Epuka kutapanya rasilimali fedha, fanya maamuzi mapema ni wapi yatakuwa makazi yako ya kudumu

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,554
Watu wengi hasa wafanyakazi wanaohama hama au kuhamishwa kutoka eneo moja au jingine, wamekuwa wakizeeka na kuchapika sana kimaisha kutokana na kutokuwa na msimamo wa wapi unaishi.

Kuna kada ambazo kuhamishwa ni lazima kama askari, hakimu, wakurugenzi wa halmashauri, DC, DED, DAS , wakuu wa idara etc.

Unakuta mtu kila anakohamishiwa au kuhama, anatamani pori la shamba au kiwanja ananunua na kuacha hapo. Anamwaga tu mawe.

Unakuta miaka inaenda. Familia iko Songea, wewe unafanya kazi Mara na umepanga sababu kila mahali we unanunua viwanja, unaweka mawe na kuhamishwa..Au pengine hata kujenga nyumba.

Swali, ni lini utajitawanya kuishi sehemu zote hizo? Kwanini usiwekeze sehemu moja au mbili vizuri zaidi ili ukija kustaafu urudi huko?

Unastaafu maskini, then umeacha viwanja na mashamba mikoa kibao huko. Muda wa kufanya follow up hauna, umezeeka, familia imechoka, unakufa then unaowaacha wanadhurumiwa!


Amua mapema ni wapi utaishi na familia yako.
 
Bado unaakili ndogo sana kama unafikiri kuwa ukinunua kiwanja au ukijenga na ukahama kiwanja/nyumba inakua haina kazi hizo ni asset mzee na zinakulipa popote nyumba unaweza kupangisha, kiwanja unaweza kuuza.
Alafu pale ulipo ndipo maisha yako yalipo kama unaweza kujenga we jenga, ukianza kuwaza kuhusu kuhama hautakaa ufanye maendeleo yoyote na umri hausimami.
 
Bado unaakili ndogo sana kama unafikiri kuwa ukinunua kiwanja au ukijenga na ukahama kiwanja/nyumba inakua haina kazi hizo ni asset mzee na zinakulipa popote nyumba unaweza kupangisha, kiwanja unaweza kuuza.
Alafu pale ulipo ndipo maisha yako yalipo kama unaweza kujenga we jenga, ukianza kuwaza kuhusu kuhama hautakaa ufanye maendeleo yoyote na umri hausimami.
Hoja yako iko sahihi, ila kumwambia mleta mada ana akili ndogo sana sio sawa, Muombe radhi tafadhali!
 
Bado unaakili ndogo sana kama unafikiri kuwa ukinunua kiwanja au ukijenga na ukahama kiwanja/nyumba inakua haina kazi hizo ni asset mzee na zinakulipa popote nyumba unaweza kupangisha, kiwanja unaweza kuuza.
Alafu pale ulipo ndipo maisha yako yalipo kama unaweza kujenga we jenga, ukianza kuwaza kuhusu kuhama hautakaa ufanye maendeleo yoyote na umri hausimami.
Bado hujamuelewa soma vizuri alicho andika...
 
Bado unaakili ndogo sana kama unafikiri kuwa ukinunua kiwanja au ukijenga na ukahama kiwanja/nyumba inakua haina kazi hizo ni asset mzee na zinakulipa popote nyumba unaweza kupangisha, kiwanja unaweza kuuza.
Alafu pale ulipo ndipo maisha yako yalipo kama unaweza kujenga we jenga, ukianza kuwaza kuhusu kuhama hautakaa ufanye maendeleo yoyote na umri hausimami.
Nakubaliana naye, na nina uzoefu wa hiyo hama hama, the best way ni kuwa na permanent settlement na uwekeze nguvu zote hapo ikiwemo kujenga nyumba yako ya familia (hapo patakuwa HQ), tafuta mashamba kama wewe unapenda kilimo na uyaendekeze, anza maandalizi ya biashara mfano kujenga fremu kadhaa za kukodisha etc Kila ukipata muda wewe au mkeo mnaenda hapo ili hata majirani, nyumba za ibada wawajue, na hata michango na harambee mbalimbali muwe mnashiriki hata mkiwa mbali, hii tunasema mnajijengea social capital na siku mkirudi baada ya kustaafu hamtakuwa wageni na maisha yatakuwa fresh sana. Kwa mfanyakazi na hii mishahara yetu ya kulilia increments na kulalamikia 23% hakuna mwenye ubavu wa kutawanya mapato yake kila mahala, labda uwe ntu wa diliii na mwizi mkubwa huko kazini kwako. Mwisho kumbuka fainali ya mfanyakazi wa umma au sekta binafsi ni pale anapostaafu, na wasema maandalizi ya kustaafu yanatakiwa kuanza siku ya kwanza unapopata ajira kwa kuwekeza kidogokidogo, umeshawahi kusoma kitabu cha Tajiri mkubwa wa Babylon??
 
Nakubaliana naye, na nina uzoefu wa hiyo hama hama, the best way ni kuwa na permanent settlement na uwekeze nguvu zote hapo ikiwemo kujenga nyumba yako ya familia (hapo patakuwa HQ), tafuta mashamba kama wewe unapenda kilimo na uyaendekeze, anza maandalizi ya biashara mfano kujenga fremu kadhaa za kukodisha etc Kila ukipata muda wewe au mkeo mnaenda hapo ili hata majirani, nyumba za ibada wawajue, na hata michango na harambee mbalimbali muwe mnashiriki hata mkiwa mbali, hii tunasema mnajijengea social capital na siku mkirudi baada ya kustaafu hamtakuwa wageni na maisha yatakuwa fresh sana. Kwa mfanyakazi na hii mishahara yetu ya kulilia increments na kulalamikia 23% hakuna mwenye ubavu wa kutawanya mapato yake kila mahala, labda uwe ntu wa diliii na mwizi mkubwa huko kazini kwako. Mwisho kumbuka fainali ya mfanyakazi wa umma au sekta binafsi ni pale anapostaafu, na wasema maandalizi ya kustaafu yanatakiwa kuanza siku ya kwanza unapopata ajira kwa kuwekeza kidogokidogo, umeshawahi kusoma kitabu cha Tajiri mkubwa wa Babylon??
Hama hama, imeniharibia sana..ila mtoa mada amesema ukweli kwa wenye kipato ambacho hatuwezi kuwekeza kila sehemu, tafuta HQ yako hata uende Sudan, pale HQ ndio unafanya maendeleo tu..ikiwa mtu haujapitia hili, hauwezi muelewa mtoa mada.
 
Naona Kuna vijana wanabisha kwakuwa hawajaona,sitotoa experience niliyoiona sababu ya privacy, ila mleta mada yupo sahihi

Unakuja kuwa na nyumba nyingi,zingine kuzifuatilia shida,wapangaji wanachafua ukuta, mashambani vitu vinaibiwa, kwingine unaweka mawe hujengi zaidi hata ya Miaka 15 papo hivo tu

Bora kununua viwanja vingi Mkoa mmoja na mashamba
 
Mimi nadhani kuwekeza katika viwanja/ardhi sio jambo baya. Ardhi inapanda thamani kila kukicha!
 
Naona Kuna vijana wanabisha kwakuwa hawajaona,sitotoa experience niliyoiona sababu ya privacy, ila mleta mada yupo sahihi

Unakuja kuwa na nyumba nyingi,zingine kuzifuatilia shida,wapangaji wanachafua ukuta, mashambani vitu vinaibiwa, kwingine unaweka mawe hujengi zaidi hata ya Miaka 15 papo hivo tu

Bora kununua viwanja vingi Mkoa mmoja na mashamba
Kweli kabisa
 
Bado unaakili ndogo sana kama unafikiri kuwa ukinunua kiwanja au ukijenga na ukahama kiwanja/nyumba inakua haina kazi hizo ni asset mzee na zinakulipa popote nyumba unaweza kupangisha, kiwanja unaweza kuuza.
Alafu pale ulipo ndipo maisha yako yalipo kama unaweza kujenga we jenga, ukianza kuwaza kuhusu kuhama hautakaa ufanye maendeleo yoyote na umri hausimami.
Nadhani wewe ndio hujamuelewa mleta uzi..kasema kwamba chagua mapema eneo ambalo utaishi na kustaafia na endeleza zaidi eneo hilo...kuliko kila mahali unanunua viwanja keho na kesho kutwa unahamishwa..unaenda kuanza upya sehemu nyingine hii ni kutapanya mali..mana usimamizi unaweza kuwa mgumu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Nakubaliana naye, na nina uzoefu wa hiyo hama hama, the best way ni kuwa na permanent settlement na uwekeze nguvu zote hapo ikiwemo kujenga nyumba yako ya familia (hapo patakuwa HQ), tafuta mashamba kama wewe unapenda kilimo na uyaendekeze, anza maandalizi ya biashara mfano kujenga fremu kadhaa za kukodisha etc Kila ukipata muda wewe au mkeo mnaenda hapo ili hata majirani, nyumba za ibada wawajue, na hata michango na harambee mbalimbali muwe mnashiriki hata mkiwa mbali, hii tunasema mnajijengea social capital na siku mkirudi baada ya kustaafu hamtakuwa wageni na maisha yatakuwa fresh sana. Kwa mfanyakazi na hii mishahara yetu ya kulilia increments na kulalamikia 23% hakuna mwenye ubavu wa kutawanya mapato yake kila mahala, labda uwe ntu wa diliii na mwizi mkubwa huko kazini kwako. Mwisho kumbuka fainali ya mfanyakazi wa umma au sekta binafsi ni pale anapostaafu, na wasema maandalizi ya kustaafu yanatakiwa kuanza siku ya kwanza unapopata ajira kwa kuwekeza kidogokidogo, umeshawahi kusoma kitabu cha Tajiri mkubwa wa Babylon??
Imekaa vyema sana hii.


#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom