Exclusive interview with Mohammed Dewji

Mh. Dewji...maswali ni haya yafuatayo:

1. We umezaliwa kwenye familia yenye nafuu na umiliki wa mali,lakini kwanini uliamua kugombea ubunge? Kwani bila ubunge ungeshindwa kutoa misaada?

2. Je ni kweli upo kambi ya Lowassa ambayo ni maandalizi ya mbio za urais 2015?

3. Kwanini huwa hutoi michango sana bungeni na Mara nyingi nimekuona ukipiga tu meza?
 
Mh. Dewji!

Kutokana na kashfa ya mkopo wa mafuta kutoka Libya kampuni yako ilitaka kuingilia na hatimae kunufaika na dola za marekani 121.9 Millioni sawa na TSH 180 Billioni. Ilikuwaje mjasiliamali mmoja (ambaye ni wewe) kuingia katika Transactions baina ya nchi mbili? Na baada ya ubalozi wa Libya Tanzania kukana makubaliano yoyote kati ya MeTL na serikali yao ulichukua hatua gani?

Kama hukuchukua hatua basi ile dhana ya kuliibia Taifa kwa mtindo wa EPA umekua kinara kupitia Massoud Mohamed Nassr ambae pia anahusika na MeTL.


Msingi wa swali:

dewji246.jpg


UBALOZI wa Libya jijini Dar es Salaam umekana mahusiano yoyote na kampuni ya Mohammed Enterprises (MeTL) na mshirika wao Massoud Mohamed Nassr.

Hatua hii inaziba mwanya wa kampuni hiyo kujipatia sehemu ya dola 121.9 milioni (sawa na kiasi cha Sh. 180 bilioni) ambazo inadaiwa ni deni la Tanzania kwa Libya linalotokana na mkopo wa mafuta.

Fedha hizo zilitarajiwa kuchotwa kwa mtindo wa EPA wa kununua madeni yaliyoshindikana kutoka benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Tayari ubalozi umeiarifu serikali kuhusu suala hilo na nakala ya barua yake kupelekwa mahakama kuu ambako mashauri mawili yamefunguliwa na MeTL.

Taarifa kutoka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali jijini Dar es Salaam zimeeleza kuwa hata ofisi hiyo tayari imetaarifiwa kuhusu suala hilo.

Nyaraka ambazo MwanaHALISI limepata zinaonyesha kuwa mfanyabiashara maarufu wa chakula nchini, Gulamabbas Hassanali Fazal Dewji anataka kujipatia mabilioni ya shilingi kutokana na kile kilichoitwa kuuziana madeni sugu kati ya serikali za Tanzania na Libya.

Vyanzo madhubuti vya habari vimelieleza gazeti hili kuwa serikali imezuia malipo ya mabilioni ya shilingi ambazo mfanyabiashara huyo amekuwa akijitahidi kuyadai kupitia kesi mbili alizofungua katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Dewji ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya Mohammed Enterprises (T) Limited (MeTL), anadai zaidi ya dola 20 milioni kupitia kesi Na. 127 ya 2009 na kesi Na. 110 ya 2010.

Wakati kesi Na. 127 ambayo MeTL ilimshitaki raia wa Libya aitwaye Massoud Mohamed Nassr au Masoud M. Nasser, iliamuliwa 26 Mei 2011, kesi Na. 110 haijasikilizwa.

Katika uamuzi wa kesi ya awali inayodaiwa kuhusu mkataba wa kuuziana deni, Jaji Augustine Mwarija aliamuru pande husika zigawane mapato pamoja na riba yaliyotokana na uuzaji wa dhamana za serikali zinazoshikiliwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Mapato hayo yanafikia Sh. 6,640,550,960 ambapo uamuzi wa Jaji Mwarija unaelekeza kuwa MeTL itaingiziwa kwenye akaunti yake Sh. 3,320,275,480.

Lakini, kulingana na nyaraka zilizopatikana, hata mapato hayo si halali na serikali imezuia malipo.

Serikali ya Libya, ambayo MeTL imeishitaki kama mdaiwa wa kwanza katika kesi Na. 110, imekataa kutambua mpango wa kuuziana deni la dola 121,900,000 ambalo linadaiwa kutokana na Tanzania kushindwa kulipa mkopo tangu mwaka 1983.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ameiambia MwanaHALISI kwamba wizara yake haitambui makubaliano ya MeTL na Nasser na haioni uhalali wa madai yao.

Membe ambaye alizungumza na gazeti hili ofisini kwake Dar es Salaam juzi Jumatatu, alisema wizara yake tayari imemjulisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa serikali ya kigeni haiwezi kushitakiwa na Mtanzania kwa mikataba ambayo haikuidhinishwa.

“Serikali ya nje haiwezi kushitakiwa bila ya kuwa na nyaraka za serikali zilizosainiwa na watu wenye kutambuliwa katika mikataba. Huyu hajalipa fedha na hana mkataba… (kama ni) deni lazima linunuliwe na serikali na kuna masharti ya kulipa,” alisema.

Akigusia maelezo yaliyotolewa na ubalozi wa Libya nchini, waziri Membe alisema ni maelezo sahihi na kwamba msimamo wa serikali ni kutokuwepo sababu yoyote wala uhalali wa kuishitaki serikali ya Libya katika suala hilo.

Alisema Mlibya anayedaiwa kufunga mikataba ya kuuziana deni na MeTL linalohusu mafuta ambayo serikali ya Libya iliiuzia Tanzania, hakuwa na hata sasa hana mamlaka ya kuiwakilisha serikali ya Libya katika jambo lolote na “hakuwa na mkataba wowote kati ya serikali ya Libya na MeTL.”

MeTL imeishitaki Libya kama mdaiwa wa kwanza katika kesi Na. 110. Ubalozi wa Libya unasema hautambui mpango wa kuuziana deni la dola 121,900,000 uliobuniwa na MeTL kutokana na Tanzania kushindwa kulipa deni lake linalotokana na Libya kuiuzia serikali ya Tanzania mafuta kwa mkopo.

Ubalozi wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Watu wa Libya jijini Dar es Salaam, imeeleza kwamba haitambui makubaliano ya aina yoyote kati ya serikali ya Libya na MeTL au anayejiita mwakilishi wa serikali ya Libya.

Akijibu takwa la kuitwa shaurini mahakama kuu, ofisa wa ubalozi wa Libya anaeleza waziri wa mambo ya nchi za nje Tanzania kuwa serikali yake haijawahi kuipeleka Tanzania mahakamani.

Katika hati yake ya maelezo yenye Kumb. N/REF 7/2/2250 ya tarehe 20 Mei 2011, ambayo nakala yake ilipepekwa mahakamani, ubalozi wa Libya unasema, katika mahusiano yake ya nje ya nchi – yawe ya kisiasa au kiuchumi – huwa inashughulika na serikali wala si mtu au taasisi binafsi hasa suala lenyewe linapohusu deni kwa biashara ya mafuta.

“Libya, katika suala hili (la kuuza mafuta), inazingatia muktadha wa udugu na Tanzania, unaotokana na uhusiano mzuri wa kisiasa tulionao. Tunaamini Libya haistahili kushitakiwa na kampuni hii kutokana na suala hili,” inasema hati hiyo.

Serikali ya Libya, unaeleza ubalozi wake, haijapata kusaini au kuidhinisha mkataba wowote wa kibiashara na kampuni inayodai katika kesi tajwa.

Inasema, “Ni muhimu ukafahamu kuwa mamlaka inayostahili kuiwakilisha serikali ya Libya katika Tanzania ni ubalozi wa Libya na si yeyote mwingine; iwe kwa kusaini mikataba au kuiidhinisha pale inapotokea…”

“Ubalozi wa Libya unaiomba mahakama tukufu kutoendekeza madai haya dhidi ya Libya. Tuna matumaini makubwa ya busara na hekima kutumika katika kutenda haki kuhusu kesi hii,” ameeleza wakala wa serikali ya Libya.

Maelezo ya serikali ya Libya yaliwasilishwa kwa Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania kwa barua ya wizara ya mambo ya nje tarehe 30 Mei 2011 yenye Kumb. Na. GA 226/336/78 iliyosainiwa na Abdallah M. Mtibora kwa niaba ya katibu mkuu wa wizara hiyo.
 
Nina maswali kadhaa kuelekea uendeshaji wa kampuni za Mohamed Dewji:

1..Je,anajua kwamba kwenye pale Head Office-Morogoro Road kuna kuna vyoo vya aina mbili,kuna kimoja kichafu kipo ground floor ambacho wanatumia watu weusi na vingine visafi ambavyo vinatumiwa na wahindi? Hata funguo kuna mbili ile ya wahindi hauwezi kupata mtanzania.Ubaguzi uliokithiri,Je amehalalisha 'Apatheid Policy' kwenye makampuni yake?

2..Je anajua kwamba baadhi ya kampuni zake zinakwepa kwa makusudi kuwalipia wafanyakazi wake ule mchango wa mifuko ya kijamii kama NSSF?

3..Je,anajua kwamba wafanyakazi hasa watanzania wanalipwa mishahara kupitia payment vouchers na pia mshahara karibia nusu unaandikwa kuwa allowance hewa ili kukwepa kuchangia kiasi stahili kwa wafanyakazi wake kwenye mifuko ya kijamii?

4..Je,ana mpango gani na yale mashamba makubwa(Mfano...Alavi sisal estate la Kibaha approx. 6000Ha) ambayo hayafanyii lolote na wala hawekezi kitu badala yake ananyonya kilichopo tu na kushindwa kabisa kuyaendeleza?Mikopo aliyochukua kwenye mabenki kwa kutumia yale mashamba amepeleka wapi?

5..Mheshimiwa Mohamed Dewji anajiita mtanzania mwenzetu lakini kwa nini amejaza wahindi huku akiwalipa mishahara hadi mara tatu ya ile wanayolipwa watanzania katika ngazi zile zile za kiutendaji?

6..Je, anajua kwamba wafanyakazi watanzania wananyimwa likizo kwa wakati kwa kuzungushwa saaaana wakati wahindi wanapewa ruhusu za kwenda likizo zilizogharamiwa na kampuni?

Naomba atoe majibu yenye kueleweka kuhusu haya mambo.
 
Sijui kama swali hili ninalielekeza kwa a "right person"

Endapo kama navyodhani, kampuni yake ndo ya kwanza kuanza kuingiza nguo za "mtumba" for business; Je, Mhe. haoni kwamba kampuni yake imechangia kuuwa uwezekano wa kuwa na viwanda vya nguo? Je hilo haliwezi kuwa limeipatia nchi hasara ya kiuchumi?
 
beahunja

Mkuu, Mbona maswali mengi namna hii, kama ukiombwa uchague swali moja tu katika haya ambalo aulizwe ili kutoa nafsi kwa maswali ya waulizaji wengine ungechagua swali gani?
 
Last edited by a moderator:
Nina maswali kadhaa kuelekea uendeshaji wa kampuni za Mohamed Dewji:

1..Je,anajua kwamba kwenye pale Head Office-Morogoro Road kuna kuna vyoo vya aina mbili,kuna kimoja kichafu kipo ground floor ambacho wanatumia watu weusi na vingine visafi ambavyo vinatumiwa na wahindi? Hata funguo kuna mbili ile ya wahindi hauwezi kupata mtanzania.Ubaguzi uliokithiri,Je amehalalisha 'Apatheid Policy' kwenye makampuni yake?

2..Je anajua kwamba baadhi ya kampuni zake zinakwepa kwa makusudi kuwalipia wafanyakazi wake ule mchango wa mifuko ya kijamii kama NSSF?

3..Je,anajua kwamba wafanyakazi hasa watanzania wanalipwa mishahara kupitia payment vouchers na pia mshahara karibia nusu unaandikwa kuwa allowance hewa ili kukwepa kuchangia kiasi stahili kwa wafanyakazi wake kwenye mifuko ya kijamii?

4..Je,ana mpango gani na yale mashamba makubwa(Mfano...Alavi sisal estate la Kibaha approx. 6000Ha) ambayo hayafanyii lolote na wala hawekezi kitu badala yake ananyonya kilichopo tu na kushindwa kabisa kuyaendeleza?Mikopo aliyochukua kwenye mabenki kwa kutumia yale mashamba amepeleka wapi?

5..Mheshimiwa Mohamed Dewji anajiita mtanzania mwenzetu lakini kwa nini amejaza wahindi huku akiwalipa mishahara hadi mara tatu ya ile wanayolipwa watanzania katika ngazi zile zile za kiutendaji?

6..Je, anajua kwamba wafanyakazi watanzania wananyimwa likizo kwa wakati kwa kuzungushwa saaaana wakati wahindi wanapewa ruhusu za kwenda likizo zilizogharamiwa na kampuni?

Naomba atoe majibu yenye kueleweka kuhusu haya mambo.

Ikiwezekana itabidi aje japo na Chief Accountant pamoja na HR Manager wake naona.
 
Swali la Mwisho:

Anajisikiaje kuwa na utajiri mkubwa katikati ya watu masikini sana, akitaka kutoa majibu ya jumla sawa, akionyesha kusita muambie achague jibu kati ya haya;
(a) Masikini wote ni kwa sababu ya kujitakia kwao
(b) Anaona Fahari na anajisifu kwa mafanikio yake
(c) Hajawahi kufikiria kitu kama hicho
(d) Ni Mapenzi ya Mungu kuchagua wachache awapendao na kuwapa mazuri yote ya dunia hii.
(e) It is non of his business
 
1. Katika kampeni 2010 aliahidi kuweka nyasi uwanja wa namfua tena mbele ya Rais na hajatekeleza hadi leo je ilikua ni danganya toto??

2. Atumbie ni kiasi gani amekusanya toka kwa wahisani wa nje kupitia mfuko wa Singida yetu na kwanini amekua akificha hilo na kujidai kuwa miradi yote inaendeswa kwa fedha zake bila kuwataja wafadhili hao kitendo kilicho sababisha wajitoe??

3. Kwanini ameshindwa kuwajengea uwezo wananchi kwa kuwekeza jimboni kwake badala yake anawekeza zaidi mikoa mingine?? Haoni sasa wakati umefika wa yeye kugombea huko alikowekeza zaidi??

4. Kwanini yeye kama mbunge ameshindwa kuonyesha mfano kwa wakazi wa singida kwa kujenga nyumba ya kisasa jimboni kwake na badala yake amekua akiishi gest kama mgeni??

5. Kwanini muda mwingi haonekani jmboni wala bungeni? Na inapotokea unashida na mbunge hatujui pa kumpata na hata ukienda ofisini hupati ushirikiano wa kutosha kwani katibu wake nae muda mwingi anakua kwenye miradi yake binafsi.

6. Kwa matatizo haya kwnini asitangaze rasmi kustaafu ubunge kabla hatujamwajibisha??

7. Kwanini baada ya uchaguzi aliwaita wasimamizi wa uchaguzi na kuwapa hela SH. elfu 50 kila mmoja je ilikua ni malipo ya kazi aliyowatuma ya kumsaidia kuba kura??

8. Mradi wake wa kuweka nyasi uwanjani utakapokamilika utamfaidisha nani? Maana mkoa hauna timu na hata uwanja haujakamilika na yeye alisaidia kuhujumu timu yetu ya Singida United na kuihamishia Dar na kisha kuiua kwa alichodai inamtia hasara je nani alimwambia sisi tuliianzisha ili tupate faida badala ya burudani?
 
Pia muulize anaifahamu au alishawahi kuitembela JF? Kama ni ndiyo nini maoni yake kuhusu JF? Kama siyo anaweza kuja kuitembelea na kujibu maswali ya wananchi na wakazi wa Jimbo lake bila kusubiri tena "Makutano?"
 
Ikiwezekana itabidi aje japo na Chief Accountant pamoja na HR Manager wake naona.
Yes good idea itakuwa vizuri akija na hao watu pamoja na mmoja wa directors ambaye anaweza kutueleza japo kwa dondoo strategic direction ya MeTL.

-Huyo HR anapaswa ajibu kwa nini watu walioajiriwa hawapewi mikataba yao kila siku wanapigwa tarehe tu.
 
Kuna video clip moja naiona kituo flani cha TV akishangilia huku akiwa kifua wazi. Je, kwa hadhi yake ya ubunge haoni kuwa ile kitu inamdhalilisha? Je, ndio aina yake ya ushangiliaji kila anapofurahi?
 
Katika kipindi cha Makutano Jumamosi ijayo mgeni atakaeongea na Fina Mango ni mbunge wa Singida Mjini Mheshimiwa Mohammed Dewji atakaeongea masuala mbalimbali ikiwepo maisha yake binafsi, ya kisiasa na kibiashara.

Kama una swali lolote ambalo ungependa Mheshimiwa Dewji alijibu tafadhali uliza na litasomwa hewani siku ya kipindi kuanzia saa tisa mchana kupitia 92.9FM Dar, 93.3FM Dodoma, 98.6FM Arusha/Moshi, 101.7FM Dodoma.

Karibu

Your company has been fairly successful as one of the first Tanzanian multinational companies.
What are some of the lessons that you can share with others in the private sector that seek to venture across our borders?
 
Mohamed Dewji wakati anagombea ubunge kwa mara ya kwanza, alishinda kwenye kura za maoni, ambapo mwenzake Musa Nkhangaa alilalamika kuwa Dewji alitoa rushwa ya unga kwa wapiga kura, matokeo yaliyotengua ushindi wake, na mshindi wa tatu akawa ndiye mgombea na kuwa mbunge.

Nakumbuka wakati anatenguliwa ushindi, kigezo alichotumia mwenyekiti wa ccm wakati ule Benjamin Mkapa ilikuwa ni kwamba Dewji bado ni kijana, na hajakomaa kisiasa. Dewji kwa hasira akasema ili Mkapa ajue nimekomaa kisiasa, atamalizia kuijenga ofisi ya ccm ambayo ilianza kujengwa tokea 1975.

Swali:
Ni vipi ile ofisi ambayo ilikuwa ghorofa moja tayari ameshaijenga kwa muda wote ambao ameshakuwa mbunge?
 
Aelezee sakata la pesa za walibya kujenga kiwanda cha cement,jinsi membe alivyofisadi pesa asiogope!
 
Swali

Kwanini makampuni yake yote yanatoa ajira kwa raia wengi wa kigeni hasa India na Pakistan? Ina maana waTanzania wazawa [weusi] hawana ujuzi wa kutosha au Mohamed Dewji ana vile vidharau vya wahindi walivyonavyo dhidi ya waTanzania?

Hili namjibia:

Kwa sababu:

Wafanya kazi wa Kitanzania wengi ni wavivu, wezi, waongo, hawaishi kufiwa na kuomba ruksa za kwenda kuzika, hawaishi kuumwa, hawaishi kuwa na kila sababu za kutokuhudhuria kazini. Watu wa India wanajuwa dhiki ya maisha na vipi kupata kazi ni kugumu na wao huchapa kazi na hawana visingizio kama Watanzania.

Inapaswa Watanzania wanaotaka maendeleo ya haraka wabadilike.

Oops, nilisahau:

Hawaishi kukopa (kujichotea) makazini, hata iwe ni viongozi wa vyama vya siasa.
 
Back
Top Bottom