Kila ulichoandika kimechafuliwa na maoni yako, tumeshindwa kujua kama kweli Dr. Slaa aliyasema hayo maneno au ni mawazo yako mleta huu uzi. Ungetueleza kasema nini, wapi na lini, then ungeweka maoni yako.WanaJF!
Huu ni moja ya usanii wa Dr Slaa katika siasa zake zilizo sheheni ulaghai kwa watanzania.
wanajf
dr slaa hii nchi ina wenyewe!
kama hayo ni kweli kwa nini mtumie nguvu kiasi hicho? kwani watu si wanaona matendo; mbona mnaongea hadi mapovu na mimacho inawatoka? ukweli kamwe huwezi kutumia nguvu kuutangaza.kwani alichosema niuongo? slaa maneno mengi utekelezaji 0. anajichumia mipesa kibao wakati maofisi ya matawi yako kwenye saloon za watu.
Tatizo la watu wengi humu wanafuata mkumbo au hawajui wanachokitetea, huu uzi tangu 2010, from Rutashubanyuma aliyasema hayo maneno lakini utawasikia watu walio na makengeza ya macho na upofu wa masikio wanasema Dr. kalishwa maneno.
Dr Slaa ni msanii wa ukweli kama mnadhani ndio mkombozi wenu andikeni maumivu, angeanza kula mihogo na hawala yake kabla hajapewa huo uraisi
Kama alishindwa kuwatumikia kondoo wa bwana, sidhani kama ataweza kuwatumikia watanzania.
"Mimi nimeweza kwa sababu nina uwezo wa kulipa zaidi ya Sh4 milioni MOI (Kitengo cha Mifupa cha Hospitali ya Muhimbili) Muhimbili. Je ni Watanzania wangapi wenye uwezo kama wa Dk Slaa, alihoji. Awagiwie sasa huo uwezo wake hao masikini ili awe nao sawa yeye si mpenda usawa? adhihirishe kwa vitendo!
Nafikiri wewe unamfuatilia HAMY-D kinyumenyume. ukweli ni kwamba, nyie machadema mlijifanya kuwa CHADEMA na DR SLAA ni watakatifu. mkasahau kuwa dr slaa ni binadamu kama walivyo binadamu wengine na hivyo hakosi mapungufu. vivyo hivyo kwa chadema, ni chama cha siasa kama ilivyo kwa vyama vingine na kwamba wakati wa harakati za kwenda Ikulu kinatumia mbinu nyingi chafu na batili. Kitendo cha HAMY-D kueleza ukweli nyie wengine mnachukia kitu ambacho sidhani kama ni busara. ukweli upokeeni hata kama ni mchungu