Dividend
JF-Expert Member
- Jan 15, 2017
- 2,080
- 3,261
Kweli hata mimi nimeona kuna maamuzi aliyofanya sio sahihi.Siungi mkono jamaa alivyomalizana na Ever but wote wana makosa.
1. Ever..alikosa utovu wa nidhamu kumleta ex nyumbani kwake, wagombane hadi majirani wajue huu ni udhalilishaji mkubwa kwa mwanaume unayeishi naye.
2. Hapakuwa na sababu ya kumtuma mwenye nyumba kupiga kufuli mlangoni.
Udikasirike kiasi cha kuutweza utu wa mtu kiasi hicho.
3. Haikuwa busara katikati ya sakata bichi ulipe kisasi kwa kuingiza mwanamke mwingine, hii inaweza kuleta maafa.
4. Likikupata jambo zito, jitahidi kujipa muda wa kufanya maamuzi, ukuwa na hasira mbichi kamwe huwezi kufanya maamuzi sahihi.
Kwa mfano alimkuta mwanamke anaishi kwake na ana maisha yake, baadae akamlazimisha ahame hapo kwake alafu baadae anakuja kumdhalilisha kwa kumfungia nje na bado kumtolea vitu nje