Exclusive interview with Mohammed Dewji

Muulize kwanini anaajiri ma Expert uchwara kutoka India wakati vijana wa kitanzania wapo mitaani hawana ajira?
 
Dada yangu Fina Big up ila una kazi ya kuchambua maswali!
Swali langu moja tuu:yeye kama mbunge ambaye anatakiwa kutetea maslai ya wananchi,amechukua hatua gani baada ya METL kuhusishwa na usambazaji mbolea feki mpaka kupigwa BAN na wizara.
Pia mpe hongera kwa biashara zake ila mwambie kulipa kodi ni muhimu ili nae awemo kwenye top ten ya large tax payers
 
muulize makampuni yake yamekuwa kwa kiasi kikubwa yakijihusisha na usafirishaji wa mazao ghafi kwenda india hasa ufuta,korosho na mengineyo kwanini asijenge viwanda vya ubanguaji au uzalishaji mafuta ya ufuta ili asaidie ajira kwa tanzania(niambiwa alinunua kiwanda cha korosho ila kimegeuzwa ghala)
Pamoja na kununua kiwanda cha nguo cha Mutex wakulima wa pamba anawalipa sawa na soko la dunia maana nasikia wamegoma kutokana na kulipwa pesa kidogo ya pamba
 
Kwanini alishindwa kuendesha television yake ya CEN huoni tuzo aliyopata hastahili kwa kushindwa kuendesha chombo kama hicho
 
Hata mimi nataka nisikilize,kuna online link ya hiyo show?Pia ni program inayorushwa kwa muda gani?na ni maswali mangapi yanategemewa kuulizwa?ama does it depend on time?

Pi kumbukumbu zangu zinaonyesha kwamba alitajwa kwenye kitabu kinachoenda kwa tittle ya "t-shirt" (simkumbuki author),ambacho kilieleze hiyo issue ya kampuni ya Mohamed Enterprises na kuhusika kwake kuwa importer mkuu wa nguo za mitumba.

Nakumbuka pia kampuni yake ndo ya kwanza kuanzisha hiyo biashara,ambapo kiukweli hizo nguo ni za misaada,kitabu hicho kinaelezea jinsi ambavyo biashara hiyo imeucost uchumi wetu.

Nadhani miaka ya nyuma nilishawahi kuuliza hili swali humu ndani.Je anaweza kusema kiukweli ana mapenzi na Taifa la Tanzania na watu wake?
 
Mkuu zomba hili swali nimelielekeza kwa Mohammed Dewji inawezekana hizo sababu zipo lakini si kwa waTanzania wote nadhani hata wewe utakubaliana na mimi.

Nafarijika Mohammed Shossi amekupa like kubwa lakini kasahau juzi alikuja na bandiko lake kwamba wakati wa zoezi la kitambulisho cha uraia alinyanyaswa kwasababu ya rangi yake leo anafurahia waTanzania weusi wanavyonyayaswa na Mohammed Dewji wametengewa vyoo vichafuu, michango yao ya NSSF haipelekwi, mishahara ya waTanzania weusi ni chini sana huku wahindi wenzao wahindi wakilipwa mishahara mara tano hadi kumi zaidi.

Yafaa Mohammed Dewji anapowaomba kura wananchi wa Singida awaambie ajira zake ni za kibaguzi na ataoa sababu hizi hizi alizotoa Zomba.

Mkuu Ngongo much respect,

Sijaunga mkono kwa watanzania kudhalilishwa kama unavyosema kwenye bolds za red. Point ya zomba ilikuwa utendaji wa kazi wa sisi watanzania nikiwemo mimi! na nimemjibu kumwambia sisi watanzania hata wenye asili za asia tuna kasumba za uswahili uswahili sio wachapa kazi! wengi wetu tukifika kazini tutaenda kunywa chai kwanza tukirudi tutashughulika na mambo yetu binafsi kama facebook na jf kisha muda mfupi tunamhudumia mwajiri halafu tunaenda lunch!

Usidhani kuwa muhindi mzaliwa wa Tanzania anapewa haki sawa kwenye kampuni ya wahindi kama anavyopewa muhindi kutoka gujrat! Muhindi wa kibongo analipwa sawa na hamisi halafu hamisi na muhindi wa bongo watamfundisha muhindi wa gujrati kazi na atakunja dola 2000, gari, nyumba. matibabu na ada ya watoto wake indian school!

Tukirudi kwenye suala la uraia nililalamika sio kwa kubaguliwa! lah hasha nililalamika zaidi ya hilo kama ulipata kuangalia ITV jumatatu iliyopita nilitoka kwenye habari na nilielezea vizuri sana.

Uraia ni kitu muhimu sana kwenye ustawi wa nchi yoyote duniani ikiwa uraia unatolewa kwa kuangalia rangi ya mtu bila kujali historia ya vizazi vyake basi taifa linaweza kukuta linagawa uraia kwa watu wenye uwiano sawa na raia wenye haki ya kuupata uraia.

Nilipenedkeza kusiwe na double standard kuwe na mfumo kama tunapoenda vyuoni requeremnts huwa hazibagui rangi unatakiwa uende na cheti cha kuzaliwa kudhibitisha kuwa umezaliwa JMT na cheti chako cha kuhitimu sekondari uwe mweusi au wa kijani lazima uwe na vitu vyote hivyo!

Ila kwenye urai ukiwa mweusi utambulisho wa mjumbe/mwny kiti wa serikali ya mtaa unatosha! Kuna wengine kwenye kituo changu waliandikishwa kwa cheti cha ndoa! kisa? ni weusi!


 


waTanzania weusi wanavyonyayaswa na Mohammed Dewji wametengewa vyoo vichafuu, michango yao ya NSSF haipelekwi, mishahara ya waTanzania weusi ni chini sana
Sasa Mkuu Ngongo labda nikuulize swali,
Wametengewa vyoo vichafu kivipi? ... Kwanini wasivisafishe? Tukubali au tusikubali usafi wa vyoo vya jumuia nchini mwetu ni wa hali ya chini sana, hata sehemu ambazo zina maji.
Michango ya NSSF haipelekwi? Yaani umenikata hela za NSSF halafu??? Peleka pay stub mahakamani.
 
Mkuu Kobello asante sana kwa swali zurio nina hakika hukunielewa.

Ofisi za MeL kuna vyoo kwaajili ya waafrika na vyoo kwaajili ya wahindi. Vyoo kwaajili ya waAfrika havifanyiwi usafi wa kutosha, haviwekwi dawa, havina toilet papers,na wakati mwingine havina maji.Vyoo vya wahindi vina maji kila wakati vinafanyiwa usafi kila mara, vifaa vikiharibika vinabadilishwa mara moja.

Wafanyakazi wazawa [waTanzania] hawakatwi NSSF wala mwajiri hachangii NSSF wengi wao wanaonekana kama vibarua tu tofauti na wahindi na waPakistan ambao wanalipwa mishahara mikubwa na michango yao inapelekwa NSSF kama sheria inavyotaka.


Sasa Mkuu Ngongo labda nikuulize swali,
Wametengewa vyoo vichafu kivipi? ... Kwanini wasivisafishe? Tukubali au tusikubali usafi wa vyoo vya jumuia nchini mwetu ni wa hali ya chini sana, hata sehemu ambazo zina maji.
Michango ya NSSF haipelekwi? Yaani umenikata hela za NSSF halafu??? Peleka pay stub mahakamani.
 
Hili namjibia:

Kwa sababu:

Wafanya kazi wa Kitanzania wengi ni wavivu, wezi, waongo, hawaishi kufiwa na kuomba ruksa za kwenda kuzika, hawaishi kuumwa, hawaishi kuwa na kila sababu za kutokuhudhuria kazini. Watu wa India wanajuwa dhiki ya maisha na vipi kupata kazi ni kugumu na wao huchapa kazi na hawana visingizio kama Watanzania.

Inapaswa Watanzania wanaotaka maendeleo ya haraka wabadilike.

Oops, nilisahau:

Hawaishi kukopa (kujichotea) makazini, hata iwe ni viongozi wa vyama vya siasa.

Mkuu, umeweka chumvi nyingi sana. NINA WASIWASI KAMA WEWE NI RAIA WA TANZANIA, LAZIMA UTAKUWA MHAMIAJI, TENA HARAMU AU UNA ROHO MBAYA. Hayo yapo kwa sababu sisi ni watanzania na tunaishi hapa na ndugu zetu. huwezi ukaacha kujumuika na jamii yako inapofikwa na misiba. mbona hata hao maboss wanapo pata misiba ya ndugu zao huko kwao nje huwa wanasafiri kwenda kujumuika na ndugu zao??? BEFORE WEALTH, THERE IS HUMANITY. cha msingi, ni kuweka utaratibu wa matukio gani hasa mfanyakazi apewe ruhusa ya kutohudhuria kazini, WATANZANIA NI WAELEWA NA WANA UBINADAMU SANA.
 
dada fina maswali karibu yote niliyopanga kuuliza yameshaulizwa na wadau kwa hiyo leo nitasikiliza kwa makini majibu, but kuna swali moja limeulizwa humu IWAPO MH HUYU ANAPOKEA POSHO BUNGENI ( ile ambayo mh zitto huwa hapokei) ,nakuomba hata kama muda hautatosha kutokana na maswali mengi ,jitahidi umuulize ,pia atoe comment zake iwapo this is fair kupokea.
NYONGEZA(kwako): last week ulikuwa na wageni wawili zzk na masha, kulikoni week hii atakuwa ni huyu huyu mmoja.
 
dada fina nakuamini sana kwa kuuliza maswali magumu bia woga,nakuomba muulize na haya
1: je kwa kumbukumbu za katika biashara zake amewahi kupata ajali za moto mara ngapi?
maana kumekuwa na mfulilizo ajali za moto katika maghala yake ya kuhifadhia bidhaa hali ambayo imekuwa ikihusishwa na "JANJA" yake kuyachoma makusudi kwa ajili ya kukwepa kodi na kujipatia faida kubwa kutoka bima,hali inayosababisha kufilisi mashirika ya bima.
2: nini maoni yake kuhusu sheria kandamizi ya kufungia vyombo vya habari vinavyokosoa serikali hasa gazeti la mwanahalisi?
3:nini maoni yake kuhusu kauli ya mh pinda ya ' LIWALO NA LIWE' katika kutatua mgomo wa madaktari?
 
Mkuu, umeweka chumvi nyingi sana. NINA WASIWASI KAMA WEWE NI RAIA WA TANZANIA, LAZIMA UTAKUWA MHAMIAJI, TENA HARAMU AU UNA ROHO MBAYA. Hayo yapo kwa sababu sisi ni watanzania na tunaishi hapa na ndugu zetu. huwezi ukaacha kujumuika na jamii yako inapofikwa na misiba. mbona hata hao maboss wanapo pata misiba ya ndugu zao huko kwao nje huwa wanasafiri kwenda kujumuika na ndugu zao??? BEFORE WEALTH, THERE IS HUMANITY. cha msingi, ni kuweka utaratibu wa matukio gani hasa mfanyakazi apewe ruhusa ya kutohudhuria kazini, WATANZANIA NI WAELEWA NA WANA UBINADAMU SANA.

Na waa jirani? na wa Mjombake shemeji yako, na wa mpwa wa ndugu yako mliyesomea nae (sio wa kuzaiwa).

Mimi si Mtanzania kwa kuzaliwa, mimi ni Mtanganyika, si kwa kukisia wala si wa kuhamia kama baba'ke Nyerere, naweza kuhesabu generations 8 za nyuma na walikozaliwa, zote ndani ya Tanganyika. Wewe unaweza ngapi?

Usisikie ni Mchagga basi ukajuwa wote hao ni Watanganyika, wapo kina "mrema" huko.
 
Katika kipindi cha Makutano Jumamosi ijayo mgeni atakaeongea na Fina Mango ni mbunge wa Singida Mjini Mheshimiwa Mohammed Dewji atakaeongea masuala mbalimbali ikiwepo maisha yake binafsi, ya kisiasa na kibiashara.

Kama una swali lolote ambalo ungependa Mheshimiwa Dewji alijibu tafadhali uliza na litasomwa hewani siku ya kipindi kuanzia saa tisa mchana kupitia 92.9FM Dar, 93.3FM Dodoma, 98.6FM Arusha/Moshi, 101.7FM Dodoma.

Karibu

Siku zingine ukiandika utaje na tarehe, Jumamosi "ijayo" pekee haitoshi.
 
Ile ya wiki iliyopita ya Mo Dewji mlifanikiwa?sijaona follow up kama ilivyokuwa ile ya Zitto.
 
Alijibu maswali yote ikiwa ni pamoja kutolea ufafanuzi kiwanja kilichokua na mgogoro

Alijibu maswali yote kabisa?najua ile ya Zitto kulikuwepo na follow up thread yenye link ya mahojiano hayo.Je unaposema maswali yote,una maana maswali yote uliyoyachagua ama ni maswali yote yaliyoulizwa na members humu kwenye ile thread?je kuna uwezekano wa sisi ambao hatukupata nafasi/uwezo kusikiliza kuyapata maswali hayo endapo uliyachagua?

Hili ni bandiko langu la mwisho lenye maswali yenye kuhusiana na mahojiano yaliyopita endapo utanijibu haya.Hili litasaidia kupisha wenye maswali kuhusiana na wageni wako watarajiwa.

Natanguliza shukran...
 
Alijibu maswali yote ikiwa ni pamoja kutolea ufafanuzi kiwanja kilichokua na mgogoro

Iko wapi link ya hiyo show ya Mo Dewji?

nilitaka nimuulize kuhusu mgogoro wa pesa kati yake na serikali ya Libya na Foreign Tanzania

anyway naomba link ya show zilizopita nisikilize kama podcast au video...
 
Alijibu maswali yote kabisa?najua ile ya Zitto kulikuwepo na follow up thread yenye link ya mahojiano hayo.Je unaposema maswali yote,una maana maswali yote uliyoyachagua ama ni maswali yote yaliyoulizwa na members humu kwenye ile thread?je kuna uwezekano wa sisi ambao hatukupata nafasi/uwezo kusikiliza kuyapata maswali hayo endapo uliyachagua?

Hili ni bandiko langu la mwisho lenye maswali yenye kuhusiana na mahojiano yaliyopita endapo utanijibu haya.Hili litasaidia kupisha wenye maswali kuhusiana na wageni wako watarajiwa.

Natanguliza shukran...

Tuliiwea labda hukuona, kwa fida ya wengine hii hapa link ya mahojiano yote

 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom