Lumbi9
JF-Expert Member
- Oct 12, 2014
- 8,566
- 11,809
Sehemu ya kwanza
Kwa Mary Robert.2010
Nayajua mengi kwakuwa nimempa kila mtu nafasi ya kuwa mwalimu wangu,,kila mtu hunifunza kwa
yale atakayo,,naheshimu kauli na mawazo ya wote kwa uzito sawa, LAKINI UELEWA NI JUU YANGU
MTANGAZAJI
Leo katika kipindi chetu, tutaendelea kusikiliza
mahojiano kati ya Patrick na mwandishi wa habari
waliowahi kuyafanya kipindi cha nyuma kabla ya
leo, tulia kwenye redio yako na kila kitu kitakujia
hapohapo ulipo, hatutakuwa na matangazo mengi
kutokana na uzito wa simulizi hii ya kusisimua
ilikuwa ni sauti ya mtangazaji wa kituo cha redio
cha SPEAK LOUD FM kilichokuwa kikirusha kipindi
cha STORY za Iam Frank, saa yangu ya mkononi ilinionyesha kuwa ilikuwa saa nne usiku na pombe
zilikuwa zimeivuruga akili yangu, lakini nilikwenda
mpaka kwenye jokofu na kuchukua Redbul kisha niliinywa haraka haraka na kurudi ili niweze
kusikiliza bila kupata chembe ya usingiziile kanda
yenye ile simulizi ilichezeshwa na sauti ya msimuliaji ilianza
kusikika.
PATRICK ANASIMULIA
".........ulifikiri nitanyamaza sio,sikutaka kufanya
yote haya ila you forced my hand(uliulazimisha
mkono wangu).."ndo sauti ya mwisho niliyoisikia katika masikio yangu ikifuatiwa na maumivu ya
kitu chenye ncha kilichoingizwa kwenye mshipa wa damu kichwani mwangu,niligundua ni sindano
baada ya kuhisi kama dawa ikisukumwa kuingia ndani ya mshipa ule, hali ya kulewa na usingizi vilianza kunisonga lakini kwa mbali niliweza kuona kama vile Mary alikuwa amezimia, nikajitahidi
kutoa sauti lakini sikuweza kabisa, wale watu sikuwaona vizuri lakini walikuwa ni zaidi ya wawili
kwakuwa nilizisikia sauti zao kwa mbali wakishauriana, sikuifahamu hata sauti moja, gari
letu lilikuwa limeharibika vibaya na ile ajali,sikumbuki ilikuwaje mpaka tukagongana na ile gari
ila nilishtuka tu na kukuta tayari ajali imetokea na wale waliokuwa kwenye ile gari ndio walioshuka na
kuja kunichoma ile sindano. Maumivu makali yaliutesa moyo wangu haswa pale nilipotaka kukumbuka hata jina langu lakini nikashindwa,,,sikukumbuka kitu chochote, niliishi maisha ya tabu
sana katika siku za ukubwa wangu, kila kitu kwenye maisha yangu kilikuwa kipya kabisa,sikumfahamu yeyote katika eneo lile. Sikukumbuka
nilipokuwa wala nilifikaje,sikufahamu chochote
kuhusu ulimwengu,kila kitu kilikuwa ni giza ndani ya maisha yangu,sikutamani kufa kwasababu
sikujua nini maana ya kuishi na nini faida ya kufa kwa wakati huo,,kwa kweli yalikuwa maisha ambayo sikuwahi kufikiri kama ningeishi. Miaka sita mbeleni nilikuja kutoka nje na ndipo nilipoona bango kubwa nje ya jengo hilo nililokuwemo bango
hilo lilisomeka Dr. ANDERSON MENTAL CLINIC,ilikuwa pia anuani chini yake iliyonijulisha kuwa
nilikuwa SUVA huko FIJI, mandhari niliyokuwepo niliipenda sana ila sikukumbuka chochote juu ya
eneo hilo,niliichukia sana hali niliyokuwa nayo wakati ule, hakuna aliyekuwa akionekana kunijali,kila mtu alikuwa busy na kazi yake.
Nilijihisi pengine nilikuwa kichaa, iweje kila mtu asinijali au kuniuliza chochote pale nilipokuwa.
Hayo yalikuwa maisha yangu kipindi cha mwanzoni mwa uzima wangu wagu wa mara ya pili, niliona watu ambao nilihisi ni tofauti sana na mimi,,,,,nilisogea mpaka mbele kwenye bustani kubwa na kutazama mbele mita 200 nikagundua pale ni
karibu kabisa na ufukwe wa bahari.
****
"hallo,,!"niliskia sauti ikiniita wakati nipo pale kwenye bustani nikageuka,alikuwa ni msichana
mwenye asili kama yangu lakini sikuwa namfahamu,,alinisogelea karibu nakuanza kunisemesha,nilielewa lugha aliyokuwa akiiongea,
niliwahi kuwa nikiiongea sehemu fulani lakini sikukumbuka ni wapi.
Patrick namshukuru sana mungu uko hai,nashukuru umerudisha fahamu zako aliongea huku akionekana kweli kuwa alikuwa akilifurahia hilo.
Sikumjua huyu dada wala sikufahamu yeye amenijuaje.
utapona kabisa na utakumbuka kila kitu,tunafanya tuwezavyo kuhakikisha kuwa unarudisha fahamu zako alizidi kusisitiza huku akifuta machozi.
wewe ni nani nilimuuliza huku nikimtazama usoni,hakika sura yake sikuijua kabisa, hata kama sikuwa na fahamu lakini sura yake ni kweli
sikuwahi kuiona hata kidogo.
Naitwa Pamela, ndiye daktari ninayemsaidia dokta Anderson katika matibabu yako, ni mimi ambaye
ndiye nakuwa na wewe muda wote kuangalia afya yako, wewe ni sababu ya mimi kuendelea kuwa hapa aliongea huku akionekana kuangalia pembeni kana kwamba alikuwa akifuta machozi.
kwanini unalia nilimuuliza huku nikimgeuza ili aniangalie.
silii, ni furaha tu kwakuwa umeamka leo kichwa changu kilikuwa kimejaa maswali mengi sana,lakini sikujua namna ya kuyauliza, kila kitu pale
kilikuwa ni michoro kwangu isiyoashiria chochote,
nilikuwa nimevurugwa akili na kila kitu kabisa,sikumfahamu yule Pamela na wala sikujua yeye ninani, sikujua anaposema nimeamka je nililala toka
lini, na kwanini kuamka kwangu kuwe ni furaha kwake, kwanini alie kwa mimi kuamka, kwanini alionyesha furaha na kusema nitapona, yeye
alikuwa nani kwangu, mimi nilikuwa na thamani gani kwake, hiyo yote ilikuwa ni jakamoyo ndani ya
moyo wangu, nilikuwa kama teja lililokuwa likihudhuria kliniki ya ukichaa.
Pamela, mimi sielewi chochote nilimuuliza huku nikilia baada ya kujitahidi sana kukumbuka lakini
ikashindikana. Hakunijibu chochote badala yake alinishika mkono na kuondoka na mimi mpaka
ndani ya ile hospitali. Tulipofika pale aliingia ndani na kutoka na daktari mmoja mzungu aliyekuja pale
na kuanza kuongea na mimi kisha Pamela alikuwa akinitafsiria.
Hellow Patrick am doctor Anderson(habari
Patrick, naitwa dokta Anderson). Alinisalimu na kunipa mkono, na mimi nilimpa mkono.
We want to discharge you, but you will be under the care of doctor Pamela, you will stay at her
place until we are sure that you can stand on your own(tunataka tukuruhusu lakini utakuwa chini ya
uangalizi wa dokta Pamela, utakaa nyumbani kwake hadi tutakapokuwa na uhakika kuwa kuwa unaweza kujitegemea) sauti ya Pamela ilisikika ikitafsiri maneno ya dokta Anderson.
Pamela dont bother to interpret, I do understand the language (Pamela usihangaike kutafsiri,
naielewa hiyo lugha), nilimuambia hayo Pamela na yeye alinyamaza kimya.
*********
Niliruhusiwa kutoka pale hospitali na sasa tuliingia kwenye gari ya dokta Pamela kuelekea kwake,
hapakuwa mbali sana na pale hospitali, muda wa dakika kumi tulikuwa tumeshafika.
karibu sana Patrick, hapa ni nyumbani kwangu,ndiko ninapoishi, na ndipo ambapo na wewe utaishi alinikaribisha huku akitabasamu na
kuruhusu vishimo vidogo kwenye mashavu yake vionekane, nilikaribia na kuketi huku nikitazama kila kona ya ile nyumba. Ilikuwa ni nyumba ndogo lakini ilikuwa ni nzuri na ilikuwa na mazingira mazuri yaliyovutia.
Unaishi na nani hapa nilimuuliza swali wakati alipokuwa akienda kuchukua kinywaji kwenye jokofu.
naishi mwenyewe, lakini kwasasa nitakuwa nikiishi na Patrick aliongea hayo na kucheka.
Sikumbuki kama niliwahi kucheka toka pale hospitali. Kwa muda mfupi niliokuwa na Pamela nilikuwa nimegundua kuwa alikuwa mtu mwenye
kupenda sana kucheka, alikuwa ni mtu mcheshi na anayependa utani muda mwingi. Nilianza maisha haya ya kuishi kwa Pamela na muda mwingi dokta Anderson alikuwa akija pale nyumbani kuniangalia.
Pamela na dokta Anderson walikuwa kama ndugu vile ingawaje Pamela alikuwa na asili tofautikidogo.
***********
Asubuhi tulivu ya desemba 1999 ilinikuta nikiwa Suva huko Fiji, ilikuwa ni miezi mitatu sasa toka
nitoke hospitali lakini mpaka wakati huo bado sikujua chochote, mbali na kumuuliza Pamela maswali mengi lakini hakuwa tayari kabisa
kunieleza chochote, siku zote historia ya maisha
yangu na sababu za kwanini sina kumbukumbu yeye hakuziona za maana.
Patrick leo tunatoka nilimsikia Pamela akinipa taarifa hiyo asubuhi wakati alipokuja kugonga chumba changu.
tunaenda wapi nilimuuliza huku nijiachanisha na shuka zito nililokuwa nimejifunika.
tunaenda Albert Park, amka ujiandae tunaondoka muda sio mrefu niliamka na kuanza kujiandaa.
***********
Safari ya kuelekea Albert Park ilianza, tulikwenda mpaka Tanoa plaza tukipitia Amy Roas na hapo
tulisimama, kisha Pamela aliniambia tushuke tuingie ndani ya lile jengo. Tuliingia mpaka ndani ya jengo lile na kwenda upande wakulia mpaka juu
kabisa ambapo tuliweza kuona mandhari yote ya
Fiji na kwambali alinionyesha nchi ya Australia.
Nikiwa pale juu nilisikia kama sauti yamsichana ikiniita na nilipogeuka nyuma sikuona mtu.
ni nini Patrick aliniuliza Pamela lakini sikuwa na la kumjibu, nilipokuwa nimegeuka sikumuona mtu
yoyote lakini kwa uhakika kabisa niliona kama kivuli cha msichana niliyehisi kumfahamu, najua
hata ningesema Pamela asingenielewa.
hamna kitu, sijui ni nini nimeona nilimueleza hayo na yeye alinifata na kunishika kichwa akiniambia
kuwa amenileta pale kwasababu japo hakunieleza ni sababu gani hiyo. Alitnitoa pale na kunipeleka
ndani zaidi kwenye chumba fulani na hapo nilianza kuhisi mapigo ya moyo yakinienda mbio.
Pamela kuna nini hapa nilimuuliza Pamela lakini hakuniambia kitu badala yake alinifunga kitambaa
usoni na kuniambia niketi, niliketi huku nikiwa na wasiwasi juu ya kilichokuwa kikitokea pale. Giza
lilikuwa limetanda kwenye macho yangu na hofu ilinifika. Nilianza kuona picha ya msichana kwa
mbali na sikujua ni nani. Alikuwa msichana mrembo mweupe ambaye nilikuwa naye sehemu kama ufukweni mwa bahari, yule msichana alikuwa
akifurahi na mimi nilikuwa nikimkumbatia kama vile tulikuwa wapenzi,,niliogopa sana kwakuwa
haikuwa kawaida, alinifungua tena kile kitambaa na kuniuliza nimeona nini lakini sikuwa na la kumjibu.
mimi ni nani Pamela? nilimuuliza huku nikiwa kama natetemeka, alinitazama machoni huku akionekana kuzuia machozi.
ukitaka kujua wewe ni nani lazima uwe makini na kile kikujiacho kwenye fikra zako aliniambia
nakuninyanyua kisha tulienda mpaka kwenye chumba kilichokuwa kulekule ndani kisha alivua nguo zake mbele yangu na kuvaa taulo na
kuelekea bafuni, akiwa bafuni nilisikia akiniita lakini
kwa uwoga nilivua nguo zangu na kuvaa taulo kisha nikamfata bafuni, nilipoingia alinikumbatia na
kuanza kunipiga mabusu mwili mzima, mihemko ya mwili wangu ilikuwa karibu kabisa na hisia zangu hivyo nilianza kulipiza mashambulizi, kila
nilipokuwa nikimshika kuna picha ya mwanamke ilikuwa ikinijia, tulitoana bafuni na kuja mpaka kitandania kisha kazi ilianza pale, Pamela alikuwa mtundu sana kitandani lakini kila alipojitahidi kunifanyia mambo flani taswira ya mwanamke
mwingine ilikuwa ikinijia, tuliendelea kusumbuana na kuchokozana hisia zetu na mwishowe
tulikutanisha maungo yetu ya uzazi, nilipokuwa katikati ya mchezo wakati Pamela akiwa juu kuongoza jahazi niliona sura ya yule msichana
tena na kushtuka ana hapo Pamela alizidisha kasi,nilikuwa kama mtoto mdogo vile jinsi ambavyo
nilikuwa nikilia na ile sura ya yule mwanamke ilikuwa ikinijia bado.
Mary,,,Mary nilijikuta nikitamka lile jina na hapo Pamela aliacha na kunishika kichwa,,kisha alikuwa
akiniangalia kwa makini.
kafanyaje aliniuliza kama vile hakuelewa ninachomaanisha, nilinyamaza kwakuwa sikujua
namna ya kuendelea kuelezea, hapo Pamela alianza tena kuushika mwili wangu na kuendelea
na shughulia yake mpaka nilipokumbuka baadhi ya vitu.
Mary ni nani Pamela nilimuuliza kisha alinyanyuka vilevile akiwa uchi na kuondoka kuelekea bafuni, alipokuwa akiondoka nilimtizama
na ile picha ilinijia tena. Nilijivuta pale kitandani na
kwenda kumfata kule bafuni, alifungua lile bomba la mvua na kunivuta kisha alinikumbatia huku maji yakitumwagikia. Nilikuwa nimetumbua macho na
yeye hakuwa anaongea zaidi ya kufungwa macho akiyaruhusu maji yazilowanishe nywele zake laini.
*****
USIKU WA SIKU HIYO.
Tulikuwa tumelala nyumbani kwa Pamela na siku hiyo ilikuwa mara ya kwanza mimi na Pamela
kufanya yote yaliyotokea mchana huo.
Mary ni nani lilikuwa swali la kwanza kumuuliza Pamela usiku ule. Alikuwa amenilalia kifuani lakini
nilipomuuliza alinyanyuka na kuketi.
Mary ni msichana uliyekuja naye Fiji miaka zaidi ya sita sasa, ni mke wako na alikaa hapa akikuuguza kwa zaidi ya miezi sita ila baadaye
aliamua kuondoka baada ya kumwambia kuwa si rahisi wewe kurudisha fahamu tena, aliondoka na
hatukujua ni wapi alikwenda, tumejaribu sana kutafuta kumbukumbu zako lakini hatukupata
alinieleza hiku akijikaza ili asilie.
kwanini sikuwa na fahamu nilimuuliza.
ulichomwa sindano ya dicomenzol, inayotumiwa kuchoma wanyama wakali ili kuwafanya watulie,
walikuchoma wakazidisha kipimo na hii ilikuwa ni baada ya wewe kupata ajali ambayo hata hivyo tunahisi ilikuwa ni ya kukusudiwa, yani kuna mtu aliitengeneza ili itokee ndo wakuchome sindano ile ambayo ilimaliza kila kitu kichwani mwako
Mary Robertnilikumbuka.
Kwa Mary Robert.2010
Nayajua mengi kwakuwa nimempa kila mtu nafasi ya kuwa mwalimu wangu,,kila mtu hunifunza kwa
yale atakayo,,naheshimu kauli na mawazo ya wote kwa uzito sawa, LAKINI UELEWA NI JUU YANGU
MTANGAZAJI
Leo katika kipindi chetu, tutaendelea kusikiliza
mahojiano kati ya Patrick na mwandishi wa habari
waliowahi kuyafanya kipindi cha nyuma kabla ya
leo, tulia kwenye redio yako na kila kitu kitakujia
hapohapo ulipo, hatutakuwa na matangazo mengi
kutokana na uzito wa simulizi hii ya kusisimua
ilikuwa ni sauti ya mtangazaji wa kituo cha redio
cha SPEAK LOUD FM kilichokuwa kikirusha kipindi
cha STORY za Iam Frank, saa yangu ya mkononi ilinionyesha kuwa ilikuwa saa nne usiku na pombe
zilikuwa zimeivuruga akili yangu, lakini nilikwenda
mpaka kwenye jokofu na kuchukua Redbul kisha niliinywa haraka haraka na kurudi ili niweze
kusikiliza bila kupata chembe ya usingiziile kanda
yenye ile simulizi ilichezeshwa na sauti ya msimuliaji ilianza
kusikika.
PATRICK ANASIMULIA
".........ulifikiri nitanyamaza sio,sikutaka kufanya
yote haya ila you forced my hand(uliulazimisha
mkono wangu).."ndo sauti ya mwisho niliyoisikia katika masikio yangu ikifuatiwa na maumivu ya
kitu chenye ncha kilichoingizwa kwenye mshipa wa damu kichwani mwangu,niligundua ni sindano
baada ya kuhisi kama dawa ikisukumwa kuingia ndani ya mshipa ule, hali ya kulewa na usingizi vilianza kunisonga lakini kwa mbali niliweza kuona kama vile Mary alikuwa amezimia, nikajitahidi
kutoa sauti lakini sikuweza kabisa, wale watu sikuwaona vizuri lakini walikuwa ni zaidi ya wawili
kwakuwa nilizisikia sauti zao kwa mbali wakishauriana, sikuifahamu hata sauti moja, gari
letu lilikuwa limeharibika vibaya na ile ajali,sikumbuki ilikuwaje mpaka tukagongana na ile gari
ila nilishtuka tu na kukuta tayari ajali imetokea na wale waliokuwa kwenye ile gari ndio walioshuka na
kuja kunichoma ile sindano. Maumivu makali yaliutesa moyo wangu haswa pale nilipotaka kukumbuka hata jina langu lakini nikashindwa,,,sikukumbuka kitu chochote, niliishi maisha ya tabu
sana katika siku za ukubwa wangu, kila kitu kwenye maisha yangu kilikuwa kipya kabisa,sikumfahamu yeyote katika eneo lile. Sikukumbuka
nilipokuwa wala nilifikaje,sikufahamu chochote
kuhusu ulimwengu,kila kitu kilikuwa ni giza ndani ya maisha yangu,sikutamani kufa kwasababu
sikujua nini maana ya kuishi na nini faida ya kufa kwa wakati huo,,kwa kweli yalikuwa maisha ambayo sikuwahi kufikiri kama ningeishi. Miaka sita mbeleni nilikuja kutoka nje na ndipo nilipoona bango kubwa nje ya jengo hilo nililokuwemo bango
hilo lilisomeka Dr. ANDERSON MENTAL CLINIC,ilikuwa pia anuani chini yake iliyonijulisha kuwa
nilikuwa SUVA huko FIJI, mandhari niliyokuwepo niliipenda sana ila sikukumbuka chochote juu ya
eneo hilo,niliichukia sana hali niliyokuwa nayo wakati ule, hakuna aliyekuwa akionekana kunijali,kila mtu alikuwa busy na kazi yake.
Nilijihisi pengine nilikuwa kichaa, iweje kila mtu asinijali au kuniuliza chochote pale nilipokuwa.
Hayo yalikuwa maisha yangu kipindi cha mwanzoni mwa uzima wangu wagu wa mara ya pili, niliona watu ambao nilihisi ni tofauti sana na mimi,,,,,nilisogea mpaka mbele kwenye bustani kubwa na kutazama mbele mita 200 nikagundua pale ni
karibu kabisa na ufukwe wa bahari.
****
"hallo,,!"niliskia sauti ikiniita wakati nipo pale kwenye bustani nikageuka,alikuwa ni msichana
mwenye asili kama yangu lakini sikuwa namfahamu,,alinisogelea karibu nakuanza kunisemesha,nilielewa lugha aliyokuwa akiiongea,
niliwahi kuwa nikiiongea sehemu fulani lakini sikukumbuka ni wapi.
Patrick namshukuru sana mungu uko hai,nashukuru umerudisha fahamu zako aliongea huku akionekana kweli kuwa alikuwa akilifurahia hilo.
Sikumjua huyu dada wala sikufahamu yeye amenijuaje.
utapona kabisa na utakumbuka kila kitu,tunafanya tuwezavyo kuhakikisha kuwa unarudisha fahamu zako alizidi kusisitiza huku akifuta machozi.
wewe ni nani nilimuuliza huku nikimtazama usoni,hakika sura yake sikuijua kabisa, hata kama sikuwa na fahamu lakini sura yake ni kweli
sikuwahi kuiona hata kidogo.
Naitwa Pamela, ndiye daktari ninayemsaidia dokta Anderson katika matibabu yako, ni mimi ambaye
ndiye nakuwa na wewe muda wote kuangalia afya yako, wewe ni sababu ya mimi kuendelea kuwa hapa aliongea huku akionekana kuangalia pembeni kana kwamba alikuwa akifuta machozi.
kwanini unalia nilimuuliza huku nikimgeuza ili aniangalie.
silii, ni furaha tu kwakuwa umeamka leo kichwa changu kilikuwa kimejaa maswali mengi sana,lakini sikujua namna ya kuyauliza, kila kitu pale
kilikuwa ni michoro kwangu isiyoashiria chochote,
nilikuwa nimevurugwa akili na kila kitu kabisa,sikumfahamu yule Pamela na wala sikujua yeye ninani, sikujua anaposema nimeamka je nililala toka
lini, na kwanini kuamka kwangu kuwe ni furaha kwake, kwanini alie kwa mimi kuamka, kwanini alionyesha furaha na kusema nitapona, yeye
alikuwa nani kwangu, mimi nilikuwa na thamani gani kwake, hiyo yote ilikuwa ni jakamoyo ndani ya
moyo wangu, nilikuwa kama teja lililokuwa likihudhuria kliniki ya ukichaa.
Pamela, mimi sielewi chochote nilimuuliza huku nikilia baada ya kujitahidi sana kukumbuka lakini
ikashindikana. Hakunijibu chochote badala yake alinishika mkono na kuondoka na mimi mpaka
ndani ya ile hospitali. Tulipofika pale aliingia ndani na kutoka na daktari mmoja mzungu aliyekuja pale
na kuanza kuongea na mimi kisha Pamela alikuwa akinitafsiria.
Hellow Patrick am doctor Anderson(habari
Patrick, naitwa dokta Anderson). Alinisalimu na kunipa mkono, na mimi nilimpa mkono.
We want to discharge you, but you will be under the care of doctor Pamela, you will stay at her
place until we are sure that you can stand on your own(tunataka tukuruhusu lakini utakuwa chini ya
uangalizi wa dokta Pamela, utakaa nyumbani kwake hadi tutakapokuwa na uhakika kuwa kuwa unaweza kujitegemea) sauti ya Pamela ilisikika ikitafsiri maneno ya dokta Anderson.
Pamela dont bother to interpret, I do understand the language (Pamela usihangaike kutafsiri,
naielewa hiyo lugha), nilimuambia hayo Pamela na yeye alinyamaza kimya.
*********
Niliruhusiwa kutoka pale hospitali na sasa tuliingia kwenye gari ya dokta Pamela kuelekea kwake,
hapakuwa mbali sana na pale hospitali, muda wa dakika kumi tulikuwa tumeshafika.
karibu sana Patrick, hapa ni nyumbani kwangu,ndiko ninapoishi, na ndipo ambapo na wewe utaishi alinikaribisha huku akitabasamu na
kuruhusu vishimo vidogo kwenye mashavu yake vionekane, nilikaribia na kuketi huku nikitazama kila kona ya ile nyumba. Ilikuwa ni nyumba ndogo lakini ilikuwa ni nzuri na ilikuwa na mazingira mazuri yaliyovutia.
Unaishi na nani hapa nilimuuliza swali wakati alipokuwa akienda kuchukua kinywaji kwenye jokofu.
naishi mwenyewe, lakini kwasasa nitakuwa nikiishi na Patrick aliongea hayo na kucheka.
Sikumbuki kama niliwahi kucheka toka pale hospitali. Kwa muda mfupi niliokuwa na Pamela nilikuwa nimegundua kuwa alikuwa mtu mwenye
kupenda sana kucheka, alikuwa ni mtu mcheshi na anayependa utani muda mwingi. Nilianza maisha haya ya kuishi kwa Pamela na muda mwingi dokta Anderson alikuwa akija pale nyumbani kuniangalia.
Pamela na dokta Anderson walikuwa kama ndugu vile ingawaje Pamela alikuwa na asili tofautikidogo.
***********
Asubuhi tulivu ya desemba 1999 ilinikuta nikiwa Suva huko Fiji, ilikuwa ni miezi mitatu sasa toka
nitoke hospitali lakini mpaka wakati huo bado sikujua chochote, mbali na kumuuliza Pamela maswali mengi lakini hakuwa tayari kabisa
kunieleza chochote, siku zote historia ya maisha
yangu na sababu za kwanini sina kumbukumbu yeye hakuziona za maana.
Patrick leo tunatoka nilimsikia Pamela akinipa taarifa hiyo asubuhi wakati alipokuja kugonga chumba changu.
tunaenda wapi nilimuuliza huku nijiachanisha na shuka zito nililokuwa nimejifunika.
tunaenda Albert Park, amka ujiandae tunaondoka muda sio mrefu niliamka na kuanza kujiandaa.
***********
Safari ya kuelekea Albert Park ilianza, tulikwenda mpaka Tanoa plaza tukipitia Amy Roas na hapo
tulisimama, kisha Pamela aliniambia tushuke tuingie ndani ya lile jengo. Tuliingia mpaka ndani ya jengo lile na kwenda upande wakulia mpaka juu
kabisa ambapo tuliweza kuona mandhari yote ya
Fiji na kwambali alinionyesha nchi ya Australia.
Nikiwa pale juu nilisikia kama sauti yamsichana ikiniita na nilipogeuka nyuma sikuona mtu.
ni nini Patrick aliniuliza Pamela lakini sikuwa na la kumjibu, nilipokuwa nimegeuka sikumuona mtu
yoyote lakini kwa uhakika kabisa niliona kama kivuli cha msichana niliyehisi kumfahamu, najua
hata ningesema Pamela asingenielewa.
hamna kitu, sijui ni nini nimeona nilimueleza hayo na yeye alinifata na kunishika kichwa akiniambia
kuwa amenileta pale kwasababu japo hakunieleza ni sababu gani hiyo. Alitnitoa pale na kunipeleka
ndani zaidi kwenye chumba fulani na hapo nilianza kuhisi mapigo ya moyo yakinienda mbio.
Pamela kuna nini hapa nilimuuliza Pamela lakini hakuniambia kitu badala yake alinifunga kitambaa
usoni na kuniambia niketi, niliketi huku nikiwa na wasiwasi juu ya kilichokuwa kikitokea pale. Giza
lilikuwa limetanda kwenye macho yangu na hofu ilinifika. Nilianza kuona picha ya msichana kwa
mbali na sikujua ni nani. Alikuwa msichana mrembo mweupe ambaye nilikuwa naye sehemu kama ufukweni mwa bahari, yule msichana alikuwa
akifurahi na mimi nilikuwa nikimkumbatia kama vile tulikuwa wapenzi,,niliogopa sana kwakuwa
haikuwa kawaida, alinifungua tena kile kitambaa na kuniuliza nimeona nini lakini sikuwa na la kumjibu.
mimi ni nani Pamela? nilimuuliza huku nikiwa kama natetemeka, alinitazama machoni huku akionekana kuzuia machozi.
ukitaka kujua wewe ni nani lazima uwe makini na kile kikujiacho kwenye fikra zako aliniambia
nakuninyanyua kisha tulienda mpaka kwenye chumba kilichokuwa kulekule ndani kisha alivua nguo zake mbele yangu na kuvaa taulo na
kuelekea bafuni, akiwa bafuni nilisikia akiniita lakini
kwa uwoga nilivua nguo zangu na kuvaa taulo kisha nikamfata bafuni, nilipoingia alinikumbatia na
kuanza kunipiga mabusu mwili mzima, mihemko ya mwili wangu ilikuwa karibu kabisa na hisia zangu hivyo nilianza kulipiza mashambulizi, kila
nilipokuwa nikimshika kuna picha ya mwanamke ilikuwa ikinijia, tulitoana bafuni na kuja mpaka kitandania kisha kazi ilianza pale, Pamela alikuwa mtundu sana kitandani lakini kila alipojitahidi kunifanyia mambo flani taswira ya mwanamke
mwingine ilikuwa ikinijia, tuliendelea kusumbuana na kuchokozana hisia zetu na mwishowe
tulikutanisha maungo yetu ya uzazi, nilipokuwa katikati ya mchezo wakati Pamela akiwa juu kuongoza jahazi niliona sura ya yule msichana
tena na kushtuka ana hapo Pamela alizidisha kasi,nilikuwa kama mtoto mdogo vile jinsi ambavyo
nilikuwa nikilia na ile sura ya yule mwanamke ilikuwa ikinijia bado.
Mary,,,Mary nilijikuta nikitamka lile jina na hapo Pamela aliacha na kunishika kichwa,,kisha alikuwa
akiniangalia kwa makini.
kafanyaje aliniuliza kama vile hakuelewa ninachomaanisha, nilinyamaza kwakuwa sikujua
namna ya kuendelea kuelezea, hapo Pamela alianza tena kuushika mwili wangu na kuendelea
na shughulia yake mpaka nilipokumbuka baadhi ya vitu.
Mary ni nani Pamela nilimuuliza kisha alinyanyuka vilevile akiwa uchi na kuondoka kuelekea bafuni, alipokuwa akiondoka nilimtizama
na ile picha ilinijia tena. Nilijivuta pale kitandani na
kwenda kumfata kule bafuni, alifungua lile bomba la mvua na kunivuta kisha alinikumbatia huku maji yakitumwagikia. Nilikuwa nimetumbua macho na
yeye hakuwa anaongea zaidi ya kufungwa macho akiyaruhusu maji yazilowanishe nywele zake laini.
*****
USIKU WA SIKU HIYO.
Tulikuwa tumelala nyumbani kwa Pamela na siku hiyo ilikuwa mara ya kwanza mimi na Pamela
kufanya yote yaliyotokea mchana huo.
Mary ni nani lilikuwa swali la kwanza kumuuliza Pamela usiku ule. Alikuwa amenilalia kifuani lakini
nilipomuuliza alinyanyuka na kuketi.
Mary ni msichana uliyekuja naye Fiji miaka zaidi ya sita sasa, ni mke wako na alikaa hapa akikuuguza kwa zaidi ya miezi sita ila baadaye
aliamua kuondoka baada ya kumwambia kuwa si rahisi wewe kurudisha fahamu tena, aliondoka na
hatukujua ni wapi alikwenda, tumejaribu sana kutafuta kumbukumbu zako lakini hatukupata
alinieleza hiku akijikaza ili asilie.
kwanini sikuwa na fahamu nilimuuliza.
ulichomwa sindano ya dicomenzol, inayotumiwa kuchoma wanyama wakali ili kuwafanya watulie,
walikuchoma wakazidisha kipimo na hii ilikuwa ni baada ya wewe kupata ajali ambayo hata hivyo tunahisi ilikuwa ni ya kukusudiwa, yani kuna mtu aliitengeneza ili itokee ndo wakuchome sindano ile ambayo ilimaliza kila kitu kichwani mwako
Mary Robertnilikumbuka.