Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,320
Mimi kama mwanachama wa kawaida wa CDM, siingii katika vikao vya juu vya chama, hivyo naamini ni sahihi nikitumia jukwaa letu hili pendwa kufikisha ujumbe kwa viongozi wangu.
Dr. Slaa, tunatambua na kuheshimu sana kazi kubwa unayofanya ya kuuza chama, lakini kuna hii homework ambayo bado haijafanyiwa kazi.
Tatizo ni kwamba, hadi sasa CDM katika baadhi ya maeneo (nadhani maeneo mengi), haina watu wenye 'uwezo' wa kuongoza, kutenda na kugombea nafasi mbalimbali.
katika uchaguzi uliopita, tulishuhudia kuwa katika maeneo mengi CDM ilishindwa sio kwa sababu haikupigiwa kura za kutosha, au sio kwa sababu haikuwa inapendwa, bali kwa sababu haikuwa na wagombea na watendaji wenye mvuto, uwezo wa kuongoza na/au uwezo wa kusimamia kura.
Wapiga kura wanashawishiwa majukwaani, lakini wapigiwa kura wanapikwa (groomed). Wenzetu CCM wanaiba ndio, lakini pia wanatuzidi pia kwa kuwa na wapigiwa kura 'wenye uwezo' zaidi. Nilishasema hapa, tungechukua majimbo 100 yenye wagombea wa CDM in random, alafu wagombea wa CCM katika majimbo hayo wakachukua kadi za CDM, then tukafanya kura za maoni, sio zaidi ya majimbo 20 kati ya hayo watakayochaguliwa waliokuwa wagombea wa CDM tokea mwanzo. CCM wanawa-groom wagombea wao mapema. Sio vibaya tukaiga kwao kama ni jambo jema.
watu wanaweza kudhani kuwa hii itacompromise demekrasia wakati wa kura za maoni; no, kama kuna mtu ameshapikwa katika jimbo au kata husika, then wakati wa kura za maoni akatokea mwingine mwenye sifa zaidi, then well anachukuliwa mwenye sifa zaidi. Hii ina maana kuwa demekrasia inazingatiwa.
Katika uchaguzi uliopita tulishuhudia (kwa wale tulioshiriki) katika baadhi ya maeneo tukiwa na wagombea wabovu na maeneo mengine tukiwa hatuna wagombea kabisa. Huu ni udhaifu ambao kwa gharama yeyote hatutakiwi tuende nao katika uchaguzi wa 2015, au uchaguzi wowote mdogo utakaojitokeza tena hapa katikakti.
Dr Slaa anza kusajili timu yako mapema, sio vizuri kuwa kama Arsene Wenger...
Dr. Slaa, tunatambua na kuheshimu sana kazi kubwa unayofanya ya kuuza chama, lakini kuna hii homework ambayo bado haijafanyiwa kazi.
Tatizo ni kwamba, hadi sasa CDM katika baadhi ya maeneo (nadhani maeneo mengi), haina watu wenye 'uwezo' wa kuongoza, kutenda na kugombea nafasi mbalimbali.
katika uchaguzi uliopita, tulishuhudia kuwa katika maeneo mengi CDM ilishindwa sio kwa sababu haikupigiwa kura za kutosha, au sio kwa sababu haikuwa inapendwa, bali kwa sababu haikuwa na wagombea na watendaji wenye mvuto, uwezo wa kuongoza na/au uwezo wa kusimamia kura.
Wapiga kura wanashawishiwa majukwaani, lakini wapigiwa kura wanapikwa (groomed). Wenzetu CCM wanaiba ndio, lakini pia wanatuzidi pia kwa kuwa na wapigiwa kura 'wenye uwezo' zaidi. Nilishasema hapa, tungechukua majimbo 100 yenye wagombea wa CDM in random, alafu wagombea wa CCM katika majimbo hayo wakachukua kadi za CDM, then tukafanya kura za maoni, sio zaidi ya majimbo 20 kati ya hayo watakayochaguliwa waliokuwa wagombea wa CDM tokea mwanzo. CCM wanawa-groom wagombea wao mapema. Sio vibaya tukaiga kwao kama ni jambo jema.
watu wanaweza kudhani kuwa hii itacompromise demekrasia wakati wa kura za maoni; no, kama kuna mtu ameshapikwa katika jimbo au kata husika, then wakati wa kura za maoni akatokea mwingine mwenye sifa zaidi, then well anachukuliwa mwenye sifa zaidi. Hii ina maana kuwa demekrasia inazingatiwa.
Katika uchaguzi uliopita tulishuhudia (kwa wale tulioshiriki) katika baadhi ya maeneo tukiwa na wagombea wabovu na maeneo mengine tukiwa hatuna wagombea kabisa. Huu ni udhaifu ambao kwa gharama yeyote hatutakiwi tuende nao katika uchaguzi wa 2015, au uchaguzi wowote mdogo utakaojitokeza tena hapa katikakti.
Dr Slaa anza kusajili timu yako mapema, sio vizuri kuwa kama Arsene Wenger...