Faida ya chakula bora

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,322
33,127
SAMAKI (FISH)

• Huyayusha damu, huifanya kuwa nyepesi
• Huilinda mishipa ya damu isiharibike
• Huzuia damu kuganda
• Hushusha shinikizo la damu
• Hupunguza hatari ya kupatwa na mshituko wa moyo na kiharusi
• Hutuoa ahueni kwa wenye ugonjwa wa kipandauso
• Husaidia kuzuia uvumbe mwilini
• Huendesha mfumo wa kinga ya mwili
• Huzuia saratani
• Hutoa ahueni kwa wenye pumu
• Hupambana na dalili za awali za ugonjwa wa figo
• Huongeza nishati ya ubongo
KITUNGUU SAUMU (GARLIC)
• Hupambana na maambukizi
• Ina kemikali zenye uwezo wa kudhibiti saratani
• Hufanya damu kuwa nyepesi
• Hupunguza shinikizo la damu na kolestro
• Huamsha mfumo wa kinga ya mwili
• Huzuia na kutoa ahueni kwa kikohozi kilaini.
• Huweza kutumika kama dawa ya kifua
TANGAWIZI (GINGER)
• Huzuia ugonjwa wa kutetemeka
• Hufanya damu kuwa nyepesi
ZABIBU (GRAPE)
• Ina uwezo wa kufanya virusi visifanyekazi
• Huzuia meno kuoza
• Ina mchanganyiko wenye uwezo wa kuzuia saratani
PILIPILI HOHO (GREEN CHILLIES)
• Dawa nzuri ya mapafu
• Hutumika kama dawa ya kifua
• Huzuia na kuponya kikohozi kikali
• Husaidia kuyeyusha mabonge ya damu
• Hutoa maumivu
• Huweza kumfanya mtu kuwa na furaha
ASALI (HONEY)
• Huua vijidudu (bacteria)
• Huondoa wadudu kwenye vidonda na malengelenge
• Huondoa dalili za maumivu
• Hutoa ahueni kwa wagonjwa wa pumu
• Hutuliza maumivu ya vidonda vya koo
• Hutuliza mishipa ya damu, humpatia mtu usingizi
• Hutoa ahueni kwa mtu anayeharisha
MAZIWA (MILK)
• Huzuia ugonjwa wa mifupa (osteoporosis)
• Hupambana na maambukizi, hasa kuharisha
• Hurekebisha kuchafuka kwa tumbo
• Huzuia vidonda vya tumbo
• Huzuia kuoza kwa meno
• Huzuia mtu kupatwa na kikohozi
• Huongeza nishati ya ubongo
• Hushusha shinikizo la damu
• Hushusha kiwango cha kolestro mwilini
• Hudhibiti baadhi ya saratani
UYOGA (MUSHROOM)
• Hufanya damu kuwa nyepesi
• Huzuia saratani
• Hushusha kiwango cha kolestro
• Huchangamsha mfumo wa kinga ya mwili
• Hudhoofisha virusi
SHAYIRI (OATS)
• Dawa bora ya moyo
• Hushusha kolestro mwilini
• Hurekebisha sukari kwenye damu
• Ina mchanganyiko wa virutubisho unaodhibiti saratani
• Hupambana na kuvimba kwa ngozi
• Ina uwezo sawa na dawa ya kumpatia mtu choo
KITUNGUU MAJI (ONION)
• Dawa kubwa ya magonjwa ya moyo
• Huimarisha kolestro nzuri (HDL)
• Huifanya damu kuwa nyepesi
• Hushusha kiwango cha kolestro mbaya
• Huzuia damu kuganda
• Hurekebisha kiwango cha sukari kwenye damu
• Huua vijidudu
• Huzuia saratani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom