Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Salim Said
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema kitendo cha Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kuendelea kuwalazimisha Wazanzibari kwenda vituoni ili kuandikishwa hadi katika sikukuu za kitaifa, ni kuvunja katiba na sheria ya nchi na kwamba kutokana na hali hiyo, uchaguzi utakuwa batili.
CUF imelezimika kutoa kauli hiyo baada ya ZEC kuamua jana kufungua vituo vya kuboresha daftari la kudumu la wapigakura katika visiwa vya Unguja na Pemba hapo huku ikijua kwamba juzi na jana ilikuwa ni sikukuu ya kitaifa ya dini ya kiislaam.
Akizungumza na Mwananchi jana, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar Juma Duni Haji alisema kitendo cha ZEC kufungua vituo hadi siku za sikukuu za dini, ni ishara ya kutapatapa
Duni ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchumi na Fedha wa chama hicho, alisema kitendo hicho cha kuwataka wananchi kwenda vituoni kujiandikisha siku ya Idd ni dhambi hata kwa mwenyezi Mungu.
Alisema katiba ya nchi inatoa uhuru wa kuabudu na kwamba sheria ya maadhimisho nchini inatoa uhuru wa kusheherekea sikukuu za kidini ambazo pia ni sehemu ya ibada.
"Kwa kweli kuwafanyisha watu kazi sikukuu si haki na dhambi hata kwa Mwenyezi Mungu. Lakini ZEC wanafanya hivyo makusudi na ni ishara ya kutapatapa kwao ili kutimiza malengo yao waliyojiwekea.
"Hata kikatiba na kisheria tayari umeshaingilia uhuru wa kuabudu wa watanzania jambo ambalo halikubaliki," alisema Duni.
Duni alisema kitendo hicho si halali na wala si haki kwa sababu asilimia kubwa ya Wazanzibari ni waislaam na wanahitaji muda huo wa mapumziko ili kutembeleana na kupumzika na familia zao. katika kutimiza malengo yao.
"Kidini si halali na kikatiba kwani imevunjwa na sheria imekiukwa na hivyo utaratibu huo si halali kwa wananchi na wananchi wamenyimwa haki ya kuabudu," alisema Duni.
Hivi karibuni Katibu Mkuu wa CUF maalim Seif Sharif Hamad aliandikia barua ZEC akiitaka kusogeza mbele daftari hilo hadi hapo mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na sikukuu zake.
Duni alisema Katiba ya Zanzibar imevunjwa na sheria ya uchaguzi ya Zanzibar ni batili na kwamba hata uchaguzi utakaofanyika visiwani 2010 utakuwa batili!
"Katiba imevunjwa na sheria ya uchaguzi ni batili na kwa mantiki hiyo hata uchaguzi wowote utakaofanyika kwa kutumia sheria hiyo utakuwa batili tu,"alidai Duni.
Aliitaka ZEC kusitisha mara moja uandaaji wa daftari hilo na kuitaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kuhakikisha kwamba, inatoa vitambulisho vya Mzanzibari Mkazi (Zan ID) kwa wazanzibari wote wenye sifa.
Mkurugenzi wa Zec Salum Kassim akizungumzia tume yake kuamua kufungua vituo vya kuandikisha wakati wa sikukuu za Idd el Fitri, alisema vituo hivyo vimefunguliwa licha ya juzi kuwa ni sikukuu ya Idd El Fitir. "Vituo viko wazi hivi sasa, lakini mimi siwezi kukujibu lolote kwa sababu leo ni siku ya mapumziko ya kitaifa, nipigie kesho nitakueleza," alisema Kassim.
Source: http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=14778
My take:
1. Hivi Duni na Maalim Seif ni viongozi wa kidini na siasa at the same time?
2. Na hao wananchi walilazimishwaje kwenda kwenye vituo vya kujiandikisha?
3. Kama wananchi wangekaa nyumbani au kuwatembelea marafiki kuna mtu angekuja kuwatoa nyumbani kwenda kujiandikisha?
4. Mbona chaguzi mbalimbali zimewahi kufanyika Jumapili au Jumamosi ambazo ni siku za mapumziko na hawajawahi kutoa tamko la kuvunjwa kwa Katiba au sheria nyingine yoyote? Au kwa sababu wao sio Wakristo?
5. Mbona kama vile wanachukua pre-emptive action inayolenga uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kama anavyofanyaga Lipumba kuwahi kutangaza matokeo kabla ya Tume ya Uchanguzi kutangaza ili kutafuta public sympathy?
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema kitendo cha Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kuendelea kuwalazimisha Wazanzibari kwenda vituoni ili kuandikishwa hadi katika sikukuu za kitaifa, ni kuvunja katiba na sheria ya nchi na kwamba kutokana na hali hiyo, uchaguzi utakuwa batili.
CUF imelezimika kutoa kauli hiyo baada ya ZEC kuamua jana kufungua vituo vya kuboresha daftari la kudumu la wapigakura katika visiwa vya Unguja na Pemba hapo huku ikijua kwamba juzi na jana ilikuwa ni sikukuu ya kitaifa ya dini ya kiislaam.
Akizungumza na Mwananchi jana, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar Juma Duni Haji alisema kitendo cha ZEC kufungua vituo hadi siku za sikukuu za dini, ni ishara ya kutapatapa
Duni ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchumi na Fedha wa chama hicho, alisema kitendo hicho cha kuwataka wananchi kwenda vituoni kujiandikisha siku ya Idd ni dhambi hata kwa mwenyezi Mungu.
Alisema katiba ya nchi inatoa uhuru wa kuabudu na kwamba sheria ya maadhimisho nchini inatoa uhuru wa kusheherekea sikukuu za kidini ambazo pia ni sehemu ya ibada.
"Kwa kweli kuwafanyisha watu kazi sikukuu si haki na dhambi hata kwa Mwenyezi Mungu. Lakini ZEC wanafanya hivyo makusudi na ni ishara ya kutapatapa kwao ili kutimiza malengo yao waliyojiwekea.
"Hata kikatiba na kisheria tayari umeshaingilia uhuru wa kuabudu wa watanzania jambo ambalo halikubaliki," alisema Duni.
Duni alisema kitendo hicho si halali na wala si haki kwa sababu asilimia kubwa ya Wazanzibari ni waislaam na wanahitaji muda huo wa mapumziko ili kutembeleana na kupumzika na familia zao. katika kutimiza malengo yao.
"Kidini si halali na kikatiba kwani imevunjwa na sheria imekiukwa na hivyo utaratibu huo si halali kwa wananchi na wananchi wamenyimwa haki ya kuabudu," alisema Duni.
Hivi karibuni Katibu Mkuu wa CUF maalim Seif Sharif Hamad aliandikia barua ZEC akiitaka kusogeza mbele daftari hilo hadi hapo mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na sikukuu zake.
Duni alisema Katiba ya Zanzibar imevunjwa na sheria ya uchaguzi ya Zanzibar ni batili na kwamba hata uchaguzi utakaofanyika visiwani 2010 utakuwa batili!
"Katiba imevunjwa na sheria ya uchaguzi ni batili na kwa mantiki hiyo hata uchaguzi wowote utakaofanyika kwa kutumia sheria hiyo utakuwa batili tu,"alidai Duni.
Aliitaka ZEC kusitisha mara moja uandaaji wa daftari hilo na kuitaka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kuhakikisha kwamba, inatoa vitambulisho vya Mzanzibari Mkazi (Zan ID) kwa wazanzibari wote wenye sifa.
Mkurugenzi wa Zec Salum Kassim akizungumzia tume yake kuamua kufungua vituo vya kuandikisha wakati wa sikukuu za Idd el Fitri, alisema vituo hivyo vimefunguliwa licha ya juzi kuwa ni sikukuu ya Idd El Fitir. "Vituo viko wazi hivi sasa, lakini mimi siwezi kukujibu lolote kwa sababu leo ni siku ya mapumziko ya kitaifa, nipigie kesho nitakueleza," alisema Kassim.
Source: http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=14778
My take:
1. Hivi Duni na Maalim Seif ni viongozi wa kidini na siasa at the same time?
2. Na hao wananchi walilazimishwaje kwenda kwenye vituo vya kujiandikisha?
3. Kama wananchi wangekaa nyumbani au kuwatembelea marafiki kuna mtu angekuja kuwatoa nyumbani kwenda kujiandikisha?
4. Mbona chaguzi mbalimbali zimewahi kufanyika Jumapili au Jumamosi ambazo ni siku za mapumziko na hawajawahi kutoa tamko la kuvunjwa kwa Katiba au sheria nyingine yoyote? Au kwa sababu wao sio Wakristo?
5. Mbona kama vile wanachukua pre-emptive action inayolenga uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kama anavyofanyaga Lipumba kuwahi kutangaza matokeo kabla ya Tume ya Uchanguzi kutangaza ili kutafuta public sympathy?
Last edited: