Haya ndo mambo ya kudare to talk openly mkuuHALAFU mimi of all the people,hakuna wana jeiefu wanaoniudhi kama wale wanaokuja na post zao mpya wamezi-source huko kwa sijui nani michuzi,mara sijui nani.mara nyingi huwa ni majungu
JuniusInawezekana kuwa JF ni Chadema kwa sababu:
Kuanzia viongozi wa ngazi ya kitaifa hadi mitaa ni wanachama hai na wakudumu wa JF.Hii ni tofauti na vyama vyengine. Na mara nyingi ukisoma katiba ya chadema utakuta falsafa na itikadi zake zinafanana sana tu na za memba vinara wa JF(mfano Mchukia Fisadi {bila ya fitna}) na wenzake.Sababu nyengine hata mijadala inayotokana na mada zinazoisema au kuikosoa chadema inakumbana na "majibu makali" kutoka kwa memba hao na wengine wengi wa JF.
Hata mada ya kawaida tu inayohusu chadema itakuwa na michango meeengi ya wana JF kuonyesha kuwa wanaguswa kwa unywele na ukucha na hali ya chama chao pendwa, mfano mada ya Mh.Zitto na hali ya uchaguzi wa chadema, hii ni tafauti na chaguzi za vyama vingine kama CUF naTLP ambavyo majuzi tu vilikuwa na chaguzi za viongozi wao, hatukuona 'server' ya JF kuzidiwa au vp na 'response' ya memba ilikuwa ndogo as if hakuna linaloendelea katika vyama hivyo.
Circumstencially unaweza kusema kuwa JF ina memba wengi wanachama wa chadema au symphasizers wa chadema au hata si dhambi kusema kuwa wanafafana na mitazamo ya chadema.
Ni mtazamo tu.
Kwanini habari za Chadema tu ndizo zinazotawala hapa? mbona hatuoni vyama vingine? au hotuba za viongozi wengine wa upinzani.