Baada ya kuona hii thread nimeenda kulisoma hili gazeti na nakukuu "Iwapo hatutatangazwa washindi katika uchaguzi mkuu ujao, Tanzania hapatatosha na tuko tayari kumwaga damu," alinukuliwa akisema kwa msisitizo Mwenyekiti Freeman Mbowe, huku akiungwa mkono na Dk Slaa. Na imeandikwa aliyazungumza September 28 mwaka huu. Kama ni kweli Mbowe alizungumza haya maneno ni vizur akemewe. Sheria ni msumeno na tunaipenda aman ya nchi yetu ndio maana hata Generali Shimbo tulimlalamikia. Kama ni uongo basi akanushe. Au mwenye maelezo alikuwa anamaanisha nini atuweke sawa.
Nimesoma Habari leo! Mwandishi Steven Peter ameanika wazi kuwa Mbowe ndiye aliyetangaza kumwaga damu kama Chadema isingechaguliwa. Nakumbuka Mh Dr Slaa akiwapa changamoto mjeshi amkamate aliyetoa kauli hio lakini Shimbo na wenzie wamejimumunya tu mdomo. Kumbe wanajua nini kilichotokea, najiuliza kwa nini hawakumsikiliza Slaa wakamkamata!?
Lakini jana Mbowe alnusura apate shida kubwa huko kwake Hai, Green Guards walimfanyia vurugu. Sasa nielewe vipi. Steven analalamika kwamba Chadema wamezidi kulalamika.
Ah someni hapa HabariLeo | Chadema uzushi, malalamiko havina tija