Eti Watanzania ni wadokozi? Au Waajiri ndo wanyonyaji wanawalipa Watanzania kidogo?

MPadmire

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
3,930
3,227
Juzi Snow Crest Imefunguliwa Arusha, na wafanyakazi wageni wameajiriwa kwa wingi. Na Watanzania wameitwa wadokozi

Sababu ni nini??

Watanzania ni Wadokozi? Au Waajiri ndo wanyonyaji wanawalipa watanzania mshahara kidogo ukilinganisha na wageni.

Mfano Mshahara wa Graduate wa Kitanzania ni laki 3 while graduate wa Kenya Au Ulaya ni Millioni moja??

Huyo Mtanzania ataweza kupanga nyumba ya hadhi yake? Ataweza kupanda gari ya hadhi yake? Mtanzania ataweza kujiwekea akiba ili baadae ajenge nyumba au anunue gari au asomeshe watoto?

Kwa hiyo Wadau hapa JF jadilini kama Watanzania ni wadokozi kweli au Watanzania wanaonewa??
 
Hivi hao Wakenya wametuzidi nini wabongo hadi wawe wanalipwa mishahara inayotuzidi? Mimi kila siku huku nakutana na Wakenya ambao sioni chochote walichonizidi. Sana sana ni wachovu na washamba na wanaotamani wangekuwa Watanzania. Sielewi kabisa hii ya kuwalipa mishahara iliyotuzidi
 
Mpadmire,

Lazima tujiulize kwanza sisi wenyewe, hao Wakenya wanatuzidi nini mpaka walipwe zaidi ya mara tatu ya Watanzania?

Sidhani kama kuna mwajiri ambaye angependa akachukue wakenya na kuwaacha Watanzania wakati skills zao zinafanana.

Kwenye dunia hii ya ushindani ni bora tujiandae na kukuza skills zetu ili tushindane na hao wengine.
Inasikitisha kuona ajira zinazotengenezwa zinaenda kwa wageni huku Watanzania tunaachwa kwenye mataa.
 
Hivi hao Wakenya wametuzidi nini wabongo hadi wawe wanalipwa mishahara inayotuzidi? Mimi kila siku huku nakutana na Wakenya ambao sioni chochote walichonizidi. Sana sana ni wachovu na washamba na wanaotamani wangekuwa Watanzania. Sielewi kabisa hii ya kuwalipa mishahara iliyotuzidi

Amini usiamini kuna kitu waKenya wametuzidi... kimojawapo hiki hapa.

Mkenya akifanya kitu ana-communicate kwamba amefanya, kina faida gani kwenye taasisi husika na kuweka open kwa organization husika,

Mtanzania anaweza kufanya mambo mazuri na makubwa sana... alafu anakaa hayo aliyofanya moyoni kwake au kwenye kitengo chake...

Matokeo yake anakuwa -invisible kwenye organisation na mwishowe kuonekana hafanyi kazi!
 
Amini usiamini kuna kitu waKenya wametuzidi... kimojawapo hiki hapa.

Mkenya akifanya kitu ana-communicate kwamba amefanya, kina faida gani kwenye taasisi husika na kuweka open kwa organization husika,

Mtanzania anaweza kufanya mambo mazuri na makubwa sana... alafu anakaa hayo aliyofanya moyoni kwake au kwenye kitengo chake...

Matokeo yake anakuwa -invisible kwenye organisation na mwishowe kuonekana hafanyi kazi!

Aaah wapi! mimi nakataa katakata. Wakenya hawajatuzidi lolote. Basi tu sisi tuna matatizo yetu ya kutukuza vya nje. Ujinga mtupu.
 
Amini usiamini kuna kitu waKenya wametuzidi... kimojawapo hiki hapa.

Matokeo yake anakuwa -invisible kwenye organisation na mwishowe kuonekana hafanyi kazi!

Heeeee...!
We Kasheshe we!..Unataka ban eeh? Invisible hafanyi kazi wakati jeiefu iko hewani 24/7!
 
Wana JF mumepotosha mada. Mada sio wakenya. Mada ni sisi wa Tz wadokozi. Nasikitikitika mumeshindwa kuona kwamba rais ametuangusha hapa kwa kushabikia wageni kuchukua kazi zetu eti sisi wadokozi. Hoja ya kitoto....
 
Nadhani tofauti iliyopo ni uwezo wa kung'ang'ania tunachotaka (kujitetea kimaslahi). Wakenya wana uwezo wa kusema wanachokitaka na kukitetea.

Si kweli kuwa waKenya wanafanya kazi zaidi yetu. Wala si kweli kuwa waTanzania ni wadokozi kuliko waKenya. Inawezekana kinyume chake ikawa kweli na hiyo ni imani yangu. Mimi nimeishi Kenya nimeona uwezo wa wengi wao.

Kuna imani potofu kuwa ukijua kiingereza sana, unakuwa na ujuzi mkubwa. Labda kuna wanaoweza kutetea hoja hiyo. Ila lugha ni kitu kimoja na uwezo wa kufanya kazi ni kitu kingine. Hao wenye Crest Hotel watakuwa wanataka watu wenye uzoefu mkubwa (command) ya English. Wasitukane watu kuwa ni wezi.
 
Juzi Snow Crest Imefunguliwa Arusha, na wafanyakazi wageni wameajiriwa kwa wingi. Na Watanzania wameitwa wadokozi

Sababu ni nini??

Watanzania ni Wadokozi? Au Waajiri ndo wanyonyaji wanawalipa watanzania mshahara kidogo ukilinganisha na wageni.

Mfano Mshahara wa Graduate wa Kitanzania ni laki 3 while graduate wa Kenya Au Ulaya ni Millioni moja??

Huyo Mtanzania ataweza kupanga nyumba ya hadhi yake? Ataweza kupanda gari ya hadhi yake? Mtanzania ataweza kujiwekea akiba ili baadae ajenge nyumba au anunue gari au asomeshe watoto?

Kwa hiyo Wadau hapa JF jadilini kama Watanzania ni wadokozi kweli au Watanzania wanaonewa??
Udokozi ni tabia ya mtu: hauna rangi, kabila au taifa. Kusema kwamba watanzania ni wadokozi si sahihi, japo kwa kweli wapo baadhi yao ambao ni wadokozi kama ilivyo kwa wakenya, nk ambao baadhi yao ni wadokozi. Ila mi nadhani sababu ya watanzania kutopendelewa na wenye ajira ni tabia ya watanzania ya kutojua kujipendekeza, kulamba miguu ya waajiri. Kwa kifupi ni watu "jeuri" japo maskini. Wanajifanya wajuaji na wenye kujua haki zao. Waajiri wengi hawapendi watu wa aina hii. Wanawakimbia na kukimbilia wale wenye kusema "ndiyo mkuu" na kutetemekea mwajiri.

Pili, ni kasumba tu! kwamba msomi kutoka Kenya ni bora kuliko msomi wa Tanzania. Huu ni ugonjwa! Hasa ukizingatia na ung'eng'e wa kubahatisha wa wasomi wengi wa kitanzania. Kumbe kwa kuwa lugha hiyo "tukufu" hawaimung'nyi vilivyo inaonekana kwa waajiri kwamba hawakusoma sawasawa. Jambo ambalo si kweli. Wanashindwa kutofautisha kati ya maarifa na lugha.
 
Nimepigwa BUTWAA na hii assumption ya rais wetu kukubaliana na hoja ya KIJINGA kutoka kwa wamiliki wa hoteli.
Kama ni udokozi, kwani vyombo ya dola vipo kwa ajili ya nini? Huyu rais kweli ananichosha. unamchekea mtu anayemtoboa mwanao macho?

Nadhani wawekezaji wa kigeni wameshamjulia muungwana wetu kwamba tell him anything that makes him to SMILE.

Am soooo down very low ktk hili suala
 
Tatizo ni viongozi wetu waliowafanya weatanzania kuwa wadokozi, bila kuwabadili viongozi hao, basi mwendo wetu utakuwa hivyo, kitu kimoja cha msingi kinacho wafanya watanzanias kuwa wadokozi ni
kukosa mikopo ya kujenga nyumba, hivyo kumlazimisha mtu atafute mashali pakuanzia kwa wizi.
pili ni viongozi wenyewe kuwa wadokozi hivyo hawaoni shida za watanzania wengi. na kufikiria kwamba watu wanaweza kuishi bila mikopo.
nk nk
 
Aaah wapi! mimi nakataa katakata. Wakenya hawajatuzidi lolote. Basi tu sisi tuna matatizo yetu ya kutukuza vya nje. Ujinga mtupu.


mkuu nakuunga mkono 100% kabisa wakenya hawatuzidi lolote bali ni uwoga wetu watz na zaidi ni hatuna confidence hususani pale tunapomwona mgeni...hapo ndo tatizo kubwa huanzia, tunauwezo zaidi yao kabisa...mie naishi,nasoma,nafanya kazi nao hapa Europe mbona sioni walilonizidi.....wabongo tuache woga mazee....we can do the best of best.
 
mkuu nakuunga mkono 100% kabisa wakenya hawatuzidi lolote bali ni uwoga wetu watz na zaidi ni hatuna confidence hususani pale tunapomwona mgeni...hapo ndo tatizo kubwa huanzia, tunauwezo zaidi yao kabisa...mie naishi,nasoma,nafanya kazi nao hapa Europe mbona sioni walilonizidi.....wabongo tuache woga mazee....we can do the best of best.
Suala hapa si woga! Suala ni kwamba waajiri wanatunyanyapaa watanzania. hawatutaki. sababu yao ni kwamba tuko wadokozi.
 
Wana JF mumepotosha mada. Mada sio wakenya. Mada ni sisi wa Tz wadokozi. Nasikitikitika mumeshindwa kuona kwamba rais ametuangusha hapa kwa kushabikia wageni kuchukua kazi zetu eti sisi wadokozi. Hoja ya kitoto....
Kunjygroup,
Nakubaliana na wewe kuwa rais ametuangusha. Amewapa aid and comfort wawekezaji ambao wanavunja sheria kwa kuleta "so called wafanyikazi" kutoka nchi zao hata kwa nafasi za kazi ambazo zingefanywa vizuri tu na Watanzania. Amewapa justification ya kuendelea kuleta makarani, madreva, wapishi kutoka nchi zao simply kwa kuwa hata rais anaafiki kuwa Watanzania ni wadokozi.
 
..wananchi na sisi turuhusiwe kuchagua expatriates ktk nafasi ya Raisi kwasababu hawa wazazi [mwinyi,mkapa,kikwete] wameishia kuwa wezi wakubwa.
 
Hivi hao Wakenya wametuzidi nini wabongo hadi wawe wanalipwa mishahara inayotuzidi? Mimi kila siku huku nakutana na Wakenya ambao sioni chochote walichonizidi. Sana sana ni wachovu na washamba na wanaotamani wangekuwa Watanzania. Sielewi kabisa hii ya kuwalipa mishahara iliyotuzidi

Juli:

Ukienda Kenya matajiri wa matatu wanapenda vijana wa Tanzania kwa sababu mashapu. Hivyo kuna vitu tuna-excel kuliko waKenya.

Tukirudi kwenye kazi za professional. Kuna kitu watanzania wa-lag behind. Kwanza english kwa watanzania wengi ni second language. Lakini wengi hatutaki ku-improve.

Hivyo kuna uwezekano mkubwa kuwa watanzania wawili wenye qualification sawa lakini mmoja akawa na command nzuri ya English, mwenye command nzuri ata-excel. Hata hapa viwanja naona tofauti.

Pili watanzania wanapokuwa shule wanakuwa tight sana. Hawajiandai kuwa profession. Wengi wakiwa mashuleni wanasoma kama vile wanataka kuwa academicians.
 
Hivi hao Wakenya wametuzidi nini wabongo hadi wawe wanalipwa mishahara inayotuzidi? Mimi kila siku huku nakutana na Wakenya ambao sioni chochote walichonizidi. Sana sana ni wachovu na washamba na wanaotamani wangekuwa Watanzania. Sielewi kabisa hii ya kuwalipa mishahara iliyotuzidi

My bro, we have to face it. Hata mimi kama nikiwa na kampuni naweza kuajiri wakenya nitaacha watanzania. Hakuna kikubwa walichotuzidi wakenya, lakini kidogo walichotuzidi ni kikubwa sana kwa employers.

Kuna wabongo wavivu sana(wapo wachache wanafanya kazi vizuri sana), they are good at being puctual and attending to work, but they hardly work. Ajabu ni kuwa wanataka mishahara mikubwa. Udokozi ni moja ya sababu ambayo inatuponza sana wabongo, tuna mfano mzuri sana Shoprite, na kwenye mashirika mengi ya Tanzania, na hata serikalini. Tunajiibia hata wenyewe, so that makes it easy kuwaibia wageni.

Lakini tumejitakia sisi wenyewe, nani aliwapa vibali hao wakenya? ni sisi wenyewe? nani amewafanya hao employers wachague wakenya? ni sisi wenyewe.
 
Mpadmire,

Lazima tujiulize kwanza sisi wenyewe, hao Wakenya wanatuzidi nini mpaka walipwe zaidi ya mara tatu ya Watanzania?

Sidhani kama kuna mwajiri ambaye angependa akachukue wakenya na kuwaacha Watanzania wakati skills zao zinafanana.

Kwenye dunia hii ya ushindani ni bora tujiandae na kukuza skills zetu ili tushindane na hao wengine.
Inasikitisha kuona ajira zinazotengenezwa zinaenda kwa wageni huku Watanzania tunaachwa kwenye mataa.
Wametuzidi kwa kingereza! Asilimia kubwa ya watanzania hawajui kingereza fasaha, na wanababaishababaisha sana wakati wa kuongea na kuandika.
Ukiona mtanzania anaongea na mdhungu basi ni yees kwa sana na kuchekacheka hatakama jambo halichekeshi.
Kutokujua kingereza kwa wabongo nadhani kinachangiwa na kuwa na waalimu feki,wanaochaguliwa kujiunga na ualimu ni wale waliofeli form four au six! Kwahiyo tunafundishwa na ma-failures! unategemea nini hapo?
 
Tukirudi kwenye kazi za professional. Kuna kitu watanzania wa-lag behind. Kwanza english kwa watanzania wengi ni second language. Lakini wengi hatutaki ku-improve.

Zakumi, kwani Kiingereza kwa Wakenya sio lugha ya pili au ya tatu? Kama ni hivyo basi hakuna tofauti sana na Watanzania. Hivi umewahi kumsikia raisi wao akiongea Kiingereza? Hata Kikwete ana afadhali!

Still, mimi bado sijashawishika kuwa eti Wakenya wanatuzidi. Mimi kila siku nawaona na sioni lolote spesheli walichonacho. Wanazimia Kiswahili changu na Kiingereza changu cha kubabaisha. Haki ya nani tena Wakenya hawatuzidi kabisa! Tatizo tulilonalo (Watanzania kwa ujumla) labda ni perceptions tu. Perceptions tulizonazo ni kwamba wanatuzidi (supposedly wanaongea kiingereza kizuri-kitu ambacho nakataa) wakati actual reality ni kwamba hawatuzidi lolote.
 
Back
Top Bottom