Epic BSS 2012 Judges - kuweni makini

babykailama

JF-Expert Member
Mar 5, 2012
251
243
Hongera EBSS- 2012

Tunawapongeza kwa maandalizi mazuri na walimu wazuri kama Banana tunamwaminia.

Kazi iko kwa majaji: Ule mchezo wa kubeba baadhi ya watu bila sababu tafadhali sana inakatisha tamaa maana umma unaangalia na kutoa uamuzi. Itakuwa kichekesho sana kama ninyi mnamsifu mtu ambaye hakika anaonekana wazi kuwa hafai aua yuko chini ya kiwango.

Katika kupunguza toka washiriki 21, binafsi niseme wazi kuwa huyu aitwaye SALMA MAHIRI; ana kiwango cha chini maana anapaza tu sauti na mara nyingi yuko nje ya key wala hana X- factor.

Master J, hakukuwa na haja ya kuuma uma na kurudia rudia maneno ukisema, "mimi naona umeimba vizuri, mimi naona umeimba vizuri!!" Hakika walikuwepo wazuri mara 100 katika wale waliorudishwa kuliko huyu. Suala ni sifa ya uwezo wa kuimba, kutumia steji na mwonekano! Pitieni tena video za alipotokea na zaidi hii ya mwisho ya elimination kabla ya kubaki wanaotakiwa na hakika mbele ya malaika zenu Salama, Master J, & Madam Rita mtakubaliana nami kuwa hatujamtendea haki kwa udhaifu wake!!

Pili suala la wapiga vyombo lina utata sana chunguzeni na wanaweza kuwa factor kubwa sana katika kumbeba mtu au kumwangusha mtu!
 
Imeniuma saana kumuodoa rosse mpangala hakika ana kipaji cha hali ya juu kuliko mushi
 
Back
Top Bottom