Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Hitimisho kwa michuano ya Kombe la Azam Sports Federation Cup (ASFC) kwa mchezo wa fainali kupigwa leo Julai 2, 2022 kwenye Dimba la Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha, ambapo Mabingwa wa Nchi kutoka viunga vya Jangwani Yanga SC, wanakwaruzana na Wajuzi wa soka Wagosi wa Kaya Coastal Union kutoka mkoani Tanga.
Mchezo huu unatarajiwa kuwa mkali mno na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika 90, kutokana na aina ya uhitaji wa mechi hiyo kwa kila timu, ambapo Yanga SC wakiwa na dhamira ya kuweka historia kutwaa ubingwa ngao ya Jamii, Ligi Kuu na ASFC, huku Coastal Union pamoja na kuhitaji sana ubingwa huu ASFC vile vile wakitaka kuwakilisha nchi kwenye michuano ya Kimataifa.
Nani kuweza kuibuka na ubingwa wa (ASFC) Kombe hili lenye mvuto na la pili kwa ukubwa nchini Tanzania? Nidhamu ya kujilinda na kushambulia ndo majibu yatapatikana baada ya mchezo kumalizika..Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 9: 00 Alasiri, Usikose Ukaambiwa Mwana Kulipewa Wewe..!
Twende pamoja..!
Nyomi ya mashabiki uwanja wa Sheikh Amri Abeid wapo kwenye foleni tayari kwa ajili ya kuingia kushuhudia mtanange wa ASFC.
==========================
Wakati wowote mpira utaanza Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Timu zote zipo tayari.
05' Naaam mpira umeanza kwa kasi huku kila timu ikichukua tahadhari kubwa, kuepusha makosa dakika hizi za mwanzo.
10' Sopu Goooooooooooaaal goal
Abdul Sopu anaipatia Coastal Union bao la kwanza baada ya Krosi mujarabu kutoka kwa Akpan
15' Yanga wanakosa nafasi mbili mfululizo za wazi kupitia kwa Mayele, kazi nzuri kwa golikipa wa Union
20' Mwamnyeto anaonyeshwa KADI ya Njano kwa kumchezea madhambi mchezaji wa Union, ni Free Kick kuelekea Yanga.
Uwanja umejaa huku Coastal Union wakitakata dakika hizi za mwanzo, wapo mbele kwa bao moja.
Kuna mchezaji Vincent wa Coastal yupo chini baada ya kupata rabsha, mpira unaendelea.
25' Yanga wamepata Kona tatu ambazo hazikuzaa bao, mabeki wa Coastal wapo imara
30' Abubakar wa Yanga anashindwa kutulia na kuweza kuweka mpira kambani, ilikuwa nafasi nzuri kabisa.
35' Coastal wamefanikiwa kudhibiti presha ya Yanga kipindi hiki cha kwanza, labda Yanga waje na mbinu tofauti
40' Shambulizi kali kuelekea Yanga, mpira unapigwa mbele, lakini golikipa Diara anacheza.
Mpira unachezwa kwake Mayele, lakini mabeki wanakataa..Ngoma ni ngumu.
45+3' Kuelekea kuwa mapumziko ambapo Coastal wapo mbele ya bao moja.
Faisal anapiga shutii lakini linapaa nje ya lango la Coastal Union.
Kona inapigwa kuelekea Coastal, inapigwa kulee mpira unamkuta Akpan anagonga kichwa na unamkuta Mayele anapiga Tikitaka lakini inakata.
Naaam mpira ni mapumziko, Kumbuka mchezo wa ASFC
HT: Yanga SC 0-1 Coastal Union
Kipindi cha pili kimeanza huku Yanga wakipata Kona ambayo haikuzaa bao
Ametoka Chiko na ameingia Makambo upande wa Yanga SC
50' Yanga wanajaribu kutafuta mpenyezo kwa mabeki wa Coastal, lakini mipango yao inakuwa migumu
Miraji anaonyeshwa KADI ya Njano, ni free kick kuelekea Coastal, inapigwa kulee lakini mpira unaokolewa
57' Feisal Goooooooooooooaaal.. Feisal anaisawazishia Yanga SC bao akipokea pasi kutoka kwa Makambo
Aucho anapiga shutii lakini linachezwa na kuwa Kona ambayo imedakwa na golikipa Mussa.
61' Mubarak Hamza anakosa nafasi nzuri ya kufunga, yeye na golikipa Diara..!
Mpira umeanza kuamka kwa pande zote mbili kupelekea mashambulizi mazito
Pascal Kitenge ameingia kuchukua nafasi ya mtu, upande wa Coastal Union
70' Coastal Union wanapanga mipango sasa, mpira unapigwa mbele lakini golikipa Diara anacheza mpira ule.
Joseph Ziwa anaonyeshwa KADI ya Njano kwa mchezo mbaya, huku Coastal wakifanya mabadikio ameingia Chambo.
73' Makambo anakosa nafasi nzuri ya kufunga ilikuwa Shambulizi kali kuelekea Coastal
75' Feisal Ooooh, anakosa nafasi nzuri ya kufunga, mpira wake umepaa juu ya lango.
Coastal wanakosa nafasi tena, mpira unaambaa ambaa unatoka nje ni wa kurusha, Akpan yupo chini akipatiwa matibabu.
81' Makambo Goooooooooooooaaal gooal.. Makambo anaipatia Yanga SC bao la pili, shuti kali la kimo cha mbuzi linamuacha golikipa Mussa akichumpa bila mafanikio.
Haya mpira ni mkali sana hii ni hadhi ya fainali sasa.
Sopu Goooooooooooaaal goal
Abdul Sopu anaipatia Coastal Union bao la pili, akijitwisha kichwa na kumuacha golikipa Diara akiangalia tu Kijana hatari sana.
Ngoma nzito sana, Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, piga nikupige.
90+4' Kuelekea kumalizika kwa mchezo huu
Mayele anakwenda, anapiga shutii lakini Ziwa anacheza na kuokoa hatari ile.
Aucho katika ya uwanja, anapiga kumtafuta Makambo, lakini Coastal Union wanakaa imara.
Naaam dakika 90 zinakamilika, sasa ni wakati wa dakika za za nyongeza au mikwaju ya penalty mpaka bingwa apatikane.
FT: Yanga SC 2-2 Coastal Union
Naaam mpira unaendelea dakika za nyongeza, Yanga wanapata Kona ambayo haikuzaa bao.
92' Farid anapiga kona nyingine lakini mabeki wa Coastal wanakaa imara kuondoa hatari ile.
98' Sopu Goooooooooooaaal goal
Abdul Sopu anaweka kambani bao la tatu Hat-trick baada ya kuwazidi mbio mabeki wa Yanga
Ametoka Mwamnyeto na ameingia Nkane upande wa Yanga SC
Vicente Abubakar anashindwa kutuliza mpira wa Krosi, ilikuwa nafasi nzuri kufunga bao
105' Yanga wanashambulia lango la Coastal, lakini mabeki wanakaa imara kuondoa hatari.
106' Golikipa Mussa yupo chini baada kukumbana na Mayele, anapatiwa matibabu.
110' Mpira unaendelea huku Bangala akimsukuma mchezaji wa Coastal, Yanga wanapigwa baridi hapa.
113' Nkane Goooooooooooooaaal gooal, Nkane anaweka kambani bao la tatu | Yanga SC 3-3 Coastal Union
Akpan anagonga kichwa lakini mpira unatoka nje, ilikuwa nafasi murua hapa,
Ameingia Haji na ametoka Vicente Abubakar upande wa Coastal Union
Diara yupo chini akipatiwa matibabu, ameinuka mpira unaendelea, Kona inapigwa kuelekea Yanga, lakini mpira unatoka upande mwingine.
Sopu anamgeuza Aucho, hatariii anapiga shutii gooo laaaaaa, ilikuwa hatari tunazika kabisa.
120' Unapigwa mbele kuleee kwake golikipa Mussa akichumpa na kudaka
Naaam mpira umekwishaaaaaa ambapo Timu zote zikitoka sare ya mabao matatu kwa matatu, sasa ni mikwaju ya penalty.
=====
Yanga SC wametwaa ubingwa wa ASFC, baada ya kuibuka na ushindi mabao 4-1 kwa mikwaju ya Penalty baada ya kumalizika kwa dakika 120 za nyongeza kwa kufungana mabao 3-3 dhidi ya Coastal Union.
FT: Yanga SC 2-2 Coastal Union
Extra Time: Yanga SC 3-3 Coastal Union
Penalty: Yanga SC 4-1 Coastal Union
...... Ghazwat..
Mchezo huu unatarajiwa kuwa mkali mno na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika 90, kutokana na aina ya uhitaji wa mechi hiyo kwa kila timu, ambapo Yanga SC wakiwa na dhamira ya kuweka historia kutwaa ubingwa ngao ya Jamii, Ligi Kuu na ASFC, huku Coastal Union pamoja na kuhitaji sana ubingwa huu ASFC vile vile wakitaka kuwakilisha nchi kwenye michuano ya Kimataifa.
Nani kuweza kuibuka na ubingwa wa (ASFC) Kombe hili lenye mvuto na la pili kwa ukubwa nchini Tanzania? Nidhamu ya kujilinda na kushambulia ndo majibu yatapatikana baada ya mchezo kumalizika..Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 9: 00 Alasiri, Usikose Ukaambiwa Mwana Kulipewa Wewe..!
Twende pamoja..!
Nyomi ya mashabiki uwanja wa Sheikh Amri Abeid wapo kwenye foleni tayari kwa ajili ya kuingia kushuhudia mtanange wa ASFC.
==========================
Wakati wowote mpira utaanza Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Timu zote zipo tayari.
05' Naaam mpira umeanza kwa kasi huku kila timu ikichukua tahadhari kubwa, kuepusha makosa dakika hizi za mwanzo.
10' Sopu Goooooooooooaaal goal
Abdul Sopu anaipatia Coastal Union bao la kwanza baada ya Krosi mujarabu kutoka kwa Akpan
15' Yanga wanakosa nafasi mbili mfululizo za wazi kupitia kwa Mayele, kazi nzuri kwa golikipa wa Union
20' Mwamnyeto anaonyeshwa KADI ya Njano kwa kumchezea madhambi mchezaji wa Union, ni Free Kick kuelekea Yanga.
Uwanja umejaa huku Coastal Union wakitakata dakika hizi za mwanzo, wapo mbele kwa bao moja.
Kuna mchezaji Vincent wa Coastal yupo chini baada ya kupata rabsha, mpira unaendelea.
25' Yanga wamepata Kona tatu ambazo hazikuzaa bao, mabeki wa Coastal wapo imara
30' Abubakar wa Yanga anashindwa kutulia na kuweza kuweka mpira kambani, ilikuwa nafasi nzuri kabisa.
35' Coastal wamefanikiwa kudhibiti presha ya Yanga kipindi hiki cha kwanza, labda Yanga waje na mbinu tofauti
40' Shambulizi kali kuelekea Yanga, mpira unapigwa mbele, lakini golikipa Diara anacheza.
Mpira unachezwa kwake Mayele, lakini mabeki wanakataa..Ngoma ni ngumu.
45+3' Kuelekea kuwa mapumziko ambapo Coastal wapo mbele ya bao moja.
Faisal anapiga shutii lakini linapaa nje ya lango la Coastal Union.
Kona inapigwa kuelekea Coastal, inapigwa kulee mpira unamkuta Akpan anagonga kichwa na unamkuta Mayele anapiga Tikitaka lakini inakata.
Naaam mpira ni mapumziko, Kumbuka mchezo wa ASFC
HT: Yanga SC 0-1 Coastal Union
Kipindi cha pili kimeanza huku Yanga wakipata Kona ambayo haikuzaa bao
Ametoka Chiko na ameingia Makambo upande wa Yanga SC
50' Yanga wanajaribu kutafuta mpenyezo kwa mabeki wa Coastal, lakini mipango yao inakuwa migumu
Miraji anaonyeshwa KADI ya Njano, ni free kick kuelekea Coastal, inapigwa kulee lakini mpira unaokolewa
57' Feisal Goooooooooooooaaal.. Feisal anaisawazishia Yanga SC bao akipokea pasi kutoka kwa Makambo
Aucho anapiga shutii lakini linachezwa na kuwa Kona ambayo imedakwa na golikipa Mussa.
61' Mubarak Hamza anakosa nafasi nzuri ya kufunga, yeye na golikipa Diara..!
Mpira umeanza kuamka kwa pande zote mbili kupelekea mashambulizi mazito
Pascal Kitenge ameingia kuchukua nafasi ya mtu, upande wa Coastal Union
70' Coastal Union wanapanga mipango sasa, mpira unapigwa mbele lakini golikipa Diara anacheza mpira ule.
Joseph Ziwa anaonyeshwa KADI ya Njano kwa mchezo mbaya, huku Coastal wakifanya mabadikio ameingia Chambo.
73' Makambo anakosa nafasi nzuri ya kufunga ilikuwa Shambulizi kali kuelekea Coastal
75' Feisal Ooooh, anakosa nafasi nzuri ya kufunga, mpira wake umepaa juu ya lango.
Coastal wanakosa nafasi tena, mpira unaambaa ambaa unatoka nje ni wa kurusha, Akpan yupo chini akipatiwa matibabu.
81' Makambo Goooooooooooooaaal gooal.. Makambo anaipatia Yanga SC bao la pili, shuti kali la kimo cha mbuzi linamuacha golikipa Mussa akichumpa bila mafanikio.
Haya mpira ni mkali sana hii ni hadhi ya fainali sasa.
Sopu Goooooooooooaaal goal
Abdul Sopu anaipatia Coastal Union bao la pili, akijitwisha kichwa na kumuacha golikipa Diara akiangalia tu Kijana hatari sana.
Ngoma nzito sana, Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, piga nikupige.
90+4' Kuelekea kumalizika kwa mchezo huu
Mayele anakwenda, anapiga shutii lakini Ziwa anacheza na kuokoa hatari ile.
Aucho katika ya uwanja, anapiga kumtafuta Makambo, lakini Coastal Union wanakaa imara.
Naaam dakika 90 zinakamilika, sasa ni wakati wa dakika za za nyongeza au mikwaju ya penalty mpaka bingwa apatikane.
FT: Yanga SC 2-2 Coastal Union
Naaam mpira unaendelea dakika za nyongeza, Yanga wanapata Kona ambayo haikuzaa bao.
92' Farid anapiga kona nyingine lakini mabeki wa Coastal wanakaa imara kuondoa hatari ile.
98' Sopu Goooooooooooaaal goal
Abdul Sopu anaweka kambani bao la tatu Hat-trick baada ya kuwazidi mbio mabeki wa Yanga
Ametoka Mwamnyeto na ameingia Nkane upande wa Yanga SC
Vicente Abubakar anashindwa kutuliza mpira wa Krosi, ilikuwa nafasi nzuri kufunga bao
105' Yanga wanashambulia lango la Coastal, lakini mabeki wanakaa imara kuondoa hatari.
106' Golikipa Mussa yupo chini baada kukumbana na Mayele, anapatiwa matibabu.
110' Mpira unaendelea huku Bangala akimsukuma mchezaji wa Coastal, Yanga wanapigwa baridi hapa.
113' Nkane Goooooooooooooaaal gooal, Nkane anaweka kambani bao la tatu | Yanga SC 3-3 Coastal Union
Akpan anagonga kichwa lakini mpira unatoka nje, ilikuwa nafasi murua hapa,
Ameingia Haji na ametoka Vicente Abubakar upande wa Coastal Union
Diara yupo chini akipatiwa matibabu, ameinuka mpira unaendelea, Kona inapigwa kuelekea Yanga, lakini mpira unatoka upande mwingine.
Sopu anamgeuza Aucho, hatariii anapiga shutii gooo laaaaaa, ilikuwa hatari tunazika kabisa.
120' Unapigwa mbele kuleee kwake golikipa Mussa akichumpa na kudaka
Naaam mpira umekwishaaaaaa ambapo Timu zote zikitoka sare ya mabao matatu kwa matatu, sasa ni mikwaju ya penalty.
=====
Yanga SC wametwaa ubingwa wa ASFC, baada ya kuibuka na ushindi mabao 4-1 kwa mikwaju ya Penalty baada ya kumalizika kwa dakika 120 za nyongeza kwa kufungana mabao 3-3 dhidi ya Coastal Union.
FT: Yanga SC 2-2 Coastal Union
Extra Time: Yanga SC 3-3 Coastal Union
Penalty: Yanga SC 4-1 Coastal Union
...... Ghazwat..