Nimejaribu kutafuta sheria inasema nini kuhusu wafanyakazi wa kigeni wanao kuja nchini na kushika ajira ambazo ni haki ya vijana wa kitanzania,wana JF sheria inasema nini?
kulingana na uelewa wangu wafanyakazi wa kigeni hawakatazwi kisheria kushika nafasi ya vijana wa kitanzania kazini kulingana na mikataba ya jumuiya mbalimbali za kimataifa.
kila mtu anahaki ya kufanya kazi yoyote na popote ilimradi ammefuata sheria, so hata wageni wanahaki ya kuajiriwa. hata hivyo sheria mbalimbali zimeweka utaratibu wa idadi ya watumishiwa kigeni hasa katika sekta binafsi. Si kosa kwa mgeni kutoka nje na kufanya kazi katika nchi hii, kumbuka kuna watanzana wengi walioajiriwa nje ya nchi sasa na wao wafukuzwe huko, .....acha ubaaguzi....., maeneo mengine ni lazima tuweke wageni kutokana na upungufu wa wataalam wa kada husika.
so shida sio kuajiri wageni bali wewe kama mtanzania unatakiwa kuhakikisha kuwa una uwezo wa kutosha ili uweke ushindani katika soko la ajira. tatizo la watanzania they are not marketable degree graduate anazidiwa na mtu wa certificate sasa nani atakuajiri....
lakini hivi hata store keepers lazima wawe ma expert? sales & marketing lazima awe expert? nafikiri si sawa,kuna maeneo tunahitaji experts lakini kama vile serikali imewafumbia macho sana hawa wageni,kuna mahali nimeenda nimekuta mtu wa IT ni expert,binafsi mimi naona hii sio fear play
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.