ELIMU: Gari yenye Cc 650 kutumia mafuta kuliko gari yenye Cc 1300

KIMOMWEMOTORS

JF-Expert Member
May 17, 2018
358
670
Salam kutoka Kimomwe Motors waagizaji wa magari kutoka Japan na Ulaya!

Watanzania tulio wengi tumekua tukiamini na kuaminishana kua gari zenye Cc ndogo kama vile Pajero Mini na Terious Kid hutumia mafuta kidogo zaidi ikilinganishwa na gari zenye Cc zaidi ya 1000. Kwa uzoefu tulio nao katika tasnia hii ya uagizaji wa magari, sehemu kubwa inaonesha kua watanzania wengi wamekua wakizitaka gari hizi kwa kwa maelezo kua zina injini ndogo ambazo hupelekea utumiaji mdogo wa mafuta.

Ukweli ni kua baadhi ya gari hizi kama nilivyozitaja hapo juu hutumia mafuta zaidi ya gari zenye Cc kubwa zaidi. Kwa wastani gari kama Terious Kid na Pajero Mini hutumia mafuta kati ya km14-16 kwa lita, wakati magari mengine kama IST ya Cc 1300, Toyota Tercel, Toyota Cami, Toyota Passo au Toyota Raum hutumia mafuta chini zaidi kiasi cha lita 1 kwa km 15-17.

Ukubwa au udogo wa injini kwa Cc sio kigezo pekee kinachosababisha utumiaji mkubwa au mdogo wa mafuta.

Sababu ya kwanza ya gari kama Pajero Mini na Terious Kid kutumia mafuta mengi zaidi ukilinganisha na gari nyingine nilizotaja haswa kutoka Toyota ni teknolojia. Teknolojia ya mfumo wa mafuta iliyotuika kwenye Mini au Terious Kidi ni ya kizamani ambayo gari hutumia mafuta zaidi katika kujiendesha, wakati hizi gari nyingine hutumia nguvu ya umeme zaidi katika uendeshaji wa gari. Mfano, Toyota Tercel ya mwaka 1996 yenye Cc 1330 huweza kuzalisha kilowati 66 ambayo huweza kuzungusha injini kwa mzunguko wa 5500 rpm, hivyo utaona kua tercel imetumia umeme mwingi zaidi katika kutengeneza mzunguko wa injini wakati Mini au Terious Kid ambazo nyingi zina mfumo wa zamani wa mafuta ujulikanao kama caburator huzalisha 37 kilowati ambayo huzungusha injini kwa mzunguko wa 7500 rpm.

pamoja na hilo la teknolojia, mambo mengine yanayochangia utumiaji mkubwa wa mafuta kwa gari hizi zenye Cc ndogo ni uwepo wa 4while drive ambayo huweka uzito kwenye injini na kufanya matumizi ya mafuta kua juu zaidi. Pia gari nilizotaja hapo juu, nyingi zina Turbo ambayo pia huchangia utumiaji wa mafuta zaidi ingawa pia turbo inapokufa injini hupoteza nguvu yake hali ambayo humuingiza gharama zisizo za lazima mmiliki wa gari hii kwa kutakiwa kufunga turbo nyingine ambapo fundi mzuri atashauri injini nzima ifanyiwe marekebisho ili nguvu yake iendane na turbo mpya.

Wengine hukimbilia gari hizi kwa sababu ya unafuu wa kuziagiza. Ni kweli kuagiza gari hizi Mini na Terious kid kwa wastani ni 7.5m mpaka 8m, lakini gari hizi huja kuwaumiza zaidi kwenye spea na mafuta bila wao wenyewe kufahamu, na wakati utakapotaka kuuza gari ya aina hii kwa wastani sio rahisi kupata mteja aliye tayari kulipa zaidi ya 5m bila kujali imetembea kiasi gani.

Kuna gari nzuri zenye injini za kisasa ambazo hutumia mafuta kidogo japo injini ni zaidi ya Cc 1000, pia spea zake ni nyingi na bei nafuu, na utakapotaka kuuza kwa wastani utaiuza kwa bei nzuri zaidi hivyo pesa yako kutopoteza thamani yake. Gari hizo kwa wastani kuagiza kwake huanzia 8m mpaka 10m.
 

Attachments

  • daihatsu-terios-kid-2003-pics-254400.jpg
    daihatsu-terios-kid-2003-pics-254400.jpg
    193.3 KB · Views: 107
  • Mini Pajero.jpg
    Mini Pajero.jpg
    40 KB · Views: 92
Wewe ndio mpotoshaji mkuu. Hizo kilowatt au bhp ni kipimo cha nguvu ya gari. Haina uhusiano wowote na umeme. Wapotoshaji wengi ndio huwa wanasema eti gari hii au ile umeme umeme mwingi mafuta kidogo.

Gari zote hapo ulizotaja hamna hata moja inayotumia umeme kupata nguvu ya kutembea hizo zinatumia petrol. Umeme unatumika kuendesha mifumo mingine wala sio kusukuma engine.

Gari za umeme ni hybrids ambazo zinahio engine ya petrol na electric motor ambayo inaendesha gari ikiwa mwendo mdogo, ikiwa mwendo mkubwa petrol engine inatake over. Au kuna gari ambazo ni electric kabisa ambazo huwa zinachajiwa betri zake ambapo utaendesha mpaka betri ikikaribia kwisha unachaji tena.

Cc za gari sio sababu pekee ya gari moja kutumia mafuta kuliko ingine ila ulichosema na wewe umepotosha.
 
Mafundi mmekutana! Ila hata mimi nakukubalia hizo point zako, umeme unaozalishwa hauna uhusiano na ulaji wa mafuta zaidi ya kutumika sehemu nyingine.
Mimi nadhani mafuta yanatumika sana kama gari ina mzigo..unaeza kuta kirikuu ya cc650 ikala mafuta kuliko passo ya cc950 kwa sababu kirikuu inabebeshwa mzigo mkubwa au hata body yake ikawa nzito.
Vitu vingine ni balance ya mafuta na hewa. Hakuna kingine, labda iwe inatumia vyote umeme na petrol consecutively! Mleta mada kaja kufanya promo ya kuagiza magari au kutapeli watu akijifanya anaagizia watu magari.....mwizi mkubwa!
Wewe ndio mpotoshaji mkuu. Hizo kilowatt au bhp ni kipimo cha nguvu ya gari. Haina uhusiano wowote na umeme. Wapotoshaji wengi ndio huwa wanasema eti gari hii au ile umeme umeme mwingi mafuta kidogo.

Gari zote hapo ulizotaja hamna hata moja inayotumia umeme kupata nguvu ya kutembea hizo zinatumia petrol. Umeme unatumika kuendesha mifumo mingine wala sio kusukuma engine.

Gari za umeme ni hybrids ambazo zinahio engine ya petrol na electric motor ambayo inaendesha gari ikiwa mwendo mdogo, ikiwa mwendo mkubwa petrol engine inatake over. Au kuna gari ambazo ni electric kabisa ambazo huwa zinachajiwa betri zake ambapo utaendesha mpaka betri ikikaribia kwisha unachaji tena.

Cc za gari sio sababu pekee ya gari moja kutumia mafuta kuliko ingine ila ulichosema na wewe umepotosha.
 
Wewe ndio mpotoshaji mkuu. Hizo kilowatt au bhp ni kipimo cha nguvu ya gari. Haina uhusiano wowote na umeme. Wapotoshaji wengi ndio huwa wanasema eti gari hii au ile umeme umeme mwingi mafuta kidogo.

Gari zote hapo ulizotaja hamna hata moja inayotumia umeme kupata nguvu ya kutembea hizo zinatumia petrol. Umeme unatumika kuendesha mifumo mingine wala sio kusukuma engine.

Gari za umeme ni hybrids ambazo zinahio engine ya petrol na electric motor ambayo inaendesha gari ikiwa mwendo mdogo, ikiwa mwendo mkubwa petrol engine inatake over. Au kuna gari ambazo ni electric kabisa ambazo huwa zinachajiwa betri zake ambapo utaendesha mpaka betri ikikaribia kwisha unachaji tena.

Cc za gari sio sababu pekee ya gari moja kutumia mafuta kuliko ingine ila ulichosema na wewe umepotosha.
Haa, mi nikifikiri anaongelea teknolojia ya hybrid, yaani engine inasaidiana na motor, hivyo ukipiga brake ile nguvuvinageuzwa kuwa umeme na kuchaji betri, kumbe sio?
 
The Jeeps were never meant to be fuel efficient!
Pamoja na kwamba Mini yenye 650cc inakula sana wese kuliko Vitz yenye 1000cc, the road handling ya Mini ni kubwa sana. There is a reason why it was called Pajero...
 
Wewe ndio mpotoshaji mkuu. Hizo kilowatt au bhp ni kipimo cha nguvu ya gari. Haina uhusiano wowote na umeme. Wapotoshaji wengi ndio huwa wanasema eti gari hii au ile umeme umeme mwingi mafuta kidogo.

Gari zote hapo ulizotaja hamna hata moja inayotumia umeme kupata nguvu ya kutembea hizo zinatumia petrol. Umeme unatumika kuendesha mifumo mingine wala sio kusukuma engine.

Gari za umeme ni hybrids ambazo zinahio engine ya petrol na electric motor ambayo inaendesha gari ikiwa mwendo mdogo, ikiwa mwendo mkubwa petrol engine inatake over. Au kuna gari ambazo ni electric kabisa ambazo huwa zinachajiwa betri zake ambapo utaendesha mpaka betri ikikaribia kwisha unachaji tena.

Cc za gari sio sababu pekee ya gari moja kutumia mafuta kuliko ingine ila ulichosema na wewe umepotosha.
Je ni kweli cc ndogo inakula mafuta kidogo?
 
Mafundi mmekutana! Ila hata mimi nakukubalia hizo point zako, umeme unaozalishwa hauna uhusiano na ulaji wa mafuta zaidi ya kutumika sehemu nyingine.
Mimi nadhani mafuta yanatumika sana kama gari ina mzigo..unaeza kuta kirikuu ya cc650 ikala mafuta kuliko passo ya cc950 kwa sababu kirikuu inabebeshwa mzigo mkubwa au hata body yake ikawa nzito.
Vitu vingine ni balance ya mafuta na hewa. Hakuna kingine, labda iwe inatumia vyote umeme na petrol consecutively! Mleta mada kaja kufanya promo ya kuagiza magari au kutapeli watu akijifanya anaagizia watu magari.....mwizi mkubwa!
Haya halafu urudi Kule kwenye Uzi wako wa mabasi ya mkoani yenye a/c unahitajika haraka sana
 
Kwa wastani gari kama Terious Kid na Pajero Mini hutumia mafuta kati ya km15-17, wakati magari mengine kama IST ya Cc 1300, Toyota Tercel, Toyota Cami, Toyota Passo au Toyota Raum hutumia mafuta chini zaidi.
Kuna gari nzuri zenye injini za kisasa ambazo hutumia mafuta kidogo japo injini ni zaidi ya Cc 1000, pia spea zake ni nyingi na bei nafuu, na utakapotaka kuuza kwa wastani utaiuza kwa bei nzuri zaidi hivyo pesa yako kutopoteza thamani yake.
Gari zipi hizo ingefaa uzitaje waliokuwa hawajui wazijue!..
 
Back
Top Bottom