Francinho
Member
- Feb 12, 2019
- 5
- 0
INGEPENDEZA SANA UNGETOA MAELEZO JINSI YA KUUTIBU MAANA NI WENGI WANAHANGAIKA KUPATA TIBA YAKEMimi nilikuwa nao lakini nilipona. Niko safarini ntakuandikia next week. Nipe Email Address yako.
INGEPENDEZA SANA UNGETOA MAELEZO JINSI YA KUUTIBU MAANA NI WENGI WANAHANGAIKA KUPATA TIBA YAKEMimi nilikuwa nao lakini nilipona. Niko safarini ntakuandikia next week. Nipe Email Address yako.
Naomba kuelewa juu ya ugonjwa wa vitiligo, madhara yake na matibabu yake
Asante sana kwa maelezo mazuriVITILIGO NI NINI? DALILI, CHANZO NA MATIBABU.
Ugonjwa wa vitiligo, ambao pia huitwa leukoderma, husababishwa pale chembe hai zinazotengeneza melanin zinapokufa au kuacha kufanya kazi. Hilo husababisha madoa na mabaka meupe kwenye ngozi. Huathiri watu wote japo hali hii huonekana kwa haraka zaidi kwa watu weusi. Ugonjwa huo hausababishi maumivu wala hauambukizwi. Ugonjwa huu si hatari au kutishia uhai japo husababisha msongo wa mawazo na mtu kujihisi vibaya au kujiona ana upungufu.
Hata hivyo, matibabu ya ugonjwa wa vitiligo huimarisha muonekano wa ngozi kuwa mzuri japo. Ugonjwa halisi hauwezi kupona na kutoweka.
Dalili za Vitiligo
Mojawapo ni kupotea kwa rangi halisi na kuota mabaka kwenye ngozi. Tatizo huanzia kujitokeza kwenye sehemu za mwili zinazopigwa na jua zaidi kama mikono, miguu, viganja, uso na midomo hasa ‘lipsi’.
Dalili zake ni ngozi kupoteza rangi halisi, kuwa na weupe au rangi ya kijivu (gray) sehemu ya ngozi ya kichwa, kope za macho au nyusi. Kupotea kwa rangi ya ngozi ya sehemu ya ndani ya mdomo au pua. Kubadlika kwa rangi ndani ya jicho. Pia kuwa na mabaka makwapani, kitovuni na sehemu za siri.
Vitiligo huanza katika umri wowote lakini mara nyingi ugonjwa huonekana kabla ya kufika miaka 20.
Sehemu moja au chache za mwili ya vitiligo aina hii hutokea eneo moja tu la mwili. Hata hivyo, ni vigumu kujua kiwango cha kusambaa kwa hali ya kupoteza rangi ya ngozi. Wakati mwingine mabaka huweza kupona bila hata ya kutumia dawa au matibabu yoyote.
Aidha mara nyingi hali ya kupoteza rangi huendelea na husambaa maeneo zaidi ya mwili na mara chache sana ngozi hurejea katika hali ya awali.
Chanzo
Ugonjwa wa vitiligo hutokea pale chembe hai zinazozalisha melanin zinapokufa au kuacha kufanya kazi. Melanini huipa ngozi, nywele na macho rangi yake ya asili. Madaktari hawajaweza kufahamu sababu ya kufa au kushindwa kufanya kazi kwa chembe hai hizi lakini hali hii huweza kuhusishwa na mfumo wa kinga ya mwili kushambulia na kuharibu kimakosa chembe hai hizi ambazo huzalisha melanin.
Matatizo ya vitiligo
Watu wenye ugonjwa huu huwa katika hatari kubwa ya kushambuliwa na matatatizo ya kisaikolojia na msongo wa mawazo.
Huhisi kuungua zaidi na jua pamoja na saratani ya ngozi. Wana matatizio ya macho. Kadhalika kushindwa kusikia kikamilifu.
Pia hupata madhara yaletwayo na utumiaji wa madawa ya kutibu ugonjwa huu kama kukauka sana kwa ngozi pamoja na muwasho.
Matibabu
Yapo matibabu ya aina nyingi na ambayo husaidia katika kurejesha rangi ya awali ya pamoja na ubora wa ngozi japo matokeo ya matibabu hayo hutofautiana na ni vigumu kutabiri ufanisi. Badhi ya matibabu huweza kuwa na madhara makubwa kwa hiyo daktari wako huanza kwa kukushauri utumie dawa nyepesi za kujaribu kuboresha muonekano wa ngozi kama ‘make-up’.
Iwapo mgonjwa na daktari watakubaliana kuanza matibabu makubwa ya madawa basi uponyaji huweza kutumia miezi kadhaa kuonekana na wakati mwingine kutumia aiana nyingi za matibabu.
CRYSTAL CELL NA TRIPLE 3-MIRACLE INTENSE ESSENCE ni dawa zinazoweza kusaidia kuzuia vitiligo kuendelea kutokea yaani kupoteza kwa chembe zinazosababisha rangi halisi ya ngozi. Pia, huweza kuboresha muonekano wa ngozi ukawa mzuri.
kwa mawasiliano zaidi ya whatapp 0682315816
Mgonjwa anapaswa kumwona daktari mara tu unapoona hali ya kupoteza rangi ya ngozi, nywele au macho. Ugonjwa wa vitiligo hauna tiba ila ukiwahi husaidia kuzuia au kupunguza hali ya ngozi kuharibiwa.
Sotty ndugu Naomba unisaidie ninasumbuliwa na tatizo la ugonjwa wa vitiNi-pm nikupe namba ya rafiki yangu mmoja alikuwa na ugonjwa huu lakini akapata nafuu.
Ugonjwa wa vitiligo huu mwaka wa tatu sasaSotty ndugu Naomba unisaidie ninasumbuliwa na tatizo la ugonjwa wa viti
Naomba unisaidie kuhusu ugonjwa wa vitiligo namba yangu 0678213083Mimi nilikuwa nao lakini nilipona. Niko safarini ntakuandikia next week. Nipe Email Address yako.
Aiseee si una bando? Kwanini usijielimishe kwa Google?Samahani Mkuu, nisaidie kuujua huu ungonjwa, ni ugonjwa gani naamnisha unakuwa na tatizo gani?
Je husababishwa na Nini mkuu?nijuavyo mimi vitiligo haitibiki,cha msingi ni kujikubali!