Dr Slaa ajibu upotoshaji wa Mwandishi Mayage dhidi ya CHADEMA

ntogwisangu said:
Ni vizuri kafanya hivyo!

Sijalisoma bado la yaelekea anajibu kwa kuonyesha postive achievements za CHADEMA na hilo ni kosa!

Mayage kasema chama kina nafasi wafanye zaidi ya walivyofanya sasa! Sasa inaonekana watu hawapendi kukosolewa, hili nalo ni mapungufu ya kiuongozi! Ndo maana Dr Slaa naye hafai kuwa kiongozi wa nchii hii!

Haya ni maoni yangu kama mwana CHADEMA, unafiki kwangu hauna nafasi!!!

Kwa kuwa umejiita mwanachadema ni vizuri nikukumbushe kwamba umekwenda kinyume na kanuni za Chadema. Huwezi kutumia maneno hayo kwa kiongozi wa juu yako. Ni sawa na kuwatukana wajumbe wote wa kamati kuu, Baraza kuu na Mkutano mkuu waliosema anayefaa kuwa mgombea wa Chadema 2015 ni Dr Slaa na siyo Ntogwisangu.

Na kama wewe ni mwanachama na hujui kanuni ndogo kama hiyo, basi una tatizo. Ukitoka safari nitafute tuelekezane vizuri maana hiyo mmoja ya majukumu yangu wala hujanisumbua.

Pili, kama Dr Slaa hukumridhia wewe, uliandika barua yo yote ya malalamiko kama mwanchadema? Kama sivyo kulikoni kuja na mawazo hayo jf?
 
nafasi ya chama kufanya zaidi hutolewa na wananchi na chama hakina uwezo wa kuinyakua. Kama umekiri kuwa kwa kiasi fulani wamefanikiwa na unaamini wanahitajika kufanya zaidi, suala sahihi la wewe kufanya ni kuunga mkono yale yaliyofikiwa ili ridhaa ya wananchi ipatikane, wapewe dola na waweze kufanya hiyo zaidi unayoitaka.

Kuna tofauti kubwa kati ya kukosoa na kuponda. Usipoijua hiyo tofauti utagombana na mama mkwe wako. mayage ameconclude kwenye makala yake kuwa solution ni kuanzishwa chama kingine, huu ni ukosoaji? yawezekana huna nia mbaya ktk comments zako, lkn yaelekea huna akili pia. ni nini unachohitaji wewe kama mwananchi, siasa za kubwabwaja majukwaani na kusubiri uchaguzi au chama kilicho active wakati wote kikiwatumikia wananchi?

uanaharakati ndio hasa msingi wa mabadiliko chanya ktk mataifa ya kidemokrasia. Ndio njia ya kupata haki toka kwa watawala dhalimu. Shida yetu watanzania ni uoga wa mabadiliko. Badilika kimtazamo, acha uoga na unga mkono harakati hizi za chadema. Tanzania haitakuwa huru kwa uwakilishi wa wabunge wanaoorodhesha msululu wa matatizo ya majimbo yao halafu wamalizie kwa 'naunga hoja mkono kwa 100%'.

Na kama shida yako ni yale yanayohubiriwa majukwaani na chadema, labda nikuulize: ulitaka wajadili nini zaidi ya yale yanayotukwamisha tusiendelee?

Kuna kingine kinachotukwamisha zaidi ya ufisadi, mikataba mibovu, wizi wa rasilimali, uwajibikaji mdogo, kujuana na kufumbiana macho tunapokosea?

ni vyema wananchi tukaaacha upuuzi, hizi nguvu za kuisakama chadema tungeielekeza kwenye kuisakama serikali iwachukulie hatua wanaotufilisi. Kama tutagoma kushiriki harakati na kukaa tusubiri kuanzishwa kwa chama kitakacholeta maajabu kwa kukaa ofisini na kukomesha mabaya haya, basi hatutakuwa na tofauti na mayage anayewaza kwa kutumia tumbo.
Wako ktk kupinga mambo ya kijinga na ukosoaji usio na mashiko,

shizukan

huo na wewe upotoshaji!!yawezekana kweli sina akili!!lakin kama ni ya darasani nina uhakika mkubwa hiyo ninayo!!tena wa 100%labda kwa vile wanasema zipo za darasani na za mtaani pengine huo upande wa pili nikawa sina!!!sijapinga yafanywayo!!!ninachokisema kwamba mapendekezo aliyotoa mayage yana tija!!ni ya kufuatwa!!!ukosoaji wake ni chama kujitizama tu!!!ila mimi nikaja na hoja nyingine nikasema kwamba tuna golden chance sasa katika siasa za nchi hii!!ila nikasema mwenyekiti wetu tangu ahachiwe na mh mtei,sasa yatosha ang'atuke!!maana si mtu sahihi wa kwenda naye 2015!!!na nikatoa baadhi ya sababu!!!!ni hayo tu!!!!na kwangu mjadala umefungwa!!!!
 
Naona huyu babu amepata la kusema.:shock::A S 465::A S 465:

Nasubiria tamko lake kuhusu posho ya wabunge.
 
Safi sana, tena huyo Mayage aende zake akamtumikie bwana wake EL.
 
Haya ni maoni yangu kama mwana CHADEMA, unafiki kwangu hauna nafasi!!!

Ntogwisangu, umeanza lini kuwa mwanaCHADEMA? Acha kutudanganya mkuu, ninakufahamu vema sana na harakati zako zote za CCM. Sitaki tu kusema kwa mifano nisije nikaambiwa name calling, lakini si vizuri kujivika ngozi ya kondoo wakati wewe ni mbwa mwitu.
 
ntogwisangu, umeanza lini kuwa mwanachadema? Acha kutudanganya mkuu, ninakufahamu vema sana na harakati zako zote za ccm. Sitaki tu kusema kwa mifano nisije nikaambiwa name calling, lakini si vizuri kujivika ngozi ya kondoo wakati wewe ni mbwa mwitu.

nimesoma nimechoka kweli!!!!!!!ruksa ulichonacho kuhusu mimi kiweke!!!!!!!!hunijui sikujui!!!that"s all!!!!majina yetu haya tabora,shinyanga,mwanza na hata mkoa mpya geita!!!
 
Nyie CHADEMA ni watu gani msiotaka kukosolewa???? Mayage katika makala yake aliwakosoa na kuwataka mfanye vizuri zaidi lakini mmeigeuza makala yake kuwa ugomvi kana kwamba amewatukana matusi ya nguoni. Ni nyie mnaolalamika hali ya nchi kwa sasa na kuhoji kama kweli Rais ana washauri. Nyie mnaukataa ushauri wa Mayage, je huyo Padri wenu aliyeasi akiingia Ikulu atamsikiliza nani?

Huo si ukosoaji, huo ni upondaji ambao haujengi. Kama anakosoa angelenga ktk kuimarisha Chadema, yeye analenga chama kingine kipya kije. Huo ni ukosoaji?
Pili, umetumia neno kuasi upadri. Huo nao ni upotoshaji mwingine. Kwa mujibu wa taratibu za kanisa katoliki, waasi hawaruhusiwi kusali humo - wanafukuzwa. Je, Dr Slaa anavyoendelea kusali huko na kupewa huduma zote za kiroho huko, unataka kusema wakatoliki wamesahau kanuni zao?
Tatu, Kwa sisi tuliotoka Manyara au tunaopakana na Karatu hicho unachokisema wewe ni uposhaji wa 100% tena wa makusudi. Dr Slaa alitumiza taratibu zote zinazopaswa ili aingie kwenye siasa. That is the fact.
 
haya ndo matatizo ya kukaa na kusubili malaika toka mbinguni akukomboe toka mimkononi mwa CCM. nani ataanzisha chama kipya? na hoja mpya kwao ni ipi? au ndo ile staili ya CHAMA CHA JAMII? hapa kimsikngi nina muunga mkono slaa. kwani mpaka sasa ndio chama kilicho mbele kutetea maslahi ya TANZANIA. kitu ambacho naona chadema kinakosea ni kwamba they are over patient, busara zimekuwa nyingi mno. ili kuspeed maendeleo ni lazima waongeze kuwa aggresive kidogo maana CCM washalala.
 
nimesoma nimechoka kweli!!!!!!!ruksa ulichonacho kuhusu mimi kiweke!!!!!!!!hunijui sikujui!!!that"s all!!!!majina yetu haya tabora,shinyanga,mwanza na hata mkoa mpya geita!!!

Sasa wewekama ni mwana CHADEMA kwanini usiende kwenye chama ukaeleza haya matakwa yako kuliko kulalama hapa JF?
 
Sasa wewekama ni mwana CHADEMA kwanini usiende kwenye chama ukaeleza haya matakwa yako kuliko kulalama hapa JF?

nilishaeleza vikwazo nilivyokutana navyo!!!ila kumbuka kwamba pamoja na mapungufu ya wana jf na mods!!bado jf kuna watu muhimu sana ambao changamoto hizi kwao wanaweza wakazigear on!!!!

 
Huyu Mayage Mayage ndio nani? Sijawahi kumsikia au kumsoma popote. Kama kuna mtu ana profile yake atumwagie hapa ili tuone kama ana sifa za kutosha kubishana na Dr wa ukweli.

Huyu ni kanjanja yuko analipwa na RA na EL wamempeleka Raia Mwama kimkakati
 
duniani kote imethibitika kuwa "the difference between ruling and oppistion parties is paper thin"
 
Mayange S Mayange yupo sahihi kwenye ili..

Ktk mijadala ya kipuuzi kama hii hua hukosekani,shame on you!Na huyo ni MAYAGE S. MAYAGE na si MAYANGE S. MAYANGE hiyo inaonyesha ni jinsi gani unavyopenda kudandia vya watu kama wale KINADADA WANAOJIUZA barabarani a.k.a CHANGUDOA.
 
Mayage kaingia Raia Mwema kwa kazi maalumu. Najua Mbwambo asingemkubali, sasa kama Mbwambo ni makamu Mwenyekiti na nina uhakika hakubaliana na Mayage. Je Mayage atakuwa kipitia mgongo wa nani?. Tukijua hili tutajua mambo mengi sana yaliyojificha nyuma ya pazia.
 
huo na wewe upotoshaji!!yawezekana kweli sina akili!!lakin kama ni ya darasani nina uhakika mkubwa hiyo ninayo!!tena wa 100%labda kwa vile wanasema zipo za darasani na za mtaani pengine huo upande wa pili nikawa sina!!!sijapinga yafanywayo!!!ninachokisema kwamba mapendekezo aliyotoa mayage yana tija!!ni ya kufuatwa!!!ukosoaji wake ni chama kujitizama tu!!!ila mimi nikaja na hoja nyingine nikasema kwamba tuna golden chance sasa katika siasa za nchi hii!!ila nikasema mwenyekiti wetu tangu ahachiwe na mh mtei,sasa yatosha ang'atuke!!maana si mtu sahihi wa kwenda naye 2015!!!na nikatoa baadhi ya sababu!!!!ni hayo tu!!!!na kwangu mjadala umefungwa!!!!
Hebu ainisha hapa matokeo mabaya ya Mbowe ktk chama kama mwenyekiti kwa kiasi cha wewe kusema sio mtu sahihi wa kwenda naye 2015. Una uhakika hauna kaudugu na Hamad Rashid kweli? coz mnafanana kimtazamo sana.
ANGALIZO: No research, no right to speak.
 
Back
Top Bottom