vikwazo tena vikubwa, lakini kama ni halisia ndani ya mtu, haijalishi vikwazo gani vitaibuka havitakuwa na uwezo wa kuua MAONO/VISION ya mtu isipokuwa mtu mwenyewe.
Wengi tunaosema tumeshindwa ni kwasababu twakosa hii kitu MAONO/VISION, na hakika si kama tunakuwa tumeshindwa bali tumeacha kujaribu, tukumbuke Quitters never win.
Asante sana Komandoo kwa kutuletea nukuu hizi.
Ubarikiwe kwa kufafanua zaidi. Lengo langu ilikuwa hasa kuamsha mjadala juu ya 'vision and mission'. Ni wanaofikiri 'Kiwendawazimu' hasa, ambao hufanikiwa. Hiyo picha iliyo kichwani mwa mtu hakika hakuna mtu mwingine anayeiona exactly kama huyo mmiliki ama mtengenezaji wa picha hiyo.
Katika mojawapo ya maandiko yake, Edson anasema aliulizwa swali "What is electricity and how does it look like?" Akatoa jibu fupi tu, "I don't know, but try it and you will see"
Nakubali kwamba 'Quiters Never Win'. What matters is persistence.