beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
HOMA YA MGUNDA NI NINI?
Ni Ugonjwa ambao huambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu. Homa ya Mgunda 'Leptospirosis' husababishwa na Bakteria aina ya 'Leptospira interrogans'
Dalili za HomaYaMgunda ni pamoja na Homa, Maumivu ya Kichwa na Misuli, Uchovu, Mwili kuwa na rangi ya njano, macho kuvilia damu, kutokwa damu puani na kukohoa damu
Maambukizi ya binadamu kwa binadamu ni nadra kutokea
BINADAMU ANAPATAJE MAAMBUKIZI?
Maambukizi kutoka kwa Wanyama hadi Binadamu yanaweza hutokea kwa;
Kugusa mkojo/maji maji mengine ya mwili kutoka kwa wanyama walioambukizwa
Kugusa Maji, Udongo au Chakula kilichochafuliwa na mkojo wa Wanyama
Kunywa Maji yaliyochafuliwa na Bakteria wa #HomaYaMgunda
Pia, Bakteria wanaweza kuingia mwilini kupitia ngozi yenye mikwaruzo, macho, pua au mdomo
Ni Ugonjwa ambao huambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu. Homa ya Mgunda 'Leptospirosis' husababishwa na Bakteria aina ya 'Leptospira interrogans'
Dalili za HomaYaMgunda ni pamoja na Homa, Maumivu ya Kichwa na Misuli, Uchovu, Mwili kuwa na rangi ya njano, macho kuvilia damu, kutokwa damu puani na kukohoa damu
Maambukizi ya binadamu kwa binadamu ni nadra kutokea
BINADAMU ANAPATAJE MAAMBUKIZI?
Maambukizi kutoka kwa Wanyama hadi Binadamu yanaweza hutokea kwa;
Kugusa mkojo/maji maji mengine ya mwili kutoka kwa wanyama walioambukizwa
Kugusa Maji, Udongo au Chakula kilichochafuliwa na mkojo wa Wanyama
Kunywa Maji yaliyochafuliwa na Bakteria wa #HomaYaMgunda
Pia, Bakteria wanaweza kuingia mwilini kupitia ngozi yenye mikwaruzo, macho, pua au mdomo