Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,036
- 20,338
TANZANIA :- FAHAMU UJENZI WA SGR UNAVYOENDELEA
Ujenzi wa Reli ya Kati kwa Kiwango cha Kimataifa (Standard Gauge Railway) ambapo ujenzi wa kipande cha Dar es Salaam - Morogoro (km 300) umefikia asilimia 90.34 na kipande cha Morogoro - Makutupora (km 422) asilimia 57.57.
Aidha, tayari Serikali imesaini mkataba wa ujenzi wa kipande cha Mwanza - Isaka (km 341) wenye thamani ya shilingi trilioni 3.07; na kuendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa vipande vya Makutupora - Tabora (km 294) na Tabora - Isaka (km 133) na hapo baadaye kujenga njia ya Tabora - Kaliua - Kigoma (km 411) na Kaliua - Mpanda (km 207).
Katika kipindi cha Julai 2020 hadi Machi 2021 jumla ya shilingi bilioni 596.8 zimetumika katika utekelezaji wa mradi huu alisema Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
Ujenzi wa Reli ya Kati kwa Kiwango cha Kimataifa (Standard Gauge Railway) ambapo ujenzi wa kipande cha Dar es Salaam - Morogoro (km 300) umefikia asilimia 90.34 na kipande cha Morogoro - Makutupora (km 422) asilimia 57.57.
Aidha, tayari Serikali imesaini mkataba wa ujenzi wa kipande cha Mwanza - Isaka (km 341) wenye thamani ya shilingi trilioni 3.07; na kuendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa vipande vya Makutupora - Tabora (km 294) na Tabora - Isaka (km 133) na hapo baadaye kujenga njia ya Tabora - Kaliua - Kigoma (km 411) na Kaliua - Mpanda (km 207).
Katika kipindi cha Julai 2020 hadi Machi 2021 jumla ya shilingi bilioni 596.8 zimetumika katika utekelezaji wa mradi huu alisema Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa