Evarist Chahali, hili limenitisha!

Chahali ni TISS, sema aliasi. Ingawa kuna usemi usemao "Ukishakula nyama ya mtu........"

Ni kawaida watu wa idara hizi duniani kote kufuatiliana, sishangai na wala haitokei kwake tu. Labda kama anatafuta public sympath

Umenena ukweli msipoteze muda kujadili hili yeye anajua vizuri chanzo cha yote hayo,anacheza na akili zenu tu anapima upepo aone ni kiasi gani anakubalika huku home anachotaka ni huruma zenu ili kuandaa mazingira yake ya baadae atakaporudi na kutaka nafasi fulani
 
ATTENTION SEEKER AT WORK.

Kitu cha ajabu hata mleta mada hamfahamu huyu jamaa. achilia mbali watanzania wengine wa kawaida.

Humu duniani ogopa sana hii kitu inayoitwa spinning. Huyu jamaa sitashangaa kama anatengeneza mazingira ya kutaka kuuza makala zake 'mahili' za kisiasa.

Haitakuwa ajabu kama hatawaokota wengi ambao ni matajiri wa fikra finyu.

Kama walioko ground zero wanatembeza siasa ambazo mpaka serikali inakuna kichwa na bado wako huru kutembea mitaani na kunywa kahawa kwenye vijiwe. Yeye huyu jamaa amefanya nini mpaka serikali ipoteze pesa kwa ajiri ya gharama za Convert operation.

Kwa mawazo kama hayai, basi hitimisho ni kila mtanzania maisa yake yako hatarini.

hata kuandika kunakushinda. Bogas!!!
 
Mkuu, kama uliwahi kuwa mmoja wa watu hawa, tena umewahi kushiriki covert mission yoyote na ukaachia ngazi basi ujue lazima utawindwa. Si ajabu, haishangazi hata kidogo. Chahali anajua sababu ya kufuatiliwa, anajua wazi hata akiandika gazetini wakiwa wamedhamiria kuikamilisha kazi yao kwake watamfikia tu. Najua, kuandika ni ku-pre-empty lakini inaweza isifanye kazi kama mkakati upo. Si yeye pekee alokimbia, wapo wengi. Yeye anatambulika kwa jina, wengine ni undercover mara zote.

Sitaki kuamini kuwa Chahali ana mkakati wa kuipindua serikali, hapana; makala zake chokonozi kwa Idara yawezekana ndiyo yanayomgharimu. Hata ukiwa CIA ukaasi, ukianza kuandika makala za kuiponda ujue hatma yako iko hatarini.

Hakuna idara takatifu; labda ingetokea Ikulu ikawa takatifu. Alofanya mission ya Ulimboka si mtu wa TISS, ni wahuni wanaoingizwa huko bila kufata ethics na hawana utaalam wowote wa covert missions. Angekuwa mtu maalum wa kazi, basi Ulimboka angekuwa historia kwa sasa.

Kwa kauli hii na ya chahali naamini kuwa hata hao wanaomfuatilia ni wahuni, inawezekana vipi wakangamuliwa na polisi wa huko? Tena sio scotland yard, inaonekana ni polisi wakawaida wamestukia mchezo.
Na yeye kumbuka kasema wabaya wake sio TISs kama taasisi ila ndani ya TISS kuna wahuni na ndio wanaomfuatilia.
 
Nina wasiwasi kama hajapata uraia wa UK na anapenda kuishi, inawezekana anajaribu kutengeneza mazingira ya kuomba hifadhi kwa kisingizio cha kwamba hawezi kurudi nyumbani kwa sababu maisha yake yako hatarini. Nimegongana na kesi za aina aina kama hizi ambazo watu wamefanikiwa kuwa convince watu wa Home Office na wakafanikiwa.

I'm just guessing as everything is possible.
 
JUMAMOSI Februari 2 mwaka huu itabaki katika kumbukumbu zangu kwa muda mrefu, pengine katika uhai wangu wote.
Majira ya saa 3 asubuhi nilikurupushwa usingizini na kelele za mlango uliokuwa ukigongwa kwa nguvu. Wakati ninajiandaa kwenda kufungua mlango, nikasikia sauti yenye dharura ikisema, "bwana Chahali, polisi hapa, tafadhali fungua mlango."
Nilichanganyikiwa kwani tangu nifike nchi hii zaidi ya miaka 10 iliyopita sijawahi kufanya kosa lolote au kukwaruzana na vyombo vya dola/sheria.

Baada ya kufungua mlango, askari waliovalia kiraia walijitambulisha na kuonyesha vitambulisho vyao. Pia walinisihi kuwa nisiwe na hofu ya kudhani kwamba nimefanya kosa lolote.

Kwa kifupi, walinieleza kuwa wamepewa ujumbe kutoka moja ya taasisi za intelijensia za hapa kuwa kuna tishio la uhakika dhidi ya maisha yangu. Hata hivyo, walieleza kuwa kwa vile wao walipewa tu ujumbe huo na kutakiwa kuuwasilisha kwangu, hawakuwa na maelezo ya ziada. Walisisitiza kuwa nichukue tahadhari muhimu na kunipa maelekezo ya mawasiliano ya dharura.

Kwa vile nilikurupushwa usingizini, awali taarifa hiyo ilionekana kama ndoto iliyokuwa inaendelea hata baada ya kutoka usingizini. Ilinichukua takriban saa tatu kuzinduka kutoka katika mshituko huo, na kutambua uzito wa taarifa niliyopewa na polisi hao.
Nikaamua kwenda kituo kimoja cha polisi kupata ufafanuzi zaidi. Mara baada ya kujitambulisha, mazingira ya namna suala hilo lilivyokuwa likishughulikiwa kituoni hapo lilinipa picha kuwa jambo hilo lina uzito. Kwa kifupi, baada ya kitambo nilipewa ufafanuzi ambao haukutofautiana na maelezo niliyopewa awali na polisi walionitembelea katika makazi yangu.

Kikubwa ni kuwa taarifa hiyo ilionyesha kuwa tishio hilo dhidi ya maisha yangu linatokea huko nyumbani. Swali linaloendelea kunisumbua kichwa ni KWA NINI iwe hivyo.

Wakati si vigumu kwangu kuhisi wahusika wa mpango huo wa kijahili, napata shida kuelewa kwanini wahusika hao watumie fedha za walipakodi kuandaa operesheni ya kutaka kunidhuru ilhali ninaamini kwa asilimia 100 kuwa mimi si tishio kwa usalama wa Taifa letu.
Ndiyo, baadhi ya ninayoandika kwenye makala zangu na tweets zangu huko kwenye mtandao wa kijamii wa twitter yanaweza kuwachukiza baadhi ya watu, lakini kwa hakika kuchukizwa huko si sababu ya kutaka kunidhuru.

Hadi wakati ninaandika makala hii nimekuwa nikiishi kwa tahadhari kubwa. Faraja kubwa kwangu inatokana na sababu tatu za msingi. Kwanza, kwa vile nilizaliwa na kukulia katika familia inayomtanguliza Mungu katika kila jambo, nina imani kubwa kuwa mamlaka pekee kuhusu uhai wangu (yaani kuwa hai au kufa) ni Mungu pekee. Hakuna mwanadamu anayeweza kupora jukumu hilo la Mungu na kufanikiwa kufupisha uhai wa yeyote.

Pili, nina imani kubwa na taasisi za usalama za hapa Uingereza. Kimsingi, wenzetu hawa wanathamini sana usalama na uhai wa binadamu pasi kujali mhusika ni mzaliwa wa hapa au ni ‘mgeni' kama mimi. Ushauri na sapoti ninayoendelea kupata inanipa matumaini makubwa kuwa nipo kwenye ‘mikono salama.'

Lakini tatu ni ukweli kwamba takriban miaka mitano sasa nimekuwa nikiishi na uelewa kwamba kuna baadhi ya watu huko nyumbani wanaoniona kama kimelea cha maradhi hatari ambacho kikiachwa bila kudhibitiwa kitazua balaa.

Kwa sababu hiyo, tangu wakati huo nimekuwa nikiishi kwa tahadhari japo si kubwa kama hii ninayolazimika kuichukua sasa. Lakini ili uweze kuchukua tahadhari ni lazima uwe na mbinu na ujuzi wa kuchukua tahadhari husika. Kwa bahati nzuri, watu hao wanafahamu fika kuwa nina ujuzi wa kutosha na kuelewa na kumudu fika mbinu za kuishi kwa tahadhari.

Hata hivyo, kumudu mbinu ni suala moja na kuishi kwa kutumia mbinu hizo ni kitu kingine. Si jambo la kupendeza hata kidogo kuishi ukiwa na uelewa kuwa siku moja, mahala fulani unaweza kukumbana na madhara fulani. Lakini kadri unavyolazimika kuishi kwa namna hiyo inakuwa kama sehemu muhimu ya maisha yako, na ndivyo ilivyo kwangu.

Pamoja na kuchukulia kwa uzito taarifa hizo za tishio dhidi ya uhai wangu, nimechukua hatua nyingine kadhaa ikiwa ni pamoja na kuwafahamisha watu ninaohisi kuwa ndio wahusika wa mpango huo dhalimu kwamba ni ukosefu wa busara wa hali ya juu kupoteza fedha za walipa kodi kutaka kunidhuru.

Ingekuwa vema raslimali zinazotumika kufanikisha mpango huo zikaelekezwa kwenye uchunguzi wa mabilioni ya fedha za Watanzania yaliyofichwa kwenye mabenki nchini Uswisi huku nchi yetu ikikabiliwa na deni kubwa la ndani na nje la zaidi ya shilingi trilioni 30!

Licha ya kuwa na mwangaza kuhusu mahala linakoanzia tishio hilo kutoka huko nyumbani, sina hakika kama ni mkakati wa kitaasisi au ndiyo yaleyale niliyowahi kuandika katika makala yangu moja huko nyuma juu ya kuwapo kwa rogue elementskatika taasisi zetu nyeti.
La muhimu kwangu kwa sasa ni kuhakikisha kuwa majahili hao hawafanikiwi katika azma yao. Pia sioni haja ya kuvifahamisha rasmi vyombo vya dola huko nyumbani. Itoshe tu kusema hapa kwamba mipango kama hii katika zama hizi haina tena tija.

Hakika suala hili limenikera sana lakini ninajitahidi kuzingatia busara za mwandishi wa Laws of Power, Robert Greene, ambapo kanuni ya 21 inausia kuwa "Play a Sucker to Catch a Sucker – Seem Dumber than your Mark" (yaani, kwa tafsiri isiyo rasmi, jifanye mjinga kumnasa mjinga).

Kanuni hii inasema, ninanukuu, "No one likes feeling stupider than the next persons. The trick, is to make your victims feel smart – and not just smart, but smarter than you are. Once convinced of this, they will never suspect that you may have ulterior motives" (hakuna mtu anayependa kuonekana mpumbavu zaidi ya mtu mwingine. Ujanja ni kumfanya mlengwa wako ajione mwerevu, na si mwerevu tu bali mwerevu zaidi yako. Pindi akaamini hivyo, hatohisi kuwa una nia kubwa zaidi yake).

Nimalizie makala hii kwa kusisitiza kuwa vitisho kama hivi kamwe havitonizuwia kusimamia ukweli na kuuhubiri pasi kumhofia mtu au taasisi.

Ninatambua yaliyowakumba baadhi ya waandishi wa habari wa nyumbani.

Kwangu hizo ni chachu za kuendeleza walichoanzisha.

Kadhalika, ni vema walioandaa mpango huo dhalimu wakatambua kuwa licha ya kitendo hicho kuwa na uwezekano wa kuharibu ‘mahusiano ya kiusalama' kati ya nchi yetu na Uingereza (kwa kuwatwisha mzigo usio wa lazima kuhakikisha mimi kama mkazi wa nchi hii sidhuriwi), lakini pia kinakwaza kiapo changu cha utii kwa nchi yangu (nilipokuwa mtumishi wa umma) ‘kuyaacha mambo fulani yaendelee kubaki yasiyopaswa kuongelewa hadharani.' Laws of Power ya 19 inasisitiza, "Never offend a wrong person" (kamwe usimkorofishe mtu asiyestahili).

"If you're not ready to die for it, take the word 'freedom' out of your vocabulary" ~ Malcom X

Raia Mwema - Tishio la uhai mlangoni kwangu

Rai yangu kwa wahusika ni kwamba kama ambavyo acid attack kwa Kubenea na torture dhidi ya Ulimboka havijaweza kuzima kelele za kudai Tanzania tunayostahili, operesheni za kihuni kama hii inayonilenga haitozaaa matokeo tarajiwa. Ni vema jitihada za kiharamia kama hizi zikaelekezwa kwa majambazi walioficha fedha huko Uswisi na visiwa vya Jersey badala ya kuwaandama raia wasio na hatia.

Kadhalika, lengo la makala hii sio kusaka sympathy bali kuujulisha umma jinsi kunshindwa ku-export mazao ya wakulima wetu yanayooze amashambani kunavyokuwareplaced na export of terror overseas.

Kwa atakayehitaji ufafanuzi zaidi, anaweza kuomba taarifa zaidi kwa ku-cite 'Freedom of Information Act' kwa kituo cha polis cha Maryhill hapa Glasgow, UK. Namba yao ya simu ni +44-[FONT=MuseoSans_300]141-532-2000 na barua-pepe ni [/FONT]MaryhillandKelvinCommunityPolicingTeam@strathclyde.pnn.police.uk
 
Raia Mwema - Tishio la uhai mlangoni kwangu

Rai yangu kwa wahusika ni kwamba kama ambavyo acid attack kwa Kubenea na torture dhidi ya Ulimboka havijaweza kuzima kelele za kudai Tanzania tunayostahili, operesheni za kihuni kama hii inayonilenga haitozaaa matokeo tarajiwa. Ni vema jitihada za kiharamia kama hizi zikaelekezwa kwa majambazi walioficha fedha huko Uswisi na visiwa vya Jersey badala ya kuwaandama raia wasio na hatia.

Kadhalika, lengo la makala hii sio kusaka sympathy bali kuujulisha umma jinsi kunshindwa ku-export mazao ya wakulima wetu yanayooze amashambani kunavyokuwareplaced na export of terror overseas.

Kwa atakayehitaji ufafanuzi zaidi, anaweza kuomba taarifa zaidi kwa ku-cite 'Freedom of Information Act' kwa kituo cha polis cha Maryhill hapa Glasgow, UK. Namba yao ya simu ni +44-[FONT=MuseoSans_300]141-532-2000 na barua-pepe ni [/FONT]MaryhillandKelvinCommunityPolicingTeam@strathclyde.pnn.police.uk

Mmm, I can smell something fishy.

Kwanza haileti hata tone la wazo na kufikiria serikali inataka kufanya mambo yaishe kwa huyu jamaa kwa njia ya convert mission wakati hata katika wachangiaji wa mada ambazo ni mwiba kwa serikali kwenye Raia Mwema hayupo hata kwenye five bora. Jina lake haliwezi hata kuwa kwenye mengineyo, in case, I stress, If convert mission sanctioned.

Kuna watu wanaojulikana ambao ni kikwazo hata kwa wafisadi na kama kungekuwa na mission za namna kama ya huyu jamaa anayotaka kutuaminisha, basi hao watu ndiyo wangeonekana kwenye flont page ya convert mission. Lakini mbona wako huru mitaani bila hata walinzi.

inawezakana pia hii kitu imetokea lakini nothing to do with TISS. labda katika mapito pito yake ya hapa na pale, ameacha watu ambao kwa sasa wana mihasira na grudge na wameamua kumfanyia kwa kupiga simu polisi UK kwa sababu kwa wenzetu every threat to individual, wanachukua very serious.

Labda anatengeneza mazingira ya kupata makaratasi kwa njia hii ambapo kuna kesi kama hizi zimetokea na watu wakafanikiwa. Point hii inanipelekea kuhoji, Kwa nini awahimize watu na kuwapa mawasiliano ya polisi UK ili wapige simu kujua kinachoendelea. Kwa faida ya nani? Kama siyo kutengeneza vielelezo mbadala kwa ajili ya kuviwasilisha kwenye Immigration and Asylum Tribunal UK ili viwe ni chagizo la madai.

We'll never know the motives.
 
ATTENTION SEEKER AT WORK.

Kitu cha ajabu hata mleta mada hamfahamu huyu jamaa. achilia mbali watanzania wengine wa kawaida.

Humu duniani ogopa sana hii kitu inayoitwa spinning. Huyu jamaa sitashangaa kama anatengeneza mazingira ya kutaka kuuza makala zake 'mahili' za kisiasa.

Haitakuwa ajabu kama hatawaokota wengi ambao ni matajiri wa fikra finyu.

Kama walioko ground zero wanatembeza siasa ambazo mpaka serikali inakuna kichwa na bado wako huru kutembea mitaani na kunywa kahawa kwenye vijiwe. Yeye huyu jamaa amefanya nini mpaka serikali ipoteze pesa kwa ajiri ya gharama za Convert operation.

Kwa mawazo kama hayai, basi hitimisho ni kila mtanzania maisa yake yako hatarini.

SPINNING. Sounds like my friend omarilyas. Jaribu kuutendea haki ubongo wako kwa kuutumia ipasavyo.Ni-spin ili iweje?Ni-seek attention kwa kudai nimetishiwa maisha, then what? Kama ni attention, nina blog iliyokwishatembelea na zaidi ya watu milioni 1,nina followers twitter zaid ya 200, na gazeti ninaloandikia makala kila wiki linalosomwa na watanzania zaidi ya milioni 10 kila wiki.

Unahoji serikali yetu na fedha za kuchezea?Though I'm in no way suggesting kuwa tukio hilo lina mkono wa serikali (though I'm not denying such a possibility),kila mwenye uelewa wa utendaji kazi wa serikali ya Kikwete anafahamu priorities zake ziko wapi.

All ain all, dhima ya makala yangu haikuwa ku-seek attention wala kusaka sympathy ya umma.Tangu mwaka 2006 nimekuwa nikiandika makala magazetini huko nyumbani,nikiongozwa na imani kuwa habari haina maana if it can't be shared.Kamwe sijawahi kuweka angalizo kwenye makala zangu kuwa LAZIMA UAMINI.Na huo ndio uzuri wa habari.Hulazimishwi kuamini.Na kila ninapoandika makala,kamwesijawahi kuwa na dhamira ya kuwashawishi wasomaji waniamini.

Makala yangu kuhusu tuklio hili ilikuwa haina tofauti na makala nyinginezo: nilikuwa nahabarisha hadhira yangu.Uamuzi wa kuamini au kutoamini,kuguswa au kupuuza unabaki mkononi na moyoni kwa msomaji.

Na kama mwana-JF tangu mwaka 2006,siku zote nimekuwa nikiitumia ipasavyo haki yangu ya kubandika posts hapa pasi hofu kuwa LABDA ITADHANIWA NI UZUSHI.Once nishaandika na kupost kitu,kilicho kichwani kwa msomaji is completely none of my headaches.

Suala kubwa ni kuwa kwa nini atishiwe maisha,tena mbali na nyumbani? Je ana organize mpango wa kupindua serikali? Je makala zake ndani ya Raia Mwema? Naamini haya ndo maswali ya msingi ambayo tunatakiwa tutafakari.
Kuna suala la Ulimboka ambao limeitia doa idara yetu takatifu na hili likiwa ni kweli ina maana kuna kasoro fulani mahali fulani.

Na ndio dhima ya makala yangu: WHY

"if u are not ready to die for it,take the word 'freedom' out of your vocabulary-Malcolm X"
Kama kweli una nia ya kuendeleza mapambano basi GO ON but kama ni pandikizi ni bora tu urudi kwenu kama walivyofanya wakina stupid Shonza.

Yes,I'm nobody lakini nadhani mkuu umenidhalilisha mno kunilinganisha na hao wachumia-tumbo. I'm no political prostitute.


Mkuu, kama uliwahi kuwa mmoja wa watu hawa, tena umewahi kushiriki covert mission yoyote na ukaachia ngazi basi ujue lazima utawindwa. Si ajabu, haishangazi hata kidogo. Chahali anajua sababu ya kufuatiliwa, anajua wazi hata akiandika gazetini wakiwa wamedhamiria kuikamilisha kazi yao kwake watamfikia tu. Najua, kuandika ni ku-pre-empty lakini inaweza isifanye kazi kama mkakati upo. Si yeye pekee alokimbia, wapo wengi. Yeye anatambulika kwa jina, wengine ni undercover mara zote.

Sitaki kuamini kuwa Chahali ana mkakati wa kuipindua serikali, hapana; makala zake chokonozi kwa Idara yawezekana ndiyo yanayomgharimu. Hata ukiwa CIA ukaasi, ukianza kuandika makala za kuiponda ujue hatma yako iko hatarini.

Hakuna idara takatifu; labda ingetokea Ikulu ikawa takatifu. Alofanya mission ya Ulimboka si mtu wa TISS, ni wahuni wanaoingizwa huko bila kufata ethics na hawana utaalam wowote wa covert missions. Angekuwa mtu maalum wa kazi, basi Ulimboka angekuwa historia kwa sasa.

The thing is hataki kusema na kurudisha hesabu za wenyewe,yeye anavuta mshiko wa kazi maalumu halafu hatekelezi ndio maana wenzake hawamuelewi,hebu tumuulize riports zao zote amerudisha?,labda wenyewe wanadoubt huenda akazitoa gazetini au zikafika pahala sipo,mind kuwa muhaini sio lazima ubebe bunduki!!

Mkuu wagu, una njia mwafaka zaidi kwa mwajiri kudai ufanisi wa mwajiriwa,and none of that is using threats.Natambua kuwa tafiti nyingi huanza na hisia lakini ili hisia zipelekee tafiti yenye maana ni vime hisia hizo zikawa na kicha na miguu (i.e. they make sense)

Mtu yeyote mwenye akilitimamu anatambua kuwa kukorofishana na mwajiri wake wa zamani hakumaanishi uhuru wa kuvunja sheria zilizotawala ajira ya mtu huyo.

Huyu bwana huwa ananiacha hoi kwa jinsi anavyojifikiria kuwa yeye ni maarufu, hizo makala zenyewe anazoandika huwa hazina lolote la maana, kama ni mambo yake na TISS uko aache kutafuta sympathy kupitia makala, au inawezekana aliishiwa cha kuandika.

Acha uvivu wa kufikiri.Hivi kwa busara zako,njia pekee ya kusaka umaarufu ni kujichulia kuwa kuna watu wanataka kukudhuru?Inaleta umaarufu gani?

Ni kwa watu wenye mtizamo finyu kma wewe wanaodhani kuwa jarida mahiri kama RAIA MWEMA linaweza kutoa kolamu KWA MTU ANAYEANDIOKA KISICHO CHA MAANA tangu lilipoanzihswa Oktoba 2007. Anyway, yawezekana ninachoandika hakina maana kwako kwa vile hakitetei maslahi yako,and Ileave that to the people with functioning brains to judge.

Sidhani kama umeshawahi kukutaka na mwandishi wa makala,iwe ya udaku au ya sinsible stuff,bcoz if you had, lazima wangekufahamisha kuwa Tanzania yetu haiishiwi na vituko au kero za kupelekea andiko flani.

Baada ya kujishughulisha na uandishi wa makala kwa zaidi ya miaka 10 sasa nimejifunza kitu kimoja cha msingi: mara nyingi wanaokosoa waandishi ni watu ambao hata uandishi wa japo SMS,let alone makala ya 1000+ words, ni mgogoro kwao.Yes,uaweza kishiwa na hakuandika kwenye sms lakini sio kwa maala zinazhus TAZANIA.

Chukua tahadhari ndugu!ukijua mbinu tayari umeshashinda nusu ya vita!

Asante ndugu yangu

utawajua tu....

Exactly

Umenena ukweli msipoteze muda kujadili hili yeye anajua vizuri chanzo cha yote hayo,anacheza na akili zenu tu anapima upepo aone ni kiasi gani anakubalika huku home anachotaka ni huruma zenu ili kuandaa mazingira yake ya baadae atakaporudi na kutaka nafasi fulani

Ningechezea akili zenu kwa kuomba msaada au hurma ya umma.Neither was lengo la bandiko langu.

Tuna tatizo la msingi katika Tanzania yetu ya sasa kwamba kila anayeongele jambo flani linaloweza kugusa hisia za wengi ana malengo ya kisiasa au kusaka 'ulaji' mahala flani.Naomba nikuhakikishie (na ukiweza kufotokopi tamko hili itakuwa vema) kamwe sitarajii kujiingiza kwenye siasa au ksakafursa y uongozi huko nyumbani.Nimeridhika na kidogo nilicho nacho, na siamini kuwa njia pekee ya kuutumikia umma ni kuwa kiongozi.

Kama umeuzowea mtandao wa internet vizuri nakusihi usome article hii ya mwaka 2006 Comments za Said Nguba ~ Kulikoni Ughaibuni labda itakupa mwangaza kuwa watawala wetu ni watu wasiopenda kuambiwa THIS IS WRONG.

Sasa wewe unaogopa kufa? unadhani hayo maisha utakaanayo mpaka lini

Kwanza ninaamini kuwa hata wewe unaogopa kufa.Nobody doesn't.Lakini last time I checked everyone will ultimately die,na sijawahi kusikia kuwa uoga dhidi ya kifo umezuwia mtu kufa.

Katika Uwanja wa Mapambano, WOGA ndiyo Silaha DHAIFU kuliko zote!!!


Manyerere Jackton

mKUU,mtu mwoga asingeweza kuwa na ujasiri wa angalau kusimulia tukio hkama hilo gazetini

Kwa kauli hii na ya chahali naamini kuwa hata hao wanaomfuatilia ni wahuni, inawezekana vipi wakangamuliwa na polisi wa huko? Tena sio scotland yard, inaonekana ni polisi wakawaida wamestukia mchezo.
Na yeye kumbuka kasema wabaya wake sio TISs kama taasisi ila ndani ya TISS kuna wahuni na ndio wanaomfuatilia.

Exactly.Ni WAHUNI wa daraja la chini kabisa kwa sababu priority kwao ni kuwainda majambazi walioliibiataifaletu na kuficha fedha huko Uswisi.

But guess what, Kikwete ameenda Uswisi(same country ambapo fedha zetu zimefichwa) and all he could do ni kupiga picha na KoMBE LA dUNIA!


Nina wasiwasi kama hajapata uraia wa UK na anapenda kuishi, inawezekana anajaribu kutengeneza mazingira ya kuomba hifadhi kwa kisingizio cha kwamba hawezi kurudi nyumbani kwa sababu maisha yake yako hatarini. Nimegongana na kesi za aina aina kama hizi ambazo watu wamefanikiwa kuwa convince watu wa Home Office na wakafanikiwa.

I'm just guessing as everything is possible.

Njia bora ya kusaka ukweli inaweza kuwa sio GUESSING pekee.ASK. Do your homework.Jilize ni kwa namna gani mu anaweza kujizulia kuwa amepewa tishio from police (bearing in mind police na ukba wapo chini ya same 'Ministry' i.e. The Home Office.Nadhani kwa busara zako unaamini kuwa hawa Waingereza ni wapumbavu sana kiasi kwamba mtu anaweza kukurupuka na KULAZIMISHA POLISI wamemletee ujumbe kuwa kuna credible threat vs his life,kisha aende UKBA kuomba asylum.

Ukijihangaisha kuelewa utafahamu kuwa kuna njia rahisi zaidi za ku-sek asylum hapa UK,na siamini kabisa kuwa one of them ni kujichulia kuwa kuna wanaotaka kudhuru maisha.Na hata hiyo ingekuwa ndo njia rahisi,how did I influence the police to come up with such info?Nimemtuma mtu?Labda kwa uelewa wako tha makes sense, lakini you don;t have to be a genius kufahamu kuwa police wa hapa wana-trace kila mwasiliano yanayowajia.And why should I take such a risk?Kwa ajili ya kupata karatasi? I was born a Tanzanian, and I will die one.Utanzania wangu una umuhimu zaidi ya kitu chochote.


Mmm, I can smell something fishy.

Kwanza haileti hata tone la wazo na kufikiria serikali inataka kufanya mambo yaishe kwa huyu jamaa kwa njia ya convert mission wakati hata katika wachangiaji wa mada ambazo ni mwiba kwa serikali kwenye Raia Mwema hayupo hata kwenye five bora. Jina lake haliwezi hata kuwa kwenye mengineyo, in case, I stress, If convert mission sanctioned.

Kuna watu wanaojulikana ambao ni kikwazo hata kwa wafisadi na kama kungekuwa na mission za namna kama ya huyu jamaa anayotaka kutuaminisha, basi hao watu ndiyo wangeonekana kwenye flont page ya convert mission. Lakini mbona wako huru mitaani bila hata walinzi.

inawezakana pia hii kitu imetokea lakini nothing to do with TISS. labda katika mapito pito yake ya hapa na pale, ameacha watu ambao kwa sasa wana mihasira na grudge na wameamua kumfanyia kwa kupiga simu polisi UK kwa sababu kwa wenzetu every threat to individual, wanachukua very serious.

Labda anatengeneza mazingira ya kupata makaratasi kwa njia hii ambapo kuna kesi kama hizi zimetokea na watu wakafanikiwa. Point hii inanipelekea kuhoji, Kwa nini awahimize watu na kuwapa mawasiliano ya polisi UK ili wapige simu kujua kinachoendelea. Kwa faida ya nani? Kama siyo kutengeneza vielelezo mbadala kwa ajili ya kuviwasilisha kwenye Immigration and Asylum Tribunal UK ili viwe ni chagizo la madai.

We'll never know the motives.

Pamoja na kuuliza kwa KEBEHI kwanini kuwe na ulazima wa mango kama huo,ninalazimika kuungana nawe mkono kwani ndilo swali linalonitatiza nakimsingindilo lililopelekea kuandika makala hiyo.

Sijui kiwango chako cha uelewa wa the siocalled covert mission za TISS lakini ninachoweza kukusihi ni hiki: DO YOUR HOMEWORK. All I can gather is huelewi PRIORITIES za taasisi hiyo kwa wakati huu,and I'min no way whatsoever suggesting kuwa mie ni Priority KWAO.

You can know the motive if you bothered to ask. Inaelekea unafahamu vyema utendaji kazi wa taasisi mbalimbali hapa UK. ARE THEY THAT STUPID AS YOU SEEM TO SUGGEST? Niliweka contact details za kituo cha polisi speciafically kwa ajili ya Doubting Thomases like you.Piga simu uulize badala ya kuishia tu kusema you'll never know the motive.

Na kabla ya kujiumiza kichwa kudhani the whole thing is about makaratasi,ni vema ungeuliza residential status yangu hapa UK
 
Last edited by a moderator:
You can know the motive if you bothered to ask. Inaelekea unafahamu vyema utendaji kazi wa taasisi mbalimbali hapa UK. ARE THEY THAT STUPID AS YOU SEEM TO SUGGEST? Niliweka contact details za kituo cha polisi speciafically kwa ajili ya Doubting Thomases like you.Piga simu uulize badala ya kuishia tu kusema you'll never know the motive.


Na kabla ya kujiumiza kichwa kudhani the whole thing is about makaratasi,ni vema ungeuliza residential status yangu hapa UK

Don't tell me about it. Hivi ni watanzania wangapi ambao wamejifanya Warundi au Wasomali na wakapata/wakapewa makaratasi hapa UK. What are you talking about? IS THAT STUPIDNESS OF THE HOME OFFICE OR TANZANIAN BEING SAGACIOUS?. Hebu nifundishe hili somo.

kuhusu residence. Unataka nimuulize nani wakati wa kuulizwa ni wewe. JUST ANSWER ME. FINITO.

eeee mkuu, Mimi siingilii maisha yako, lakini unapoleta hapa allegation ukiwa maelezo kama haya. we ought to question the motives kama maelezo yana mashimo.
 
Don't tell me about it. Hivi ni watanzania wangapi ambao wamejifanya Warundi au Wasomali na wakapata/wakapewa makaratasi hapa UK. What are you talking about? IS THAT STUPIDNESS OF THE HOME OFFICE OR TANZANIAN BEING SAGACIOUS?. Hebu nifundishe hili somo.

kuhusu residence. Unataka nimuulize nani wakati wa kuulizwa ni wewe. JUST ANSWER ME. FINITO.

eeee mkuu, Mimi siingilii maisha yako, lakini unapoleta hapa allegation ukiwa maelezo kama haya. we ought to question the motives kama maelezo yana mashimo.

Kwa vile kuna Watanzania walijifanya Warundi au Wasomali kisha wakapewa makaratasi doesn't mean,moja, kila Mtanzania liyepo UK atajifanya Mrundi au Msomali kupata makaratasi.Pili,si kila Mtanzania aliyepo UK anahitaji makaratasi,na tatu,haihitaji kuwa na akili timamu kutofautisha kilichomo ktk makala yangu na kujivika Urundi au Usomali

Nikujibu kuhusu residential status yangu hapa kwa vile ukiendelea kuamini tofauti nitapungukiwa na siku za kuishi? Mie ni mkazi halali wa nchi hii nisiyehitaji 'kujilipua.' Ukitaka uhakiki wa hilo, nenda UKBA watakufahamisha

Sijaleta allegation, nilibandika habari. Sidhani hata kama ulisoma makala husika kabla ya kukurupuka na conspiracy theories zako. Katika makala yangu sikumtaja ninayemhisi kuhusika na suala hilo. Sasa utahitimishaje kuwa ni allegation pasi mtu anayetuhumiwa?

Thing is, kila wiki naandika gazetini, na kama kuna suala linanihusu na ninalodhani lina umuhimu wa kuwemo katika makala basi nitaliandika. Sijawahi kuomba approval ya mtu kabla ya kuandika makala. Na sijawahi kujihangaisha na "huyu atatafsiri hivi" au "yule atafsiri vile."

Maelezo yenye mashimo? Seriously you think nimekuwa nikitoa maelezo? Ili iweje? Kukushawishi uamini nilichoandika? Nah, I have never held anybody at gunpoint to believe what I publish on print or electronic media.
 
Kwa vile kuna Watanzania walijifanya Warundi au Wasomali kisha wakapewa makaratasi doesn't mean,moja, kila Mtanzania liyepo UK atajifanya Mrundi au Msomali kupata makaratasi.Pili,si kila Mtanzania aliyepo UK anahitaji makaratasi,na tatu,haihitaji kuwa na akili timamu kutofautisha kilichomo ktk makala yangu na kujivika Urundi au Usomali

Nikujibu kuhusu residential status yangu hapa kwa vile ukiendelea kuamini tofauti nitapungukiwa na siku za kuishi? Mie ni mkazi halali wa nchi hii nisiyehitaji 'kujilipua.' Ukitaka uhakiki wa hilo, nenda UKBA watakufahamisha

Sijaleta allegation, nilibandika habari. Sidhani hata kama ulisoma makala husika kabla ya kukurupuka na conspiracy theories zako. Katika makala yangu sikumtaja ninayemhisi kuhusika na suala hilo. Sasa utahitimishaje kuwa ni allegation pasi mtu anayetuhumiwa?

Thing is, kila wiki naandika gazetini, na kama kuna suala linanihusu na ninalodhani lina umuhimu wa kuwemo katika makala basi nitaliandika. Sijawahi kuomba approval ya mtu kabla ya kuandika makala. Na sijawahi kujihangaisha na "huyu atatafsiri hivi" au "yule atafsiri vile."

Maelezo yenye mashimo? Seriously you think nimekuwa nikitoa maelezo? Ili iweje? Kukushawishi uamini nilichoandika? Nah, I have never held anybody at gunpoint to believe what I publish on print or electronic media.

I'm confused. Who is KULIKONI UGHAID with avantar photo and who is Mlalahoi on JF.

Sasa sijui nielewe yupi ndiyo yupi na nani ndiye mwenye madai kati ya hawa wawili wenye ID's tofauti.

Ninaposema something fishy, nina maana pia vitu kama hivi. Who is Evarist CHahali in these two different ID's. siwezi nikawa ninaongea na watu wawili ambao wote ni Evarist Chahali. CAN YOU PUT ME TO BED ON THESE TWO ID's
 
I'm confused. Who is KULIKONI UGHAID with avantar photo and who is Mlalahoi on JF.

Sasa sijui nielewe yupi ndiyo yupi na nani ndiye mwenye madai kati ya hawa wawili wenye ID's tofauti.

Ninaposema something fishy, nina maana pia vitu kama hivi. Who is Evarist CHahali in these two different ID's. siwezi nikawa ninaongea na watu wawili ambao wote ni Evarist Chahali. CAN YOU PUT ME TO BED ON THESE TWO ID's


Tatizo ni IDs au kujibiwa hoja zako? Yes, mlalahoi and Kulikoni Ughaib are related. Former is my personal JF membership ID,latter's my blog's membership ID. Is that a treasonable offence?
 
Back
Top Bottom