Imany John
JF-Expert Member
- Jul 30, 2011
- 2,930
- 1,165
Makampuni yachota yatakavyo Yamo pia Deep Green, Tangold WIZI wa mabilioni ya
shilingi katika Benki
Kuu ya Tanzania (BoT)
ulifanywa kwa baraka
za serikali,
MwanaHALISI limegundua. Nyaraka za benki na
Hazina ambazo nakala zake zimeifikia gazeti hili zinaonyesha ushirika
usiokuwa wa kawaida katika kuwezesha
uchotaji wa fedha za umma. Ushirika huo unahusisha makampuni ya Tangold
Limited, Deep Green Finance Company na benki
ya Nedbank ya Afrika Kusini. Kwa mfano, kile ambacho BoT inaonyesha
kuwa ni hati za dhamana zilizouzwa kwa
kampuni ya Tangold Limited, kimegundulika
kuwa ni hewa. Nyaraka zinaonyesha kuwa mwaka 2005
Tangold ilinunua hati za dhamana za Sh. 50
bilioni, lakini taarifa kutoka ndani ya BoT na
Hazina zinaeleza kinyume chake. Kwa mujibu wa taarifa Na. 001/2005 ya BoT,
Tangold Limited ilinunua na kupewa hati ya
dhamana yenye thamani ya Sh. 25 bilioni, tarehe
1 Mei 2005. Hii ilikuwa Siku Kuu ya Wafanyakazi
(Mei Dei) ambayo huwa ni siku ya mapumziko
kwa ofisi zote za serikali. Vilevile kwa taarifa Na. 002/2005 ya BoT,
Tangold ilinunua na kupewa hati ya dhamana ya
thamani ya Sh. 25 bilioni, tarehe hiyohiyo. Kufuatana na masharti ya mkataba, Tangold
ilipaswa kulipwa na serikali riba ya asilimia 10
kila mwaka, kwa mikataba yote miwili kwa
kipindi cha miaka 10 hadi mwaka 2015. Lakini kumbukumbu za BoT ambazo ni nadra
sana kuonekana hata kwa wakaguzi
zinaonyesha kuwa hakukuwa na mnada wala
tangazo la serikali la kuuza dhamana ambako
Tangold ilinunua dhamana hizo. Kwa utaratibu, dhamana za serikali
hutangazwa rasmi kwa umma kupitia Gazeti la
Serikali (Official Government Gazette) au hata
kwenye vyombo vingine vya habari, ameeleza
ofisa mwandamizi wa BoT. Nakwambia kama kungekuwa na hati ya
dhamana ambayo imenunuliwa na Tangold,
ingetangazwa na kujulikana kwa umma.
Haikuwepo, amefafanua ofisa huyo. Mbali na gazeti la serikali na vyombo vya habari,
matangazo huweza pia kutolewa kupitia tovuti
ya BoT ambayo ni www.bot-tz.org ambako
imethibitishwa kwamba hakukuwa na
matangazo kuhusu uuzaji dhamana hizo,
ameeleza. Kauli hizo na ukweli wa nyaraka
vinathibitishwa na hali halisi ya Tangold kama
ilivyoonyeshwa kwenye akaunti yake iliyoko
mjini Port Luis, Mauritius. Taarifa ya akaunti ya Tangold ya tarehe 31 Julai
2005 inaonyesha kiwa Tangold ilikuwa na
amana ya kiasi cha dola za Marekani 996.75 tu. Tangold ilipofungua akaunti yake Na. 04413136
katika benki ya Federal Trust mjini Port Louis,
tarehe 31 Desemba 2004, iliweka dola 2,455.00.
Kiasi hicho hakikuongezeka hadi 31 Julai 2005. Aidha, hata kwenye akaunti yake nchini
Tanzania, katika benki ya NBC, makao makuu,
haikuwa na fedha za kununulia dhamana za
serikali. Fedha za kwanza kuingia akaunti ya Tangold
hapa nchini zilikuwa Sh. 1.5 bilioni na ilikuwa 1
Agosti 2005. Fedha hizo zilitoka BoT na
haikuelezwa ni kwa kazi ipi. Siku hiyo hiyo zilihamishwa Sh. 1.5 bilioni
kwenda kampuni ya Deep Green kutoka BoT
vilevile kwa kazi ambayo haijaweza
kugundulika. Tangold ni moja ya makampuni yenye utata
katika miliki na usajili wake. Wakati
inaonyeshwa ilisajiliwa Mauritius na baadaye
kufungua tawi Tanzania, serikali ilieleza
bungeni kuwa ni kampuni yake kwa asilimia
100. Kwa mujibu wa taarifa zilizopo kwa Wakala wa
Usajili wa Makampuni (BRELA), wakurugenzi wa
Tangold ni pamoja na Daudi Ballali, Gray Mgonja,
Andrew Chenge, Patrick Rutabanzibwa na
Vincent Mrisho. Nayo Deep Green inaonyesha ilisajiliwa
Tanzania mwaka 2005 na kwamba anwani
yake ya usajili ni IMMA House, Kiwanja Na. 357
Barabara ya Umoja wa mataifa, Upanga Dar es
Salaam. IMMA ni kampuni ya mawakili Protase
Ishengoma, Aloysius Mujulizi, Lawrance Masha
na Sadock Magai ya Dar es Salaam. Hivi sasa
Mujulizi ni jaji wa mahakama kuu na Masha ni
waziri wa mambo ya ndani. Gazeti hili liliwahi kufichua ukwapuaji wa Sh. 8
bilioni kutoka BoT uliofanywa na Deep Green,
kati ya Septemba na Desemba 2005
(MwanaHALISI Na. 087). Haikuelezwa pia
zilikuwa kwa shughuli ipi. Katika hali isiyo ya kawaida, Tangold
inayodaiwa kuwa kampuni ya serikali, iliingia
mkataba na Deep Green ambayo ni ya binafsi
ambao uliipa Deep Green haki zote za mikataba
yake na BoT na serikali. Nyaraka za Tangold zinaiagiza serikali na BoT
kutii mikataba yake na bila swali, na gavana
Ballali na Katibu Mkuu Hazina Gray Mgonja
wanakubaliana kutii. Kwa mfano vifungu Na. 3 na 4(e) vya mkataba
wa Tangold na Deep Green, vinafanya Tangold,
ambayo inadaiwa kuwa mali ya serikali, kukosa
kabisa maamuzi katika mkataba. Hili linajidhirisha katika barua Na. PST/GEN/2005
ya 25 Mei 2005 kutoka Hazina kwenda Deep
Green ikikubali masharti ya kutobadili lolote
katika mikaba ya makampuni hayo. Kwa mfano, BoT ilikubali kuwasilisha malipo
yoyote, pamoja na kile kinachoitwa riba kwa
dhamana hewa, katika akaunti Na.
011103024840 katika NBC makao makuu na
akaunti nyingine ambazo Deep Green itaagiza. Tutalipa bila masharti yoyote kwetu, fedha
zote zinazohitajika katika akaunti Na.
011103024840 au kama itakavyoelekezwa na
Deep Green, ilisema barua ya serikali. Barua hiyo ina saini ya mwenye mamlaka ya
kusaini kwa niaba ya serikali Authorised
Signatory for and on behalf of the government
of the United Republic of Tanzania na nakala
kupelekwa Tangold. Ni hali hii ambayo inafanya wafuatiliaji wa
masuala ya utawala wa fedha BoT kuwa na
mawazo kuwa Deep Green ama ni ya
Watanzania au wana ubia ndani yake. Kufuatia serikali kujifunga kulipa katika akaunti
za Deep Green, gavana Daudi Ballali aliagiza
malipo ya Sh. 1, 546,778,770.92 (1.6 bilioni)
yafanywe kwenye akaunti ya Tangold Na.
011103024840 iliyoko NBC makao makuu. Katika maelekezo kwenye karatasi isiyo na
tarehe wala saini (maofisa BoT
wamethibitisha), Ballali anasema dhamana
tayari imejikusanyia riba tangu 1 Mei 2005. Mkanganyiko hapa ni kwamba Tangold
haikuwa na fedha kwenye akaunti zake ndani
na nje ya nchi. Ilikuwa haijasajiliwa Tanzania. Aidha, siku inayotajwa kuwa Tangold tayari ina
limbikizo la riba, ni siku hiyohiyo
inayoonyeshwa kuwa ndipo kampuni hiyo
ilifunga mkataba wa kununua dhamana! Bila kujali kuwa Tangold haina dhamana,
haijasajiliwa, haijawa na lundo la riba, wala
fedha kwenye akaunti zake, gavana Ballali
anaagiza kuwa fedha zinazobaki, zipelekwe
akaunti Na. 011103024852. Tangold, Deep Green na benki ya Nedbank
wanatumia karatasi na anwani zilezile za mitaa
na jengo mjini Sandton, Afrika Kusini nakupitia
msemaji mmoja aliyetajwa kuwa Wayne
Khoury katika Nedbank. Gazeti lilijitahidi kumpata Bw. Khoury kwa
baruapepe yake ili kujua uhusiano wake na
taarifa za malipo. Hata hivyo hadi tunakwenda
mitamboni baruapepe ilikuwa haijajibiwa. Simu
yake haikujibu. Nedbank, kwa mujibu wa uchunguzi wa
MwanaHALISI, ilitumika pia kupitisha malipo
kwa ajili ya kampuni ya Meremeta, moja ya
makampuni yanayodaiwa kukwapua mabilioni
ya shilingi kutoka BoT na serikalini. Wiki iliyopita, gazeti hili liliripoti ukosefu wa
kanuni za utoaji fedha katika akaunti ya EPA;
udhaifu katika utendaji na wizi wa nyaraka za
BoT. Imefahamika kuwa gavana Ballali alikuwa
akimwagiza meneja wa tawi la NBC makao
maku, P.J. Mapunda kulipa mabilioni ya shilingi
kwa Deep Green, Tangold na Meremeta. Mwandishi alipotaka kupata maoni ya Bw.
Mapunda kuhusu madai hayo, aliambiwa na
maofisa wa NBC kuwa kuwa ameishafariki. Gavana Ballali alifariki Mei mwaka jana katika
mazingira yaliyoacha maswali mengi; baada ya
serikali kuficha alipo kwa kipindi kirefu.
shilingi katika Benki
Kuu ya Tanzania (BoT)
ulifanywa kwa baraka
za serikali,
MwanaHALISI limegundua. Nyaraka za benki na
Hazina ambazo nakala zake zimeifikia gazeti hili zinaonyesha ushirika
usiokuwa wa kawaida katika kuwezesha
uchotaji wa fedha za umma. Ushirika huo unahusisha makampuni ya Tangold
Limited, Deep Green Finance Company na benki
ya Nedbank ya Afrika Kusini. Kwa mfano, kile ambacho BoT inaonyesha
kuwa ni hati za dhamana zilizouzwa kwa
kampuni ya Tangold Limited, kimegundulika
kuwa ni hewa. Nyaraka zinaonyesha kuwa mwaka 2005
Tangold ilinunua hati za dhamana za Sh. 50
bilioni, lakini taarifa kutoka ndani ya BoT na
Hazina zinaeleza kinyume chake. Kwa mujibu wa taarifa Na. 001/2005 ya BoT,
Tangold Limited ilinunua na kupewa hati ya
dhamana yenye thamani ya Sh. 25 bilioni, tarehe
1 Mei 2005. Hii ilikuwa Siku Kuu ya Wafanyakazi
(Mei Dei) ambayo huwa ni siku ya mapumziko
kwa ofisi zote za serikali. Vilevile kwa taarifa Na. 002/2005 ya BoT,
Tangold ilinunua na kupewa hati ya dhamana ya
thamani ya Sh. 25 bilioni, tarehe hiyohiyo. Kufuatana na masharti ya mkataba, Tangold
ilipaswa kulipwa na serikali riba ya asilimia 10
kila mwaka, kwa mikataba yote miwili kwa
kipindi cha miaka 10 hadi mwaka 2015. Lakini kumbukumbu za BoT ambazo ni nadra
sana kuonekana hata kwa wakaguzi
zinaonyesha kuwa hakukuwa na mnada wala
tangazo la serikali la kuuza dhamana ambako
Tangold ilinunua dhamana hizo. Kwa utaratibu, dhamana za serikali
hutangazwa rasmi kwa umma kupitia Gazeti la
Serikali (Official Government Gazette) au hata
kwenye vyombo vingine vya habari, ameeleza
ofisa mwandamizi wa BoT. Nakwambia kama kungekuwa na hati ya
dhamana ambayo imenunuliwa na Tangold,
ingetangazwa na kujulikana kwa umma.
Haikuwepo, amefafanua ofisa huyo. Mbali na gazeti la serikali na vyombo vya habari,
matangazo huweza pia kutolewa kupitia tovuti
ya BoT ambayo ni www.bot-tz.org ambako
imethibitishwa kwamba hakukuwa na
matangazo kuhusu uuzaji dhamana hizo,
ameeleza. Kauli hizo na ukweli wa nyaraka
vinathibitishwa na hali halisi ya Tangold kama
ilivyoonyeshwa kwenye akaunti yake iliyoko
mjini Port Luis, Mauritius. Taarifa ya akaunti ya Tangold ya tarehe 31 Julai
2005 inaonyesha kiwa Tangold ilikuwa na
amana ya kiasi cha dola za Marekani 996.75 tu. Tangold ilipofungua akaunti yake Na. 04413136
katika benki ya Federal Trust mjini Port Louis,
tarehe 31 Desemba 2004, iliweka dola 2,455.00.
Kiasi hicho hakikuongezeka hadi 31 Julai 2005. Aidha, hata kwenye akaunti yake nchini
Tanzania, katika benki ya NBC, makao makuu,
haikuwa na fedha za kununulia dhamana za
serikali. Fedha za kwanza kuingia akaunti ya Tangold
hapa nchini zilikuwa Sh. 1.5 bilioni na ilikuwa 1
Agosti 2005. Fedha hizo zilitoka BoT na
haikuelezwa ni kwa kazi ipi. Siku hiyo hiyo zilihamishwa Sh. 1.5 bilioni
kwenda kampuni ya Deep Green kutoka BoT
vilevile kwa kazi ambayo haijaweza
kugundulika. Tangold ni moja ya makampuni yenye utata
katika miliki na usajili wake. Wakati
inaonyeshwa ilisajiliwa Mauritius na baadaye
kufungua tawi Tanzania, serikali ilieleza
bungeni kuwa ni kampuni yake kwa asilimia
100. Kwa mujibu wa taarifa zilizopo kwa Wakala wa
Usajili wa Makampuni (BRELA), wakurugenzi wa
Tangold ni pamoja na Daudi Ballali, Gray Mgonja,
Andrew Chenge, Patrick Rutabanzibwa na
Vincent Mrisho. Nayo Deep Green inaonyesha ilisajiliwa
Tanzania mwaka 2005 na kwamba anwani
yake ya usajili ni IMMA House, Kiwanja Na. 357
Barabara ya Umoja wa mataifa, Upanga Dar es
Salaam. IMMA ni kampuni ya mawakili Protase
Ishengoma, Aloysius Mujulizi, Lawrance Masha
na Sadock Magai ya Dar es Salaam. Hivi sasa
Mujulizi ni jaji wa mahakama kuu na Masha ni
waziri wa mambo ya ndani. Gazeti hili liliwahi kufichua ukwapuaji wa Sh. 8
bilioni kutoka BoT uliofanywa na Deep Green,
kati ya Septemba na Desemba 2005
(MwanaHALISI Na. 087). Haikuelezwa pia
zilikuwa kwa shughuli ipi. Katika hali isiyo ya kawaida, Tangold
inayodaiwa kuwa kampuni ya serikali, iliingia
mkataba na Deep Green ambayo ni ya binafsi
ambao uliipa Deep Green haki zote za mikataba
yake na BoT na serikali. Nyaraka za Tangold zinaiagiza serikali na BoT
kutii mikataba yake na bila swali, na gavana
Ballali na Katibu Mkuu Hazina Gray Mgonja
wanakubaliana kutii. Kwa mfano vifungu Na. 3 na 4(e) vya mkataba
wa Tangold na Deep Green, vinafanya Tangold,
ambayo inadaiwa kuwa mali ya serikali, kukosa
kabisa maamuzi katika mkataba. Hili linajidhirisha katika barua Na. PST/GEN/2005
ya 25 Mei 2005 kutoka Hazina kwenda Deep
Green ikikubali masharti ya kutobadili lolote
katika mikaba ya makampuni hayo. Kwa mfano, BoT ilikubali kuwasilisha malipo
yoyote, pamoja na kile kinachoitwa riba kwa
dhamana hewa, katika akaunti Na.
011103024840 katika NBC makao makuu na
akaunti nyingine ambazo Deep Green itaagiza. Tutalipa bila masharti yoyote kwetu, fedha
zote zinazohitajika katika akaunti Na.
011103024840 au kama itakavyoelekezwa na
Deep Green, ilisema barua ya serikali. Barua hiyo ina saini ya mwenye mamlaka ya
kusaini kwa niaba ya serikali Authorised
Signatory for and on behalf of the government
of the United Republic of Tanzania na nakala
kupelekwa Tangold. Ni hali hii ambayo inafanya wafuatiliaji wa
masuala ya utawala wa fedha BoT kuwa na
mawazo kuwa Deep Green ama ni ya
Watanzania au wana ubia ndani yake. Kufuatia serikali kujifunga kulipa katika akaunti
za Deep Green, gavana Daudi Ballali aliagiza
malipo ya Sh. 1, 546,778,770.92 (1.6 bilioni)
yafanywe kwenye akaunti ya Tangold Na.
011103024840 iliyoko NBC makao makuu. Katika maelekezo kwenye karatasi isiyo na
tarehe wala saini (maofisa BoT
wamethibitisha), Ballali anasema dhamana
tayari imejikusanyia riba tangu 1 Mei 2005. Mkanganyiko hapa ni kwamba Tangold
haikuwa na fedha kwenye akaunti zake ndani
na nje ya nchi. Ilikuwa haijasajiliwa Tanzania. Aidha, siku inayotajwa kuwa Tangold tayari ina
limbikizo la riba, ni siku hiyohiyo
inayoonyeshwa kuwa ndipo kampuni hiyo
ilifunga mkataba wa kununua dhamana! Bila kujali kuwa Tangold haina dhamana,
haijasajiliwa, haijawa na lundo la riba, wala
fedha kwenye akaunti zake, gavana Ballali
anaagiza kuwa fedha zinazobaki, zipelekwe
akaunti Na. 011103024852. Tangold, Deep Green na benki ya Nedbank
wanatumia karatasi na anwani zilezile za mitaa
na jengo mjini Sandton, Afrika Kusini nakupitia
msemaji mmoja aliyetajwa kuwa Wayne
Khoury katika Nedbank. Gazeti lilijitahidi kumpata Bw. Khoury kwa
baruapepe yake ili kujua uhusiano wake na
taarifa za malipo. Hata hivyo hadi tunakwenda
mitamboni baruapepe ilikuwa haijajibiwa. Simu
yake haikujibu. Nedbank, kwa mujibu wa uchunguzi wa
MwanaHALISI, ilitumika pia kupitisha malipo
kwa ajili ya kampuni ya Meremeta, moja ya
makampuni yanayodaiwa kukwapua mabilioni
ya shilingi kutoka BoT na serikalini. Wiki iliyopita, gazeti hili liliripoti ukosefu wa
kanuni za utoaji fedha katika akaunti ya EPA;
udhaifu katika utendaji na wizi wa nyaraka za
BoT. Imefahamika kuwa gavana Ballali alikuwa
akimwagiza meneja wa tawi la NBC makao
maku, P.J. Mapunda kulipa mabilioni ya shilingi
kwa Deep Green, Tangold na Meremeta. Mwandishi alipotaka kupata maoni ya Bw.
Mapunda kuhusu madai hayo, aliambiwa na
maofisa wa NBC kuwa kuwa ameishafariki. Gavana Ballali alifariki Mei mwaka jana katika
mazingira yaliyoacha maswali mengi; baada ya
serikali kuficha alipo kwa kipindi kirefu.