OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,238
- 103,907
Hello mwanaJF kila ninapopata nafasi nitakujuza mambo ya hovyo ambayo hufanyika serikalini na wengi wetu hatufahamu. Wengi tunafahamu zaidi kuhusu matokeo na sio chanzo.
Wengi wetu hudhani kwamba watumishi wa serikali ni watu makini sana na hufanya majukumu yao kwa ustadi na weledi. Acha kujidanganya. Huko serikali watu hao hawapo.
Je, unafahamu kwamba wengi wa wafanya maamuzi serikali huwa hawana muda wa kusoma nyaraka na makablasha, kuchambua na kuamua? Subiri nikueleze.
Hii inahusisha ngazi karibia zote, kuanzia vikao vya serikali za vijiji mpaka wizarani na idara zingine za serikali ikiwemo bunge la jamhuri.
Wafanya maamuzi hawa huwa wanakuta nyaraka na makabrasha hayo kwenye ukumbi wa kikao siku ya kufanya maamuzi. Tarehe ya kikao inaweza kutangazwa wiki moja kabla ya kikao lakini sio kwamba waheshimiwa watapatiwa nyaraka hizo ili wapate wasaa wa kuzichambua ili awe kwenye nafasi nzuri ya kuhoji na kushauri HAPANA. Bali ataenda kupitia na kuchambua humohumo ukumbini.
Hili hufanyika pia bungeni kuanzia kwenye vikao vya kamati mpaka vile mubashara. Wanasomea mule mule ukumbini na hivyo kujikuta wanahitaji zaidi msaada wa waandaaji ili kuzielewa hizo nyaraka.
Wafanya maamuzi hawa hujikuta wana uelewa mdogo sana juu ya jambo wanalohitaji kulipitisha. Na hivyo kujikuta wanapitisha kama ilivyokuja.
Hii ndio sababu hasa ya sheria za hovyo kupitishwa kwa sababu watunga sheria hawana muda wa kuchambua miswada.
Nazungumzia kinachofanyika. Lakini kinachotakiwa kufanyika kwa mujibu wa taratibu ni tofauti. Taratibu zinaelekeza nyaraka kusambazwa kwa wakati ili mtoa maamuzi apate muda wa kutosha kuchambua.
Ndio maana wabunge wachache wanaopata muda wa kusoma na kuchambua huonekana vipanga. Ni kwa sababu 90% ni vilaza huku baadhi wakijua tu kusoma na kuandika.
Huku serikali za Halmashauri hali ni mbaya zaidi. Waheshimiwa madiwani hata ajenda tu za kikao huwa wanazikuta ukumbini. Kila kilichomo wanapitisha kama kilivyokuja. Mpaka itokee shida ikajulikana baada ya kuleta athari ndio wanakuwa wakali na kuhoji.
Hitimisho
Kusubiri nchi ya maziwa na asali kwa serikali hii na watu wake ni kupoteza muda. Usitegemee mipango na mikakati mizito kuhusu kilimo, ufugaji, madini na rasilimali zingine kwa wafanya maamuzi wa namna hii.
Wengi wetu hudhani kwamba watumishi wa serikali ni watu makini sana na hufanya majukumu yao kwa ustadi na weledi. Acha kujidanganya. Huko serikali watu hao hawapo.
Je, unafahamu kwamba wengi wa wafanya maamuzi serikali huwa hawana muda wa kusoma nyaraka na makablasha, kuchambua na kuamua? Subiri nikueleze.
Hii inahusisha ngazi karibia zote, kuanzia vikao vya serikali za vijiji mpaka wizarani na idara zingine za serikali ikiwemo bunge la jamhuri.
Wafanya maamuzi hawa huwa wanakuta nyaraka na makabrasha hayo kwenye ukumbi wa kikao siku ya kufanya maamuzi. Tarehe ya kikao inaweza kutangazwa wiki moja kabla ya kikao lakini sio kwamba waheshimiwa watapatiwa nyaraka hizo ili wapate wasaa wa kuzichambua ili awe kwenye nafasi nzuri ya kuhoji na kushauri HAPANA. Bali ataenda kupitia na kuchambua humohumo ukumbini.
Hili hufanyika pia bungeni kuanzia kwenye vikao vya kamati mpaka vile mubashara. Wanasomea mule mule ukumbini na hivyo kujikuta wanahitaji zaidi msaada wa waandaaji ili kuzielewa hizo nyaraka.
Wafanya maamuzi hawa hujikuta wana uelewa mdogo sana juu ya jambo wanalohitaji kulipitisha. Na hivyo kujikuta wanapitisha kama ilivyokuja.
Hii ndio sababu hasa ya sheria za hovyo kupitishwa kwa sababu watunga sheria hawana muda wa kuchambua miswada.
Nazungumzia kinachofanyika. Lakini kinachotakiwa kufanyika kwa mujibu wa taratibu ni tofauti. Taratibu zinaelekeza nyaraka kusambazwa kwa wakati ili mtoa maamuzi apate muda wa kutosha kuchambua.
Ndio maana wabunge wachache wanaopata muda wa kusoma na kuchambua huonekana vipanga. Ni kwa sababu 90% ni vilaza huku baadhi wakijua tu kusoma na kuandika.
Huku serikali za Halmashauri hali ni mbaya zaidi. Waheshimiwa madiwani hata ajenda tu za kikao huwa wanazikuta ukumbini. Kila kilichomo wanapitisha kama kilivyokuja. Mpaka itokee shida ikajulikana baada ya kuleta athari ndio wanakuwa wakali na kuhoji.
Hitimisho
Kusubiri nchi ya maziwa na asali kwa serikali hii na watu wake ni kupoteza muda. Usitegemee mipango na mikakati mizito kuhusu kilimo, ufugaji, madini na rasilimali zingine kwa wafanya maamuzi wa namna hii.