Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Hayati Moringe alikuwa halali, kila siku alihakikisha anapambana vikali na walanguzi pamoja na wahujumu uchumi. Alikuwa ni kati ya mawaziri wakuu bora kabisa. Ngoyae naye akiwa na wadhifa huohuo alihakikisha anapambana na viongozi wazembe kwa nguvu zake pamoja na kuhimiza bidii katika kulijenga taifa.
Moringe alifariki kwa ajali ya gari kabla ya kutimiza ndoto yake ya kuwafyeka wahujumu, Ngoyae yeye alijiuzulu kwa kutwishwa zigo la dhambi za watu wengine ili kupitia yeye waokoke na kuingia katika ufalme wa milele.
Wajuvi wa mambo walitabiri kuwa Moringe ndiye angekuwa mrithi wa Julius wakati wadadisi wa mambo wanaamini kuwa Ngoyae ndiye atakuwa mrithi wa kiti cha Mrisho.
Haya ni maoni, watukanaji watukane! Wenye akili timamu wanakaribishwa sana.
Moringe alifariki kwa ajali ya gari kabla ya kutimiza ndoto yake ya kuwafyeka wahujumu, Ngoyae yeye alijiuzulu kwa kutwishwa zigo la dhambi za watu wengine ili kupitia yeye waokoke na kuingia katika ufalme wa milele.
Wajuvi wa mambo walitabiri kuwa Moringe ndiye angekuwa mrithi wa Julius wakati wadadisi wa mambo wanaamini kuwa Ngoyae ndiye atakuwa mrithi wa kiti cha Mrisho.
Haya ni maoni, watukanaji watukane! Wenye akili timamu wanakaribishwa sana.