Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 864
Kwa kweli wasomi ni problem,wengi hata kwenye daftari hawajiandikishi.Wanajifanya hawana muda wa kupanga foleni...Tunahitaji kubadilika wasomi wa Tz.
Kikwazo kikubwa cha kuleta mabadiliko ya kweli nchi hii ni wasomi na wakaazi wa maeneo ya mjini. Nimesoma kwenye threads nyingi hapa, watu wengi wenye mashaka kuwa DR Slaa hatapita ni watu ambao wanatamani mabadiliko yatokee ila hawatambui kuwa wao ni sehemu ya kufanya hayo mabadiliko yatokee.
Jana tulikuwa na wenzangu hapa Mzumbe University (Dar Campus) tunajadili kuhusu uchaguzi. Wengi wakawa wanasema watafurahi sana siku CCM ikiondoka madarakani. Lakini papo hapo wakawa wanasema Dr Slaa hataweza kuishinda maana CCM ni ''wezi'' wa kura hivyo haina haja ya kwenda kupiga kura maana upige kura usipige watashinda tu.
Nilisikitika sana maana tuliokuwa tunajadili wengi walikuwa ni wanafunzi wa shahada za uzamili. Nikajiuliza hivi wasomi wa nchi hii wana matatizo gani, maana hii si mara ya kwanza kusikia maneno kama haya kutoka kwa wasomi wa nchi hii. Nilishaona mwaka 2000, 2005 na sasa 2010.
Lakini cha ajabu mwezi wa tatu mwaka huu nilitembelea wilaya ya Newala kijiji kimoja kinaitwa Nkunya, nilikutana na wananchi wengi ambao kielimu naweza kusema sio wasomi- yaani ni darasa la saba kushuka chini, wao walikuwa wanasema kulingana na tabu wanazozipata akijitokeza mgombea yoyote wa upinzani ambaye ''anaeleweka'' wao watampigia kura na atashinda bila shida maana wamechoka na CCM. Maelezo kama haya nimeshayasikia mara nyingi sana huko vijijini kutoka kwa watu wasio wasomi.
Sasa najiuliza kwanini wasiosoma wanaona upinzani unaweza kushinda lakini waliosoma wanaona tofauti?. Zamani kidogo kuna mwalimu mmoja mstaafu aliniambia tabia ya watanzania wasomi kuwa wapole, kuburuzwa, uoga wa kuthubutu na kutokuwa tayari kujitoa mhanga ni mpango kamili ulioratibitiwa katika aina ya elimu tunayopatiwa- yeye alisema Nyerere alitengeneza mfumo wa elimu ambao unatufanya tuwe hivyo. Sikukubaliana na mawazo yake kwa vile huyo mwalimu alikuwa hampendi kabisa Nyerere.
Lakini sasa naanza kuamini watanzania ambao hawajasoma (wengi walioko vijijini) hawajalishwa sumu (indoctrinated) na elimu ya ''Nyerere'' ndo maana wanaona mageuzi yanawezekana lakini wasomi wanaona tofauti.
Anyway, unahitajika utafiti kubaini kwanini wasomi wako pessmistic upinzani kushinda tofauti na watu wasio soma?
Taib,kama tatizo ni 'wasomi' mboni hata huko CCM wamejaa?? akina Mwakyembe, sijui nani etc etc..To say the truth wasomi wa ukweli Tz ni kama hamna na kama wapo ni kama asilimia isiozidi 1,ndio maana mambo yataendelea kuwa vivihivi milele.wasomi wetu wengi wao wamesomea chieti na si kuelimika ndo maana wako hivyo!!
Inawezekana, timiza wajibu wako. Mbona imewezekana kuving'oa KANU na UNIP?
sio wasomi, wengi watakamuangusha ni watu wa chini
1. Kwanza wewe ndugu, hivi uliweza wauliza hao wenzako wa Mzumbe kuwa ni kwanini wanataka kuitoa CCM madarakani? Usije ukawa umeenda pale ukaanza kuongelea upinzani nao wakakuunga mkono ukadhani kuwa kwa kukuunga mkono wanataka chama pinzani kiingie madarani! Ukiwa mpinzani wa kitu siyo lazima ukikatae chote, unaweza ukawa unapinga baadhi ya vitu. Kumweka mpinzani madarakani si kwamba atatekeleza yale unayotaka. No necessarily. This is true in Zambia, Kenya, Ghana na nchi chache zilizowahi fanya mabadiliko ya kweli Africa. Kwa kifupi, nikipinga CCM simaanishi kwamba wapinzani nawaunga mkono. I can make change within CCM. Na hii dhana ndiyo inawavuruga Watanzania wengi hata hawaelewi maana ya mabadiliko na lini kuyaanzisha.
2. Hao watu wako uliwauliza kama wamejiandisha? Au hata kama wamejiandikisha wana hizo card za kupigia kura? Je walikwambia mikakati yao na Mpinzani wao mtarjiwa ya kuwawezesha kutoka hapo walipo kwenda juu? Uliuza kama watoto wao wamewapeleka shule au kuwinda? Pia uliwakumbusha kuhusu Elimu Dunia ilivyo tofauti na elimu ahera?
Mimi nilienda kijiji kingine kiko Kilwa Kinaitwa Nyuni, kule katika majadiliano walisema wanataka mpinzani,, hasa CUF,,, kwa kuwa itawezesha wao kujiunga na OIC na pia kuwezesha sharia nchini!.
3. Wasomi ni analytical. Kwanza unatakiwa mwenyewe ujiulize kama ume-fanya change kwako mwenyewe kabla ya kutafuta change nje. Afterall, change ni lazima? Kama ni lazima sawa. Lakini kam siyo lazima why go for it now and not later.
4.Kama ukitaka mabadiliko, yafanye wewe mwenyewe. Usiangalie wasomi au wana kijiji Nkunya. Afterall kura unapiga peke yako hakuna mtu unakuwa naye.
wasomi wengi wa tanzania ni waoga wa mabadiliko wamekarili tu mfumo unawangozi ndiyo sahihi, utasikia utafuti wa REDET utakavyompamba kikwete,
Kikwazo kikubwa cha kuleta mabadiliko ya kweli nchi hii ni wasomi na wakaazi wa maeneo ya mjini. Nimesoma kwenye threads nyingi hapa, watu wengi wenye mashaka kuwa DR Slaa hatapita ni watu ambao wanatamani mabadiliko yatokee ila hawatambui kuwa wao ni sehemu ya kufanya hayo mabadiliko yatokee.
Jana tulikuwa na wenzangu hapa Mzumbe University (Dar Campus) tunajadili kuhusu uchaguzi. Wengi wakawa wanasema watafurahi sana siku CCM ikiondoka madarakani. Lakini papo hapo wakawa wanasema Dr Slaa hataweza kuishinda maana CCM ni ''wezi'' wa kura hivyo haina haja ya kwenda kupiga kura maana upige kura usipige watashinda tu.
Nilisikitika sana maana tuliokuwa tunajadili wengi walikuwa ni wanafunzi wa shahada za uzamili. Nikajiuliza hivi wasomi wa nchi hii wana matatizo gani, maana hii si mara ya kwanza kusikia maneno kama haya kutoka kwa wasomi wa nchi hii. Nilishaona mwaka 2000, 2005 na sasa 2010.
Lakini cha ajabu mwezi wa tatu mwaka huu nilitembelea wilaya ya Newala kijiji kimoja kinaitwa Nkunya, nilikutana na wananchi wengi ambao kielimu naweza kusema sio wasomi- yaani ni darasa la saba kushuka chini, wao walikuwa wanasema kulingana na tabu wanazozipata akijitokeza mgombea yoyote wa upinzani ambaye ''anaeleweka'' wao watampigia kura na atashinda bila shida maana wamechoka na CCM. Maelezo kama haya nimeshayasikia mara nyingi sana huko vijijini kutoka kwa watu wasio wasomi.
Sasa najiuliza kwanini wasiosoma wanaona upinzani unaweza kushinda lakini waliosoma wanaona tofauti?. Zamani kidogo kuna mwalimu mmoja mstaafu aliniambia tabia ya watanzania wasomi kuwa wapole, kuburuzwa, uoga wa kuthubutu na kutokuwa tayari kujitoa mhanga ni mpango kamili ulioratibitiwa katika aina ya elimu tunayopatiwa- yeye alisema Nyerere alitengeneza mfumo wa elimu ambao unatufanya tuwe hivyo. Sikukubaliana na mawazo yake kwa vile huyo mwalimu alikuwa hampendi kabisa Nyerere.
Lakini sasa naanza kuamini watanzania ambao hawajasoma (wengi walioko vijijini) hawajalishwa sumu (indoctrinated) na elimu ya ''Nyerere'' ndo maana wanaona mageuzi yanawezekana lakini wasomi wanaona tofauti.
Anyway, unahitajika utafiti kubaini kwanini wasomi wako pessmistic upinzani kushinda tofauti na watu wasio soma?